Utangulizi wa Sehemu ya 9
Hii sehemu itatusaidia kujua vijana, manabii, na wafalme wenye walionyesha kama wanamuamini kabisa Yehova. Mutoto mwanamuke Mwisraeli mwenye alikuwa anaishi Siria alikuwa hakika kama nabii wa Yehova angeweza kuponyesha Naamani. Nabii Elisha alikuwa hakika kama Yehova angemulinda kutokana na jeshi la maadui. Kuhani Mukubwa Yehoyada alitia uzima wake mu hatari juu ya kulinda mutoto Yehoashi, sababu Atalia, tate (nkambo) yake mwanamuke, mwenye alikuwa muovu sana, alitaka kumuua. Mufalme Hezekia alikuwa hakika kama Yehova ataokoa Yerusalemu, na hata wakati Waashuru walimuogopesha, hakujitia
mu mikono yao. Mufalme Yosia alitosha ibada ya sanamu mu inchi yote. Alitengeneza tena hekalu na alitia watu moyo waanze tena kumuabudu Yehova.KATIKA SEHEMU HII
SOMO LA 51
Mupiganaji-vita na Mutoto Mudogo Mwanamuke
Mutoto mwanamuke Mwisraeli alielezea bibi ya bwana mukubwa wake kuhusu nguvu za Yehova, na Naamani aliponyeshwa kwa njia ya muujiza.
SOMO LA 52
Jeshi la Yehova Lenye Farasi na Magari ya Vita ya Moto
Namna mutumishi wa Elisha aliona kwamba ‘wale wenye kuwa pamoja na sisi ni wengi kuliko wale wenye kuwa pamoja nao.’
SOMO LA 54
Yehova Alivumilia Yona
Ni jambo gani lilifanya nabii mumoja wa Mungu amezwe na samaki kubwa? Namna gani alitoka mu tumbo la ile samaki? Na Yehova alimufundisha nini?
SOMO LA 55
Malaika wa Yehova Alilinda Hezekia
Maadui wa Yuda walisema kama Yehova hatalinda watu wake, lakini walijidanganya!
SOMO LA 56
Yosia Alipenda Sheria ya Mungu
Yosia aliwekwa kuwa mufalme wakati alikuwa na miaka munane, na alisaidia watu wake wamuabudu Yehova.