Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Utangulizi wa Sehemu ya 10

Utangulizi wa Sehemu ya 10

Yehova ni Mfalme juu ya kila kitu. Sikuzote amekuwa na mamlaka juu ya kila kitu, naye ataendelea kuwa na mamlaka. Kwa mfano, Yeremia alipotupwa ndani ya shimo, Yehova alimwokoa ili asife. Alimwokoa Shadraki, Meshaki, na Abednego kutoka katika tanuru ya moto na akamwokoa Danieli kutoka katika midomo ya simba. Yehova alimlinda Esta ili aokoe taifa zima. Hataruhusu uovu uendelee milele. Unabii kuhusu ile sanamu kubwa na mti mkubwa unatoa uhakikisho kwamba hivi karibuni Ufalme wa Yehova utaondoa uovu wote na kutawala dunia.

KATIKA SEHEMU HII

Yehova Amtuma Yeremia Akahubiri

Mambo ambayo nabii huyu kijana alisema yaliwafanya wazee wa Yuda wakasirike sana.

Yerusalemu Laharibiwa

Watu wa Yuda waendelea kuabudu miungu ya uwongo, hivyo Yehova awaacha.

Wavulana Wanne Walimtii Yehova

Wavulana Wayudea waliazimia kubaki waaminifu kwa Yehova hata walipokuwa katika makao ya mfalme huko Babiloni.

Ufalme Ambao Utadumu Milele

Danieli aeleza maana ya ndoto ya ajabu ya Nebukadneza.

Hawakuinamia Sanamu

Shadraki, Meshaki, na Abednego wakataa kuabudu sanamu ya dhahabu ya mfalme wa Babiloni.

Ufalme Unaofananishwa na Mti Mkubwa

Ndoto ya Nebukadneza yatabiri wakati wake ujao.

Mwandiko Ukutani

Maandishi hayo ya ajabu yalitokea wakati gani, nayo yalimaanisha nini?

Danieli Ndani ya Shimo la Simba

Sali kwa Yehova kila siku, kama Danieli alivyofanya!

Esta Awaokoa Watu Wake

Ingawa alikuwa yatima kutoka nchi nyingine, baadaye alikuwa malkia.

Ezra Alifundisha Sheria ya Mungu

Baada ya Waisraeli kumsikiliza Ezra, walimtolea Mungu ahadi ya pekee.

Kuta za Yerusalemu

Nehemia alipogundua kwamba maadui wake walitaka kuwashambulia, kwa nini hakuogopa?