Utangulizi wa Sehemu ya 10
Yehova ni mukubwa kupita wafalme wote. Hakuna kitu chenye kimekwisha kumushinda, na hakuna kitu chenye kitamushindaka. Kwa mufano, wakati walitupa Yeremia mu shimo, Yehova alimuokoa ili asikufe. Aliokoa Shadraki, Meshaki, na Abednego kutoka katika tanuru ya moto na aliokoa Danieli ili simba wasimukule. Yehova alilinda Esta ili aokoe taifa lote. Hataacha mambo ya mubaya iendelee milele. Unabii wenye unazungumuzia sanamu kubwa na wenye unazungumuzia muti mukubwa unaonyesha kabisa kama karibuni Ufalme wa Yehova utatosha mambo yote ya mubaya na utatawala dunia.
KATIKA SEHEMU HII
SOMO LA 57
Yehova Anatuma Yeremia Aende Kuhubiri
Mambo yenye huyu nabii kijana alisema iliwafanya wazee wa Yuda wakasirike sana.
SOMO LA 58
Yerusalemu Inaharibiwa
Watu wa Yuda waliendelea kuabudu miungu ya uongo, njo maana Yehova aliwaacha.
SOMO LA 59
Vijana Ine Wenye Walimutii Yehova
Vijana Wayudea waliazimia kubakia waaminifu kwa Yehova hata wakati walikuwa mu nyumba ya mufalme kule Babiloni.
SOMO LA 60
Ufalme Wenye Utaendelea Milele
Danieli anafasiria maana ya ndoto ya kushangaza ya Nebukadneza.
SOMO LA 61
Walikataa Kuinamia Sanamu
Shadraki, Meshaki, na Abednego wanakataa kuabudu sanamu ya zahabu ya mufalme wa Babiloni.
SOMO LA 62
Ufalme Wenye Uko Sawa Muti Mukubwa
Ndoto ya Nebukadneza inaonyesha mambo yenye itamupata.
SOMO LA 63
Maneno Inaandikwa Kwenye Ukuta
Maneno yenye haieleweke inaandikwa ku ukuta wakati gani, na inamaanisha nini?
SOMO LA 64
Danieli Anatupwa Ndani ya Shimo la Simba
Ukuwe unasali kwa Yehova kila siku, sawa vile Danieli alikuwa anafanya!
SOMO LA 65
Esta Anaokoa Watu Wake
Hata kama alikuwa yatima kutoka inchi ingine, alifikia kuwa malkia.
SOMO LA 66
Ezra Alifundisha Watu Sheria ya Mungu
Kisha Waisraeli kumusikiliza Ezra, walimutolea Mungu ahadi fulani ya pekee.
SOMO LA 67
Kuta za Yerusalemu
Wakati Nehemia alivumbua kama maadui wake walitaka kuwashambulia, juu ya nini hakuogopa?