Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Utangulizi wa Sehemu ya 11

Utangulizi wa Sehemu ya 11

Hii sehemu itakusaidia ujue mambo yenye kuzungumuziwa mu Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Yesu alizaliwa mu familia ya hali ya chini na waliishi katika muji mudogo. Alifanya kazi na baba yake, mwenye alikuwa seremala. Yesu njo angeokoa wanadamu. Yehova alimuchagua ili akuwe Mufalme wa Ufalme wa mbinguni. Kama uko muzazi, usaidie mutoto wako aelewe kama Yehova alichagua kwa uangalifu ni katika familia gani Yesu angekomalia. Umusaidie aelewe kama Yehova alilinda Yesu juu Herode asimuue, na umusaidie aelewe kama hakuna kitu kinaweza kumuzuia Mungu kutimiza kusudi lake. Umuonyeshe kama Yehova alipatiaka Yohana kazi ya kutayarisha njia kwa ajili ya kuja kwa Yesu. Umufasirie muzuri namna Yesu alionyesha kama alikuwa anapenda mashauri yenye hekima ya Yehova tangu wakati alikuwa mutoto.

KATIKA SEHEMU HII

SOMO LA 68

Elizabeti Anakuwa na Mutoto

Juu ya nini bwana ya Elizabeti aliambiwa kwamba hangeweza tena kusema mupaka wakati mutoto atazaliwa?

SOMO LA 69

Gabrieli Anatembelea Maria

Alimupatia ujumbe wenye ulibadilisha maisha yake.

SOMO LA 70

Malaika Wanatangaza Kama Yesu Amezaliwa

Wachungaji wenye walisikia ile tangazo walitenda haraka.

SOMO LA 71

Yehova Alimulinda Yesu

Mufalme muovu alitaka kuua Yesu.

SOMO LA 72

Wakati Yesu Alikuwa na Miaka 12

Namna gani Yesu alishangaza walimu mu hekalu?

SOMO LA 73

Yohana Anatayarisha Kuja kwa Masiya

Wakati Yohana alikomaa, akakuwa nabii. Alifundisha kama Masiya anakaribia kuja. Watu walifanya nini wakati walisikia mafundisho yake?