Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Utangulizi wa Sehemu ya 12

Utangulizi wa Sehemu ya 12

Yesu aliwafundisha watu kuhusu Ufalme wa mbinguni. Pia aliwafundisha kusali jina la Mungu litakaswe, Ufalme wake uje, na mapenzi yake yatendeke duniani. Ikiwa wewe ni mzazi, mweleze mtoto wako sala hiyo inamaanisha nini kwetu. Yesu hakumruhusu Shetani amfanye avunje ushikamanifu wake. Yesu aliwachagua mitume wake, nao wakafanyiza msingi wa Ufalme. Ona jinsi Yesu alivyokuwa na bidii kwa ajili ya ibada safi. Kwa kuwa alitaka kuwasaidia watu, Yesu aliponya wagonjwa, akalisha wenye njaa, na hata akawafanya watu wawe hai tena. Kupitia miujiza hiyo yote, alionyesha kile ambacho Ufalme utawafanyia wanadamu.

KATIKA SEHEMU HII

Yesu Anakuwa Masihi

Yohana anamaanisha nini anaposema kwamba Yesu ndiye Mwana-Kondoo wa Mungu?

Ibilisi Anamjaribu Yesu

Ibilisi anamjaribu Yesu mara tatu. Vishawishi hivyo vitatu ni nini? Yesu anatendaje?

Yesu Analisafisha Hekalu

Kwa nini Yesu anawafukuza wanyama nje ya hekalu na kupindua meza za wanaobadili pesa?

Mwanamke Kisimani

Mwanamke Msamaria anashangaa kamba Yesu anazungumza naye. Kwa nini? Yesu anamwambia jambo gani ambalo hakuwa amemwambia mtu mwingine yeyote?

Yesu Anahubiri Ujumbe wa Ufalme

Yesu anawaalika baadhi ya wanafunzi wake wawe ‘wavuvi wa watu.’ Baadaye, anawazoeza 70 kati ya wafuasi wake kuhubiri habari njema.

Yesu Anafanya Miujiza Mingi

Popote anapoenda, wagonjwa wanamfikia ili awasaidie, naye anawaponya wote. Hata anamfufua msichana mdogo.

Yesu Anachagua Mitume Kumi na Wawili

Kwa nini Yesu anawachagua? Je, unakumbuka majina yao?

Mahubiri ya Mlimani

Yesu aliufundisha umati uliokusanyika mambo muhimu sana.

Yesu Anawafundisha Wanafunzi Wake Jinsi ya Kusali

Yesu aliwaambia wanafunzi wake waendelee kuomba mambo gani?

Yesu Analisha Maelfu ya Watu

Muujiza huo unatufundisha nini kuhusu Yehova na Yesu?

Yesu Anatembea Juu ya Maji

Je, unaweza kuwazia jinsi ambavyo mitume walihisi walipoona muujiza huo?

Yesu Aponya Siku ya Sabato

Kwa nini si watu wote waliofurahishwa na mambo ambayo Yesu alifanya?

Yesu Amfufua Lazaro

Yesu alipomwona Maria akilia, yeye pia alianza kulia. Hata hivyo huzuni yao ikageuka na kuwa shangwe.