Utangulizi wa Sehemu ya 12
Yesu alifundisha watu juu ya Ufalme wa mbinguni. Tena aliwaambia kama inafaa wakuwe wanasali jina la Mungu litakaswe, Ufalme wake ukuje, na mapenzi yake ifanyike ku dunia. Kama uko muzazi, saidia mutoto wako aelewe juu ya nini ile sala ni ya maana kwetu. Yesu hakuruhusu Shetani amufanye avunje ushikamanifu wake. Mitume, wenye Yesu alichaguaka njo washiriki wa kwanza wa Ufalme, na wako na kazi ya maana sana katika ule Ufalme. Onyesha mutoto wako kama Yesu alikuwa na bidii kwa ajili ya ibada safi. Kwa sababu alitaka kusaidia watu, Yesu aliponyesha wagonjwa, alipatia wenye kuwa na njaa chakula, na hata
alifufua wafu. Kwa kufanya vile, alionyesha mambo yenye Ufalme utafanyia wanadamu.KATIKA SEHEMU HII
SOMO LA 74
Yesu Anakuwa Masiya
Yohana anamaanisha nini wakati anasema kama Yesu njo Mwana-Kondoo wa Mungu?
SOMO LA 75
Ibilisi Anamujaribu Yesu
Ibilisi anamujaribu Yesu mara tatu. Anamujaribu namna gani? Yesu anatenda namna gani?
SOMO LA 76
Yesu Anasafisha Hekalu
Juu ya nini Yesu anafukuza wanyama inje ya hekalu na kupindua meza za wenye wako wanabadilisha feza?
SOMO LA 77
Mwanamuke Kwenye Kisima
Mwanamuke Musamaria anashangaa wakati Yesu anazungumuza naye. Juu ya nini? Yesu anamuambia jambo gani lenye alikuwa hajaambiaka mutu mwingine?
SOMO LA 78
Yesu Anahubiri Habari ya Ufalme
Yesu anaalika wanafunzi wake fulani wakuwe ‘wavuvi wa watu.’ Kisha, anachagua wafuasi 70 ili wahubiri habari njema.
SOMO LA 79
Yesu Anafanya Miujiza Mingi
Kila fasi kwenye Yesu anaenda, wagonjwa wanakuja kumuona juu awasaidie, na anawaponyesha. Hata anamufufua mutoto mwanamuke.
SOMO LA 81
Mahubiri Kwenye Mulima
Yesu anafundisha watu mingi wenye walikusanyika pembeni ya mulima mambo ya maana sana.
SOMO LA 82
Yesu Anafundisha Wanafunzi Wake Namna ya Kusali
Yesu anawaambia wanafunzi wake waendelee kuomba mambo gani?
SOMO LA 84
Yesu Anatembea Juu ya Maji
Unaweza kuwazia namna mitume wanajisikia wakati wanaona ule muujiza?
SOMO LA 85
Yesu Anaponyesha Mutu Siku ya Sabato
Juu ya nini haiko watu wote njo wanafurahia mambo yenye Yesu iko anafanya?
SOMO LA 86
Yesu Anamufufua Lazaro
Wakati Yesu anaona namna Maria iko analia, yeye pia anaanza kulia. Lakini huzuni yao iligeuka kuwa furaha.