Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Utangulizi wa Sehemu ya 13

Utangulizi wa Sehemu ya 13

Yesu alikuja ku dunia ili atoe uzima wake kwa ajili ya wanadamu wenye hawakamilike. Hata kama alikufa, alishinda ulimwengu. Yehova alikuwa mushikamanifu kwa Mwana wake na alimufufua. Wakati alikuwa muzima hapa ku dunia, Yesu alitumikia watu kwa unyenyekevu na kuwasamehe wakati walimukosea. Kisha kufufuliwa, Yesu alitokea wanafunzi wake. Aliwafundisha kufanya kazi ya maana sana yenye aliwapatia. Kama uko muzazi, saidia mutoto wako aelewe kama sisi pia tunapaswa kufanya ile kazi leo.

KATIKA SEHEMU HII

SOMO LA 87

Pasaka ya Mwisho ya Yesu

Yesu anapatia mitume wake maagizo ya maana wakati iko anakula chakula pamoja nao kwa mara ya mwisho.

SOMO LA 88

Yesu Anakamatwa

Yuda Iskariote anaongoza watu mingi wenye wako na fimbo na mipanga juu wamukamate Yesu.

SOMO LA 89

Petro Anamukana Yesu

Ni nini ilifanyika mu kiwanja cha nyumba ya Kayafa? Namna gani walitendea Yesu ndani ya nyumba?

SOMO LA 90

Yesu Anakufa Kule Golgota

Juu ya nini Pilato anaruhusu Yesu auawe?

SOMO YA 91

Yesu Anafufuliwa

Ni mambo gani ya kufurahisha ilitokea kisha Yesu kuuawa?

SOMO LA 92

Yesu Anawatokea Wavuvi

Anafanya nini ili wamutambue?

SOMO LA 93

Yesu Anarudia Mbinguni

Lakini mbele ya kurudia, anapatia wanafunzi wake maagizo fulani ya maana sana.