Utangulizi wa Sehemu ya 13
Yesu alikuja ku dunia ili atoe uzima wake kwa ajili ya wanadamu wenye hawakamilike. Hata kama alikufa, alishinda ulimwengu. Yehova alikuwa mushikamanifu kwa Mwana wake na alimufufua. Wakati alikuwa muzima hapa ku dunia, Yesu alitumikia watu kwa unyenyekevu na kuwasamehe wakati walimukosea. Kisha kufufuliwa, Yesu alitokea wanafunzi wake. Aliwafundisha kufanya kazi ya maana sana yenye aliwapatia. Kama uko muzazi, saidia mutoto wako aelewe kama sisi pia tunapaswa kufanya ile kazi leo.
KATIKA SEHEMU HII
SOMO LA 87
Pasaka ya Mwisho ya Yesu
Yesu anapatia mitume wake maagizo ya maana wakati iko anakula chakula pamoja nao kwa mara ya mwisho.
SOMO LA 88
Yesu Anakamatwa
Yuda Iskariote anaongoza watu mingi wenye wako na fimbo na mipanga juu wamukamate Yesu.
SOMO LA 89
Petro Anamukana Yesu
Ni nini ilifanyika mu kiwanja cha nyumba ya Kayafa? Namna gani walitendea Yesu ndani ya nyumba?
SOMO LA 93
Yesu Anarudia Mbinguni
Lakini mbele ya kurudia, anapatia wanafunzi wake maagizo fulani ya maana sana.