Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Utangulizi wa Sehemu ya 14

Utangulizi wa Sehemu ya 14

Wakristo wa karne ya kwanza walieneza habari njema ya Ufalme mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia. Yesu aliwaelekeza mahali pa kuhubiri na akawawezesha kimuujiza kuwafundisha watu katika lugha zao wenyewe. Yehova aliwapa ujasiri na nguvu za kushinda mateso makali.

Yesu alimpa mtume Yohana maono ya utukufu wa Yehova. Katika maono mengine, Yohana aliona Ufalme wa mbinguni ukimshinda Shetani na kukomesha utawala wake milele. Yohana alimwona Yesu akitawala akiwa Mfalme pamoja na watawala wenzake 144,000. Pia, Yohana aliona dunia yote ikigeuzwa kuwa paradiso ambapo watu wote wanamwabudu Yehova kwa amani na umoja.

KATIKA SEHEMU HII

Wanafunzi Wapokea Roho Takatifu

Roho takatifu iliwapatia nguvu gani kimuujiza?

Hawakuvunjwa Moyo na Kitu Chochote

Viongozi wa kidini waliofanya Yesu auawe, wajaribu kuwanyamazisha wanafunzi. Lakini hawawezi.

Yesu Amchagua Sauli

Sauli ni adui mkatili wa Wakristo, lakini angebadilika baada ya muda mfupi.

Kornelio Apokea Roho Takatifu

Kwa nini Mungu alimtuma Petro nyumbani kwa mwanamume huyo, ambaye si Myahudi?

Ukristo Waenea Katika Mataifa Mengi

Mtume Paulo na waandamani wenzake wamishonari waanza kuhubiri katika maeneo ya mbali.

Mlinzi wa Jela Ajifunza Kweli

Hadithi hii inahusuje roho mwovu, tetemeko la nchi, na upanga?

Paulo na Timotheo

Wanaume hao wawili walifanya kazi pamoja wakiwa marafiki na wafanyakazi wenzi.

Paulo Apelekwa Roma

Safari imejaa hatari, lakini hakuna hali yoyote ngumu inayoweza kumzuia mtume huyu.

Ufunuo kwa Yohana

Yesu alimpa mfululizo wa maoni kuhusu wakati ujao.

“Ufalme Wako na Uje”

Ufunuo kwa Yohana unaonyesha jinsi Ufalme wa Mungu utakavyobadili maisha duniani.