Utangulizi wa Sehemu ya 14
Wakristo wa karne ya kwanza walieneza habari njema ya Ufalme mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia. Yesu aliwaelekeza mahali pa kuhubiri na akawawezesha kimuujiza kuwafundisha watu katika lugha zao wenyewe. Yehova aliwapa ujasiri na nguvu za kushinda mateso makali.
Yesu alimpa mtume Yohana maono ya utukufu wa Yehova. Katika maono mengine, Yohana aliona Ufalme wa mbinguni ukimshinda Shetani na kukomesha utawala wake milele. Yohana alimwona Yesu akitawala akiwa Mfalme pamoja na watawala wenzake 144,000. Pia, Yohana aliona dunia yote ikigeuzwa kuwa paradiso ambapo watu wote wanamwabudu Yehova kwa amani na umoja.
KATIKA SEHEMU HII
Wanafunzi Wapokea Roho Takatifu
Roho takatifu iliwapatia nguvu gani kimuujiza?
Hawakuvunjwa Moyo na Kitu Chochote
Viongozi wa kidini waliofanya Yesu auawe, wajaribu kuwanyamazisha wanafunzi. Lakini hawawezi.
Yesu Amchagua Sauli
Sauli ni adui mkatili wa Wakristo, lakini angebadilika baada ya muda mfupi.
Kornelio Apokea Roho Takatifu
Kwa nini Mungu alimtuma Petro nyumbani kwa mwanamume huyo, ambaye si Myahudi?
Ukristo Waenea Katika Mataifa Mengi
Mtume Paulo na waandamani wenzake wamishonari waanza kuhubiri katika maeneo ya mbali.
Mlinzi wa Jela Ajifunza Kweli
Hadithi hii inahusuje roho mwovu, tetemeko la nchi, na upanga?
Paulo na Timotheo
Wanaume hao wawili walifanya kazi pamoja wakiwa marafiki na wafanyakazi wenzi.
Paulo Apelekwa Roma
Safari imejaa hatari, lakini hakuna hali yoyote ngumu inayoweza kumzuia mtume huyu.
Ufunuo kwa Yohana
Yesu alimpa mfululizo wa maoni kuhusu wakati ujao.
“Ufalme Wako na Uje”
Ufunuo kwa Yohana unaonyesha jinsi Ufalme wa Mungu utakavyobadili maisha duniani.