Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Utangulizi wa Sehemu ya 14

Utangulizi wa Sehemu ya 14

Wakristo wa wakati wa mitume walitangaza habari njema ya Ufalme mupaka sehemu ya mbali sana ya dunia. Yesu aliwaambia fasi kwenye walipaswa kuhubiri, na kupitia muujiza, akawapatia uwezo wa kufundisha watu mu luga zao wenyewe. Yehova aliwapatia uhodari na nguvu ya kupambana na mateso makali sana.

Yesu alimuonyesha mutume Yohana maono ya utukufu wa Yehova. Katika maono ingine, Yohana aliona namna Ufalme wa mbinguni unapata ushindi juu ya Shetani na kumaliza utawala wa Shetani milele. Yohana aliona Yesu iko anatawala pamoja na wenzake 144000. Tena, aliona dunia yote inakuwa paradiso. Na aliona wanadamu wote wanamuabudu Yehova katika amani na umoja.

KATIKA SEHEMU HII

SOMO LA 94

Wanafunzi Wanapokea Roho Takatifu

Roho takatifu iliwapatia nguvu gani kwa njia ya muujiza?

SOMO LA 95

Hakuna Kitu Kingeweza Kuwazuia Kuhubiri

Viongozi wa dini wenye walifanya Yesu auawe, wanajaribu sasa kunyamazisha wanafunzi. Lakini hawawezi.

SOMO LA 96

Yesu Anamuchagua Sauli

Sauli ni adui wa sana wa Wakristo, lakini iko karibu kubadilika.

SOMO LA 97

Kornelio Anapokea Roho Takatifu

Juu ya nini Mungu anamutuma Petro ku nyumba ya ule mwanaume , mwenye haiko Muyahudi?

SOMO LA 98

Ukristo Unaenea Katika Mataifa Mingi

Mutume Paulo na wamisionere wenzake wanaanza kuhubiri mu maeneo ya mbali.

SOMO LA 99

Mulinzi wa Gereza Anajifunza Kweli

Hii hadisi inahusu namna gani pepo muchafu, tetemeko la inchi, na upanga?

SOMO LA 100

Paulo na Timoteo

Wale wanaume wawili wanatumika pamoja, na walikuwa marafiki kwa miaka mingi.

SOMO LA 101

Paulo Anapelekwa Roma

Safari imejaa hatari, lakini hakuna tatizo lenye linaweza kumuzuia huyu mutume.

SOMO LA 102

Yohana Anapokea Ufunuo

Yesu anamuonyesha Yohana maono mingi juu ya wakati wenye kuja.

SOMO LA 103

‘Ufalme Wako Ukuje’

Ufunuo wenye Yohana alipewa unaonyesha namna Ufalme wa Mungu utabadilisha maisha ku dunia.