Utangulizi wa Sehemu ya 14
Wakristo wa wakati wa mitume walitangaza habari njema ya Ufalme mupaka sehemu ya mbali sana ya dunia. Yesu aliwaambia fasi kwenye walipaswa kuhubiri, na kupitia muujiza, akawapatia uwezo wa kufundisha watu mu luga zao wenyewe. Yehova aliwapatia uhodari na nguvu ya kupambana na mateso makali sana.
Yesu alimuonyesha mutume Yohana maono ya utukufu wa Yehova. Katika maono ingine, Yohana aliona namna Ufalme wa mbinguni unapata ushindi juu ya Shetani na kumaliza utawala wa Shetani milele. Yohana aliona Yesu iko anatawala pamoja na wenzake 144000. Tena, aliona dunia
yote inakuwa paradiso. Na aliona wanadamu wote wanamuabudu Yehova katika amani na umoja.KATIKA SEHEMU HII
SOMO LA 94
Wanafunzi Wanapokea Roho Takatifu
Roho takatifu iliwapatia nguvu gani kwa njia ya muujiza?
SOMO LA 95
Hakuna Kitu Kingeweza Kuwazuia Kuhubiri
Viongozi wa dini wenye walifanya Yesu auawe, wanajaribu sasa kunyamazisha wanafunzi. Lakini hawawezi.
SOMO LA 97
Kornelio Anapokea Roho Takatifu
Juu ya nini Mungu anamutuma Petro ku nyumba ya ule mwanaume , mwenye haiko Muyahudi?
SOMO LA 98
Ukristo Unaenea Katika Mataifa Mingi
Mutume Paulo na wamisionere wenzake wanaanza kuhubiri mu maeneo ya mbali.
SOMO LA 99
Mulinzi wa Gereza Anajifunza Kweli
Hii hadisi inahusu namna gani pepo muchafu, tetemeko la inchi, na upanga?
SOMO LA 100
Paulo na Timoteo
Wale wanaume wawili wanatumika pamoja, na walikuwa marafiki kwa miaka mingi.
SOMO LA 101
Paulo Anapelekwa Roma
Safari imejaa hatari, lakini hakuna tatizo lenye linaweza kumuzuia huyu mutume.
SOMO LA 103
‘Ufalme Wako Ukuje’
Ufunuo wenye Yohana alipewa unaonyesha namna Ufalme wa Mungu utabadilisha maisha ku dunia.