WIMBO NA. 2
Jina Lako Ni Yehova
-
1. Mwenye enzi kuu—
Mungu uliye hai.
Milele na milele—
Wewe ni Yehova.
Tunajivunia,
Kuitwa watu wako.
Na duniani pote,
Tunakutangaza.
(KORASI)
Yehova, Yehova,
Wewe ndiye Mungu.
Mbinguni na duniani,
Hakuna mwingine.
Wewe ndiye mweza yote,
Wote watambue.
Yehova, Yehova,
Hakuna Mungu mwingine.
-
2. Unatuwezesha,
Kufanya upendalo,
Mapenzi yako wewe—
Wewe ni Yehova
Mashahidi wako,
Tunakuwakilisha.
Heshima kubwa sana—
Kuwa watu wako.
(KORASI)
Yehova, Yehova,
Wewe ndiye Mungu.
Mbinguni na duniani,
Hakuna mwingine.
Wewe ndiye mweza yote,
Wote watambue.
Yehova, Yehova,
Hakuna Mungu mwingine.
(Ona pia 2 Nya. 6:14; Zab. 72:19; Isa. 42:8.)