WIMBO 12
Yehova Ni Mungu Mukubwa
-
1. Mungu Mukubwa, unastahili
Kusifiwa milele,
uko mwenye upendo,
Mwenye hekima na mwenye haki.
Uko na nguvu mingi.
-
2. Tuko mavumbi, lakini weye
Unatusikiliza
wakati tunasali.
Unafundisha na kuongoza
Watu wako milele.
-
3. Tunakusifu kwa nyimbo zetu;
Na malaika nao
wote wanakusifu.
Mungu Mukubwa, mwenye huruma,
Pokea sifa zetu.
(Ona pia Kum. 32:4; Mez. 16:12; Mt. 6:10; Ufu. 4:11.)