Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 13

Kristo, Kielelezo Chetu

Kristo, Kielelezo Chetu

(1 Petro 2:21)

  1. 1. Yehova ni mwenye,

    upendo na mwema,

    Katoa Mwana wake wa Pekee

    Awe mwanadamu,

    kusudi tumwige

    Tulitukuze jina la Mungu

  2. 2. Neno la Yehova,

    lilimwimarisha.

    Kwake lilikuwa kama chakula.

    Kawa na hekima,

    ufahamu pia,

    Katuachia kielelezo

  3. 3. Kama Yesu Kristo,

    tumsifu Mungu

    Tuzifuate hatua za Yesu.

    Tumwige daima,

    maishani mwetu.

    Tutapata kibali cha Mungu.