Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

WIMBO 19

Chakula cha Mangaribi cha Bwana

Chakula cha Mangaribi cha Bwana

(Matayo 26:26-30)

  1. 1. Yehova Baba wa mbinguni,

    Leo siku takatifu!

    Zamani ulionyeshaka upendo,

    hekima, haki, na nguvu.

    Na damu ya mwana-kondoo

    Ililinda watu wako.

    Na kisha wakati Yesu akakufa

    Na kutimiza unabii.

  2. 2. Leo mukate na divai

    Vinatukumbusha Yesu,

    Na faida zote zenye tunapata

    Kupitia kifo yake.

    Leo siku ya Ukumbusho

    Tunamukumbuka Yesu,

    Mwenye alilipa bei ya ukombozi

    Ili tupate uzima.

  3. 3. Yehova tunakusanyika;

    Ulitualika hapa

    Ili tukusifu kwa upendo wako,

    Na kuheshimia Kristo.

    Ukumbusho unatufanya

    Tukuwe wenye shukrani.

    Basi tuige Kristo Mufalme wetu,

    Kusudi tuishi milele.