WIMBO 19
Chakula cha Mangaribi cha Bwana
-
1. Yehova Baba wa mbinguni,
Leo siku takatifu!
Zamani ulionyeshaka upendo,
hekima, haki, na nguvu.
Na damu ya mwana-kondoo
Ililinda watu wako.
Na kisha wakati Yesu akakufa
Na kutimiza unabii.
-
2. Leo mukate na divai
Vinatukumbusha Yesu,
Na faida zote zenye tunapata
Kupitia kifo yake.
Leo siku ya Ukumbusho
Tunamukumbuka Yesu,
Mwenye alilipa bei ya ukombozi
Ili tupate uzima.
-
3. Yehova tunakusanyika;
Ulitualika hapa
Ili tukusifu kwa upendo wako,
Na kuheshimia Kristo.
Ukumbusho unatufanya
Tukuwe wenye shukrani.
Basi tuige Kristo Mufalme wetu,
Kusudi tuishi milele.
(Ona pia Lu. 22:14-20; 1 Ko. 11:23-26.)