WIMBO NA. 24
Njooni Kwenye Mlima wa Yehova
-
1. Tazama uone,
Mlima wa Yehova.
Uko, juu zaidi,
Kuliko mingine.
Toka pande zote,
Watu wamiminika.
Nao waita wengi,
Wamwabudu Mungu.
Mdogo, mnyonge,
Atakuwa taifa kubwa.
Twapiga hatua,
Yehova anatubariki.
Umati mkubwa,
Unajiunga nasi.
Nao waukubali
Ufalme wa Mungu.
-
2. Agizo tunalo,
La kuhubiri Neno.
Nasi tunatangazia
wote Ufalme.
Kristo atawala,
Awahimiza wote.
Kote duniani
Wamsikie Yeye.
Neno la Yehova,
Linawafungulia njia.
Tunayo furaha,
Kuwasaidia wengine!
Sote tushiriki
Kwa kuwasaidia
Watu wajue Mungu
Wapate uzima.
(Ona pia Zab. 43:3; 99:9; Isa. 60:22; Mdo. 16:5.)