WIMBO 24
Tuende ku Mulima wa Yehova
-
1. Simama uone
Mulima wa Yehova,
Uko juu zaidi
Kupita ingine.
Watu wengi sana,
Kutoka fasi yote,
Wanaita wengine
Waabudu Mungu.
Sasa njo wakati
Mudogo kuwa elfu moja.
Na sasa Yehova
Anabariki kazi yake.
Watu wengi sana
Wanajitoa kwake.
Nao wanaitika
Utawala wake.
-
2. Yesu alisema
Tuhubirie wote
Habari njema ya
Ufalme wa Yehova.
Kristo anaomba
Watu watii Mungu.
Na wapole wanapenda
Neno ya Mungu.
Tuko na furaha
ya kusaidia wengine.
Wajue Yehova,
na kisha wapate uzima.
Basi tualike
Watu wote wakuye
Kwenye mulima wa
Yehova Mungu wetu.
(Ona pia Zb. 43:3; 99:9; Isa. 60:22; Mdo. 16:5.)