Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 33

Mtupie Yehova Mzigo Wako

Mtupie Yehova Mzigo Wako

(Zaburi 55)

  1. 1. Ee Yehova nakuomba,

    Usijifiche mbali.

    Sikiliza, unijibu,

    Ili nisiogope.

    (KORASI)

    Mtupie Yah mzigo;

    Naye atakutegemeza.

    Hataacha utikiswe,

    Atakuimarisha.

  2. 2. Kama ningekuwa njiwa,

    Ningeruka nyikani,

    Mbali na watu waovu,

    Watendao jeuri.

    (KORASI)

    Mtupie Yah mzigo;

    Naye atakutegemeza.

    Hataacha utikiswe,

    Atakuimarisha.

  3. 3. Yehova hutufariji,

    Na kutupa amani.

    Ijapo tunalemewa,

    Ana fadhili nyingi.

    (KORASI)

    Mtupie Yah mzigo;

    Naye atakutegemeza.

    Hataacha utikiswe,

    Atakuimarisha.