Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 38

Atakupa Nguvu

Atakupa Nguvu

(1 Petro 5:10)

  1. 1. Kweli yake Mungu amekufundisha,

    Amekutoa katika giza.

    Aliona moyo wako watamani,

    Kufanya mambo yaliyo mema.

    Kwa sala ulijiweka wakfu;

    Daima atakuimarisha.

    (KORASI)

    Kwa damu ya Mwanaye,

    alikununua.

    Hukuimarisha,

    na kukupa nguvu.

    Atakulinda na

    kukuongoza wewe.

    Hukuimarisha,

    na kukupa nguvu.

  2. 2. Katoa Mwanaye, kwa niaba yako;

    Hivyo, ataka ufanikiwe.

    Basi kama Mungu alifanya hivyo,

    Bila shaka atakupa nguvu.

    Imani yako hatasahau;

    Walio wake atawatunza.

    (KORASI)

    Kwa damu ya Mwanaye,

    alikununua.

    Hukuimarisha,

    na kukupa nguvu.

    Atakulinda na

    kukuongoza wewe.

    Hukuimarisha,

    na kukupa nguvu.