WIMBO NA. 42
Sala ya Mtumishi wa Mungu
-
1. Baba Yetu, Mwenye Enzi Kuu,
Jina lako litakaswe milele;
Mapenzi yako yatimizwe.
Tunakuomba, Ufalme uje.
Utakapoagiza,
Baraka tuzione.
-
2. Twashukuru kwa baraka zako,
Unatupa zawadi nyingi njema.
Chanzo cha uhai na nuru,
Watupa hekima, ufahamu.
Twashukuru daima,
Twakusifu Yehova.
-
3. Ulimwengu una dhiki nyingi.
Tufariji tunakutegemea.
Tunakutupia mizigo.
Tupe nguvu za kusonga mbele.
Tufanye upendayo,
Tutimize nadhiri.
(Ona pia Zab. 36:9; 50:14; Yoh 16:33; Yak. 1:5.)