Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 44

Sala ya Mtu wa Hali ya Chini

Sala ya Mtu wa Hali ya Chini

(Zaburi 4:1)

  1. 1. Yehova nakuomba:

    ‘Sala yangu sikia.’

    Vidonda vyangu haviponi;

    ninalemewa.

    Nimevunjika moyo

    na kukata tamaa.

    Yehova Mungu wa faraja,

    ninakusihi.

    (KORASI)

    Niinue; nipe nguvu.

    Nifariji, Niongoze.

    Naja kwako. Ee Yehova,

    Mungu wangu, Nguvu zangu.

  2. 2. Neno lako lanifariji,

    lanipa nguvu.

    Lafunua hisia zangu

    za ndani sana.

    Niwezeshe kulitumaini

    Neno lako.

    Wewe U mkuu kuliko

    mioyo yetu.

    (KORASI)

    Niinue; nipe nguvu.

    Nifariji, Niongoze.

    Naja kwako. Ee Yehova,

    Mungu wangu, Nguvu zangu.