Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 45

Kutafakari kwa Moyo Wangu

Kutafakari kwa Moyo Wangu

(Zaburi 19:14)

  1. 1. Mambo nitafakariyo;

    Nayo mawazo ya moyo,—

    Bwana, na yakupendeze,

    Nitembee nawe Bwana.

    Kila ninapolemewa,

    Nikosapo usingizi,

    Nikutafakari wewe,

    Na mambo yaliyo mema.

  2. 2. Mambo safi na ya kweli,

    Wema adili wowote,

    Mambo yasemwayo vema—

    Niyatafakari hayo

    Mawazo yako ni bora!

    Kamwe hayahesabiki.

    Mungu nitatafakari,

    Neno Lako sikuzote.