WIMBO 48
Tutembee na Yehova Kila Siku
(Mika 6:8)
-
1. Tutembee na Yehova;
Na tujishushe mbele yake.
Kama tunamutafuta
Atatuonyesha fazili!
Sababu anatupenda,
Tutatembea naye.
Na tunajitoa kwake;
Tumutumikie yeye.
-
2. Mu siku hizi za mwisho,
Shetani anakasirika.
Iko natutesa sana
Ili tumuache Yehova.
Lakini tujue kama
Mungu atatulinda.
Basi tumutumikie
na kumupenda milele.
-
3. Yah anatusaidia
Kwa kutumia roho yake,
Pia Biblia na sala,
Na kutaniko ya Kikristo.
Tukifurahisha Mungu,
Atatusaidia
Tukuwe waaminifu
Na kuwa wenye kiasi.
(Ona pia Mwa. 5:24; 6:9; 1 Fa. 2:3, 4.)