WIMBO 52
Kujitoa na Kubatizwa
-
1. Ni Yehova aliumba
Ulimwengu wote.
Mbingu, dunia, bahari,
Na vitu vingine.
Alituumba na siye
Kwa upendo wake.
Kwa hiyo, tumusifu yeye,
Tena tumuabudu.
-
2. Wakati alibatizwa,
Yesu alisali:
‘Najitoa kwako baba
Nikutumikie.’
Na kisha njo akakuwa
Mutiwa-mafuta,
Na alimutii Yehova
Maisha yake yote.
-
3. Baba ninakuya kwako
Ili kukusifu.
Na ninajitoa kwako,
Nikutumikie.
Ulitoa Mwana wako;
Ni zawadi kubwa.
Na miye ninakutolea
Maisha yangu yote.
(Ona pia Mt. 16:24; Mk. 8:34; Lu. 9:23.)