WIMBO NA. 59
Msifu Yah Pamoja Nami
-
1. Tusifu Yah;
Tumwimbie!
Uhai na vyote anatupa.
Kila siku,
Tumsifu.
Ana upendo na nguvu nyingi.
Tumwimbie na kumtukuza.
-
2. Tusifu Yah,
Hutujali.
Husikiliza maombi yetu.
Huinua
Wadhaifu;
Roho yake huwaimarisha.
Jina lake na tulitangaze.
-
3. Tusifu Yah.
Mungu wetu;
Hutufariji kukiwa shida.
Husamehe;
Na kuponya.
Baraka anatumiminia.
Njooni tumsifu kwa shangwe!
(Ona pia Zab. 94:18, 19; 145:21; 147:1; 150:2; Mdo. 17:25.)