WIMBO 63
Tuko Mashahidi wa Yehova
-
1. Watu wanaabudu
Sanamu na majiwe.
Mungu Mweza-Yote,
Hawamujue.
Ile miungu yote
Haiwezi kuona,
Tena haina mashahidi
Sababu ni ya uongo.
(REFREE)
Siye njo Mashahidi
wa kweli wa Yehova.
Mungu wetu akitabiri
Lazima atimize.
-
2. Tuko tunafundisha
Watu jina ya Mungu,
Na tunahubiri
Habari njema.
Tunawasaidia
Wajue kweli yake,
Kusudi wapate uhuru,
Na wamusifu milele.
(REFREE)
Siye njo Mashahidi
wa kweli wa Yehova.
Mungu wetu akitabiri
Lazima atimize.
-
3. Tukifundisha watu
Tunaheshimu Mungu.
Tunahubiria
Watu wabaya.
Kama tu wanatubu,
Yah atawasamehe.
Kama wanamutumikia
Njo watapata uzima.
(REFREE)
Siye njo Mashahidi
wa kweli wa Yehova.
Mungu wetu akitabiri
Lazima atimize.
(Ona pia Isa. 37:19; 55:11; Eze. 3:19.)