WIMBO NA. 64
Kuyashiriki Mavuno kwa Furaha
-
1. Twaishi siku za mavuno,
Pendeleo kubwa sana.
Mashamba ya ngano tayari,
Twashiriki kuyavuna.
Kristo ameweka mfano;
Anaelekeza kazi.
Tuna pendeleo kubwa sana,
Tufanye kazi ya Bwana.
-
2. Mungu, jirani, tukipenda,
Tutachochewa kutenda.
Tuna kazi muhimu sana,
Mwisho u karibu sana.
Tuzidipo kufanya kazi,
Tutakuwa na furaha.
Kazi ya Ufalme tushiriki,
Mungu atatubariki.
(Ona pia Mt. 24:13; 1 Kor. 3:9; 2 Tim. 4:2.)