Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 64

Kuyashiriki Mavuno kwa Furaha

Kuyashiriki Mavuno kwa Furaha

(Mathayo 13:1-23)

  1. 1. Twaishi siku za mavuno,

    Pendeleo kubwa sana.

    Mashamba ya ngano tayari,

    Twashiriki kuyavuna.

    Kristo ameweka mfano;

    Anaelekeza kazi.

    Tuna pendeleo kubwa sana,

    Tufanye kazi ya Bwana.

  2. 2. Mungu, jirani, tukipenda,

    Tutachochewa kutenda.

    Tuna kazi muhimu sana,

    Mwisho u karibu sana.

    Tuzidipo kufanya kazi,

    Tutakuwa na furaha.

    Kazi ya Ufalme tushiriki,

    Mungu atatubariki.