WIMBO NA. 71
Sisi Ni Jeshi la Yehova!
-
1. Sisi ni jeshi lake,
Yehova Mungu,
Ambalo latangaza,
Ufalme wa Mungu.
Yesu anatawala,
Ndiye Mfalme.
Tumejitolea
Pasipo woga.
(KORASI)
Sisi ni jeshi lake,
Yehova Mungu,
Twatangaza kwamba
“Anatawala.”
-
2. Sisi ni watumishi
Wake Yehova.
Twatafuta kondoo
Wanaougua.
Na chakula kuwapa
Bila kuchoka;
Tuwakaribishe
Mikutanoni.
(KORASI)
Sisi ni jeshi lake,
Yehova Mungu,
Twatangaza kwamba
“Anatawala.”
-
3. Jeshi lake Yehova
Latii Kristo,
Na tayari kwa vita,
Likiwa imara.
Laonyesha busara,
Na ujasiri.
Licha ya hatari,
Liko imara.
(KORASI)
Sisi ni jeshi lake,
Yehova Mungu,
Twatangaza kwamba
“Anatawala.”