WIMBO NA. 78
Kufundisha Neno la Mungu
-
1. Tuwafundishapo watu,
Neno lake Mungu.
Baraka tunazopata,
Hazina kifani.
Tunamwiga Kristo Yesu,
Alivyofundisha.
Tungependa tufundishao
Wawe rafikize.
-
2. Tukiwa walimu stadi
Tuweke mfano;
Waone unyofu wetu,
Tuangaze nuru.
Tuchunguze Maandiko,
Tuyatafakari.
Tujifunze ili tufunze
Na wengine pia.
-
3. Yehova hutuwezesha,
Kufundisha Neno.
Tukimwomba msaada,
Atatusikia.
Twalipenda Neno Lake,
Tunalithamini.
Tuwapende tuwafunzao
Wajiunge nasi.
(Ona pia Zab. 119:97; 2 Tim. 4:2; Tito 2:7; 1 Yoh. 5:14.)