Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 78

Kufundisha Neno la Mungu

Kufundisha Neno la Mungu

(Matendo 18:11)

  1. 1. Tuwafundishapo watu,

    Neno lake Mungu.

    Baraka tunazopata,

    Hazina kifani.

    Tunamwiga Kristo Yesu,

    Alivyofundisha.

    Tungependa tufundishao

    Wawe rafikize.

  2. 2. Tukiwa walimu stadi

    Tuweke mfano;

    Waone unyofu wetu,

    Tuangaze nuru.

    Tuchunguze Maandiko,

    Tuyatafakari.

    Tujifunze ili tufunze

    Na wengine pia.

  3. 3. Yehova hutuwezesha,

    Kufundisha Neno.

    Tukimwomba msaada,

    Atatusikia.

    Twalipenda Neno Lake,

    Tunalithamini.

    Tuwapende tuwafunzao

    Wajiunge nasi.