WIMBO 78
‘Kufundisha Neno ya Mungu’
-
1. Wakati tunafundisha
Neno ya Yehova,
Anatubariki sana.
Tuko na furaha.
Tunajikaza kuiga
Upendo wa Kristo,
Wakati tunafundisha
Watu kuhusu Mungu.
-
2. Siye wenye kufundisha
Tunatii Mungu,
Ili kwa matendo yetu
Watu wamusifu.
Tunaipenda Biblia
na tunaisoma,
Ili tuielewe
Na kufundisha wengine.
-
3. Wakati tunafundisha,
Tumuombe Mungu
Atupatie hekima
Na atuongoze.
Tunapenda watu wote
Na kuwafundisha,
Ili nao pia
Wafundishe watu wengine.
(Ona pia Zb. 119:97; 2 Ti. 4:2; Tit. 2:7; 1 Yo. 5:14.)