WIMBO 87
Tunatiana Moyo ku Mikutano
-
1. Tuko naishi na watu wabaya
Wenye hawajue Mungu.
Tuko na lazima ya kuongozwa
Ili tuishi muzuri.
Mikutano inatusaidia
Tukuwe na tumaini;
Tunatiana moyo kwa maneno
Kusudi tuvumilie.
Hatutaacha kutii Yehova
Na kusaidia watu.
Ku mikutano tunajifunzaka
Kuipenda sana kweli.
-
2. Yehova anatujua muzuri,
Basi tumusikilize.
Kukusanyika na ndugu na dada,
Ni alama ya hekima.
Tunafundishwa kuogopa Mungu
Na kuonyesha imani.
Tunajua ndugu wanatupenda,
Na hatuko peke yetu.
Mbele ya dunia mupya kufika
Tusiache kukutana.
Ku mikutano njo tunajifunza
Hekima kutoka juu.
(Ona pia Zb. 37:18; 140:1; Mez. 18:1; Efe. 5:16; Yak. 3:17.)