Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 88

Nijulishe Njia Zako

Nijulishe Njia Zako

(Zaburi 25:4)

  1. 1. Tumekutanika, Yehova Mungu;

    Mwaliko wako twakubali.

    Na Neno lako latuangazia,

    Njia zako tunafundishwa.

    (KORASI)

    Nifundishe njia zako wewe;

    Nieleweshe hekima yako.

    Unitembeze katika kweli.

    Nami nipende sheria yako.

  2. 2. Hekima yako haina kifani;

    Hukumu zako ni za haki.

    Neno lako ni la ajabu sana.

    Maneno yako yanadumu.

    (KORASI)

    Nifundishe njia zako wewe;

    Nieleweshe hekima yako.

    Unitembeze katika kweli.

    Nami nipende sheria yako.