WIMBO NA. 98
Maandiko—Yaliongozwa na Roho ya Mungu
-
1. Neno la Mungu ni nuru.
Mungu twamshukuru.
Tutii na kufaulu.
Huwaweka watu huru.
-
2. Neno la Yehova Mungu,
Latufunza matakwa.
Hunyoosha mambo yote,
Na kututia nidhamu.
-
3. Tusomapo Maandiko,
Twaona badiliko.
Nasi twapata hekima,
Na zawadi ya uzima.
(Ona pia Zab. 119:105; Met. 4:13.)