WIMBO 100
Tukuwe Tayari Kukaribishana
-
1. Yehova Mungu haiko muchoyo.
Anasaidiaka watu wote.
Hamuime mutu mvua wala jua.
Anatupatia chakula.
Tukisaidia watu wengine,
Tunaiga Mungu mwenye upendo.
Na tuko hakika atatubariki
Kwa yote tuko tunafanya.
-
2. Kupatia watu kunaletaka
Baraka zenye hatukuwazia.
Basi tusiache kukaribishana;
Tufanye kama vile Lidia,
Na siye tuseme: ‘Karibu kwetu.’
Tuwape chakula na hata maji.
Kwa kweli Yehova hawezi sahau
Wenye upendo na huruma.
(Ona pia Mdo. 16:14, 15; Ro. 12:13; 1 Ti. 3:2; Ebr. 13:2; 1 Pe. 4:9.)