WIMBO 117
Tukomalishe Sifa ya Wema
-
1. Yehova unaonyesha
Wema kwa watu wote.
Na uko mutakatifu
Tena muaminifu.
Unatusamehe zambi
Bila kuhesabia.
Sifa na ibada yetu,
Baba ikufikie.
-
2. Tunaona wema wako
Kila siku Yehova.
Unasaidia watu
Wajifunze Biblia.
Mambo tuko najifunza
Ni ya lazima sana.
Tupatie roho yako
Ili ituongoze.
-
3. Yehova tunakuomba
Ili utubariki
Kwa yote tuko nafanya
Kwa ajili ya ndugu.
Na mu kila kutaniko
Na kila familia,
Yehova tusaidie
Tuonyeshane wema.
(Ona pia Zb. 103:10; Mk. 10:18; Gal. 5:22; Efe. 5:9.)