WIMBO NA. 125
“Wenye Furaha Ni Walio na Rehema! ”
-
1. Mungu ni mwenye rehema!
Hurehemu kwa kupenda.
Hupendezwa na fadhili.
Huturuzuku daima,
Tunapotubu twajua,
Husikia dua zetu.
Anajua tu dhaifu,
Naye anaturehemu.
-
2. Na tunapohuzunika,
Tumkoseapo Mungu.
Kristo alitufundisha
Tusali kwake Yehova:
‘Tusamehe dhambi zetu,
Tusamehevyo wengine.’
Mambo yatakuwa sawa,
Nasi tuwe na amani.
-
3. Tunaporehemu watu
Tuonyeshe ukarimu.
Hatutafuti pongezi,
Bali kwa moyo mweupe.
Mungu aonaye vyote,
Huona rehema zetu.
Waonyeshao rehema,
Wanampendeza Mungu.
(Ona pia Mt. 6:2-4, 12-14.)