Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

WIMBO NA. 136

Malipo Kamili Kutoka kwa Yehova

Malipo Kamili Kutoka kwa Yehova

(Ruthu 2:12)

  1. 1. Yehova ni mwaminifu, ajua,

    Kuna nyakati ambazo,

    Watumishi wake hupata shida,

    Ilitabiriwa kale.

    Ikiwa umeacha familia,

    Makao au rafiki,

    Utapata ndugu na dada sasa

    Na uzima wa milele.

    (KORASI)

    Yehova na akuthawabishe.

    Malipo kamili na akupe.

    Kimbilio upate kwake.

    Yehova kwa kweli; ni mwaminifu.

  2. 2. Nyakati nyingine tunalemewa,

    Au kuvunjika moyo.

    Nyakati nyingine yaonekana

    Kuwa hatuna uwezo.

    Mungu wa faraja yote Yehova,

    Husikia sala zetu.

    Tujapolemewa, Yehova Mungu,

    Hutuimarisha sana.

    (KORASI)

    Yehova na akuthawabishe.

    Malipo kamili na akupe.

    Kimbilio upate kwake.

    Yehova kwa kweli; ni mwaminifu.