WIMBO NA. 143
Endeleeni Kufanya Kazi, Kukesha, na Kusubiri
-
1. Mweka majira, nyakati,
Anayeitwa Yehova—
Wakati wa kutetewa,
Uko karibu sana.
(KORASI)
Endeleeni kufanya kazi,
Kesheni na kusubiri,
Baraka za Ufalme.
-
2. Wakati umeshawekwa,
Mwana wake yu tayari.
Kwa ajili ya pigano,
Dhidi ya wapinzani.
(KORASI)
Endeleeni kufanya kazi,
Kesheni na kusubiri,
Baraka za Ufalme.
-
3. Japo sote twaugua,
Tunasubiri kwa hamu.
Ije siku ya Yehova,
Tuachiliwe huru.
(KORASI)
Endeleeni kufanya kazi,
Kesheni na kusubiri,
Baraka za Ufalme.
(Ona pia Mt. 25:13; Luka 12:36.)