WIMBO 146
“Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya”
-
1. Mambo mingi inaonyesha kama
Sasa Yesu Kristo ni Mufalme.
Mbinguni sasa kuko furaha,
Kesho itakuwa ku dunia.
(REFREE)
Tutafurahi kabisa
Kuwa pamoja na Mungu.
Atatosha maumivu yote,
Na kifo hakitakuwa tena.
Ni yeye njo atafanya vitu
Vyote vikuwe vipya.
-
2. Yerusalemu Mupya inakuya,
Na bibi-harusi anakuya;
Alishapambwa na kupendeza,
Yehova anamupa mwangaza.
(REFREE)
Tutafurahi kabisa
Kuwa pamoja na Mungu.
Atatosha maumivu yote,
Na kifo hakitakuwa tena.
Ni yeye njo atafanya vitu
Vyote vikuwe vipya.
-
3. Ule muji utapendeza sana,
Milango yake haitafungwa.
Leo Mashahidi wa Yehova
Wanautangaza fasi yote.
(REFREE)
Tutafurahi kabisa
Kuwa pamoja na Mungu.
Atatosha maumivu yote,
Na kifo hakitakuwa tena.
Ni yeye njo atafanya vitu
Vyote vikuwe vipya.
(Ona pia Mt. 16:3; Ufu. 12:7-9; 21:23-25.)