Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 2

“Mungu Alikubali” Zawadi Zao

“Mungu Alikubali” Zawadi Zao

WAEBRANIA 11:4

WAZO KUBWA: Historia ya mupango wa Yehova kwa ajili ya ibada safi

1-3. (a) Tutazungumuzia maulizo gani? (b) Tutachunguza mambo gani ine ya musingi yenye ibada safi inaomba? (Ona picha ku mwanzo wa habari.)

ABELI anachunguza kwa uangalifu kundi lake. Amechunga wale wanyama kwa upendo tangu walizaliwa. Sasa, anachagua wanyama fulani, anawachinja, na kuwatoa kuwa zawadi kwa Mungu. Je, ile tendo ya ibada, yenye kutolewa na mwanadamu mwenye hakamilike, itakubaliwa na Yehova?

2 Mutume Paulo aliongozwa na roho ya Mungu kuandika hivi kuhusu Abeli: “Mungu alikubali zawadi zake.” Lakini, Yehova, alikataa toleo la Kaini. (Soma Waebrania 11:4.) Ile inatokeza maulizo yenye tunapaswa kufikiria. Juu ya nini Mungu alikubali ibada ya Abeli lakini hapana ya Kaini? Mifano ya Kaini na Abeli na ya wengine wenye kutajwa mu Waebrania sura ya 11 inaweza kutufundisha nini? Majibu ya ile maulizo itatusaidia tuelewe muzuri zaidi mambo yenye ibada safi inatia ndani.

3 Wakati tunazungumuzia kwa kifupi matukio kuanzia siku za Abeli mupaka siku za Ezekieli, ona mambo ine ya musingi yenye wakati inachangwa pamoja inafanya ibada ikubaliwe na Mungu: Mupokeaji anapaswa kuwa Yehova, hali ya ibada inapaswa kuwa ya muzuri, namna inatolewa inapaswa kuwa yenye kukubaliwa na Mungu, na nia ya muabudu inapaswa kuwa safi.

Juu ya Nini Ibada ya Kaini Ilikataliwa?

4, 5. Ni mambo gani yenye pengine ilisaidia Kaini aone kwamba alipaswa kumutolea Mungu zawadi yake?

4 Soma Mwanzo 4:2-5. Kaini alijua kama mupokeaji wa zawadi yake angekuwa Yehova. Kaini alikuwa na wakati na nafasi mingi za kujifunza juu ya Yehova. Pengine yeye na ndugu yake Abeli walikuwa karibu kueneza miaka 100 wakati walitoa zawadi zao. * Wakati walikuwa wanakomaa, wale vijana wawili walijua kuhusu bustani ya Edeni, pengine walikuwa wanaona kwa mbali ile shamba yenye mbolea. Bila shaka walikuwa wameona makerubi wenye walikuwa ku muingilio wa bustani juu ya kuzuia mutu yeyote asiingie ndani. (Mwa. 3:24) Inawezekana wazazi wa wale vijana waliwaambia kwamba Yehova aliumba kila kitu chenye uzima na kwamba kusudi lake la kwanza kwa ajili ya wanadamu lilikuwa tofauti na kile walikuwa wanaona ile wakati​—kuwa zaifu polepole na kufikia kufa. (Mwa. 1:24-28) Inawezekana kujua ile mambo kulisaidia Kaini aone kwamba alipaswa kumutolea Mungu zawadi yake.

5 Ni mambo gani ingine yenye pengine ilimuchochea Kaini atoe zabihu? Yehova alikuwa ametabiri kwamba kungetokea “uzao,” ao mutu fulani mwenye angeponda kichwa cha ule “nyoka” mwenye alimushawishi Eva afanye uamuzi mubaya sana. (Mwa. 3:4-6, 14, 15) Pengine, kwa sababu alikuwa muzaliwa wa kwanza, Kaini aliwaza kama ni yeye alikuwa “uzao” wenye uliahidiwa. (Mwa. 4:1) Zaidi ya ile, Yehova hakukuwa amekata uhusiano wote na wanadamu wenye zambi; hata kisha Adamu kufanya zambi, Mungu alizungumuza naye, inawezekana kupitia malaika. (Mwa. 3:8-10) Na Yehova alizungumuza na Kaini kisha yeye kutoa zabihu yake. (Mwa. 4:6) Bila shaka, Kaini alijua kwamba Yehova anastahili ibada.

6, 7. Je, zabihu ya Kaini na namna aliitoa haikukuwa ya muzuri? Fasiria.

6 Sasa, juu ya nini Yehova hakukubali toleo la Kaini? Je, zawadi yake haikukuwa mu hali ya muzuri? Biblia haiseme vile. Inasema tu kwamba Kaini alileta “mazao ya shamba.” Kisha wakati fulani, Yehova alionyesha mu Sheria yenye alipatia Musa kwamba zabihu ya vile ilikuwa yenye kukubalika. (Hes. 15:8, 9) Tena, fikiria hali za ile wakati. Mu ile kipindi, wanadamu walikuwa wanakula tu mimea. (Mwa. 1:29) Na kwa sababu udongo wenye kuwa inje ya Edeni ulikuwa umelaaniwa na Mungu, Kaini alifanya kazi ya jasho juu apate toleo lake. (Mwa. 3:17-19) Alitoa chakula chenye kinasaidia mutu aishi, chenye kilipatikana kwa jasho! Lakini, Yehova hakukubali toleo la Kaini.

7 Je, tunaweza kusema kama namna ile zawadi ilitolewa haikukuwa ya muzuri? Je, Kaini alishindwa kuitoa mu njia yenye kukubalika? Pengine hapana. Juu ya nini tunasema vile? Juu, wakati Yehova alikataa toleo la Kaini, Yeye hakusema kwamba ile toleo ilitolewa mubaya. Kwa kweli, Biblia haionyeshe namna Kaini na Abeli walitoa toleo lao. Sasa, shida ilikuwa nini?

Nia ya Kaini haikukuwa safi (Ona fungu la 8, 9)

8, 9. (a) Juu ya nini Yehova hakukubali Kaini na toleo lake? (b) Ni nini inakushangaza sana kuhusu habari yenye Biblia inatoa juu ya Kaini na Abeli?

8 Maneno ya Paulo yenye iliongozwa na roho ya Mungu, yenye aliandikia Waebrania, inaonyesha kwamba nia yenye ilimuchochea Kaini atoe toleo lake haikukuwa safi. Kaini alikosa imani. (Ebr. 11:4; 1 Yo. 3:11, 12) Njo maana Yehova hakukubali Kaini mwenyewe na pia toleo lake. (Mwa. 4:5-8) Yehova ni Baba mwenye upendo, kwa hiyo alijaribu kurekebisha mwana wake kwa upole. Lakini Kaini, alitupilia mbali mukono wa Yehova wenye ulitaka kumusaidia. Matendo ya mwili wenye haukamilike kama vile “uadui, mizozo, wivu” iliharibisha sana moyo wa mufano wa Kaini. (Gal. 5:19, 20) Moyo mubaya wa Kaini ulifanya sehemu zingine za muzuri za ibada yake kuwa bure. Mufano wake unatufundisha kwamba ibada safi inaomba mambo mingi zaidi ya kuonyesha kwa inje tu kama tunashikamana na Yehova.

9 Biblia inatuambia mambo mingi kuhusu Kaini​—tunasikia namna Yehova anazungumuza naye, tunasoma majibu yenye Kaini alitoa, na tunajifunza hata majina ya watoto wake na mambo fulani yenye walifanya. (Mwa. 4:17-24) Lakini kuhusu Abeli, hatuna habari kwamba alikuwa na watoto na hakuna maneno yenye alisema yenye imeandikwa mu Biblia. Hata hivyo, matendo ya Abeli ingali inasema na sisi leo. Namna gani?

Abeli Anaweka Mufano kwa Ajili ya Ibada Safi

10. Ni nini inaonyesha kama Abeli aliweka mufano muzuri kwa ajili ya ibada safi?

10 Abeli alimutolea Yehova toleo lake, akijua kwamba Yeye tu njo anastahili kuwa mupokeaji. Ile zawadi ilikuwa mu hali ya muzuri sana juu Abeli alichagua “wazaliwa wa kwanza wa kundi lake.” Hata kama Biblia haiseme kwamba aliwatoa ku mazabahu ao hapana, ni wazi kwamba namna alitoa zawadi yake ilikuwa yenye kukubalika. Lakini jambo lenye kupendeza kuhusu zawadi ya Abeli​—lenye lingali linatufundisha hata kama kumepita miaka karibu elfu sita—​ni nia yenye ilimuchochea atoe ile zawadi. Abeli alichochewa na imani katika Mungu na upendo wa kanuni za haki za Yehova. Tunajua vile namna gani?

Abeli alitimiza mambo ine ya musingi yenye ibada safi inaomba (Ona fungu la 10)

11. Juu ya nini Yesu alitaja Abeli kuwa mwenye haki?

11 Kwanza, fikiria mambo yenye Yesu alisema kuhusu Abeli, mutu mwenye alijua muzuri. Yesu alikuwa anaishi mbinguni wakati Abeli alikuwa anaishi duniani. Yesu alipendezwa sana na ule mwana wa Adamu. (Mez. 8:22, 30, 31; Yoh. 8:58; Kol. 1:15, 16) Kwa hiyo, Yesu alikuwa anatoa ushuhuda wa mambo yenye alijionea na macho yake wakati alitaja Abeli kuwa mwenye haki. (Mt. 23:35) Mutu mwenye haki ni ule mwenye anatambua kama Yehova njo anapaswa kuweka kanuni za mema na mabaya. Lakini mutu wa vile anafanya zaidi ya ile​—anaonyesha kwa maneno na matendo yake kwamba anakubali zile kanuni. (Linganisha na Luka 1:5, 6.) Inaomba wakati juu ya kufikia kujulikana kuwa mutu mwenye haki. Kwa hiyo, hata mbele ya kumutolea Mungu zawadi yake, Abeli alipaswa kujulikana kuwa mutu mwenye kuishi kulingana na kanuni za Yehova. Haikukuwa mwepesi kwake kufanya vile. Hatuwezi kusema kabisa kama kaka yake mukubwa alikuwa mufano muzuri kwake kwa sababu moyo wa Kaini ulifikia kuwa muovu. (1 Yo. 3:12) Mama ya Abeli alikosa kutii amri ya Mungu yenye kuwa wazi, na baba yake alimuasi Yehova, kwa kutaka kujiamulia mema na mabaya. (Mwa. 2:16, 17; 3:6) Bila shaka Abeli alionyesha uhodari mukubwa kwa kuchagua njia yenye ilikuwa tofauti na ile yenye familia yake ilifuata!

12. Kulikuwa tofauti gani kubwa kati ya Kaini na Abeli?

12 Pia, ona namna mutume Paulo alionyesha uhusiano wenye kuwa kati ya sifa ya imani na haki. Paulo aliandika: “Kwa imani Abeli alimutolea Mungu zabihu yenye samani kubwa kuliko ile ya Kaini, na kupitia imani hiyo alitolewa ushahidi kwamba alikuwa mwenye haki.” (Ebr. 11:4) Maneno ya Paulo inaonyesha kama, tofauti na Kaini, Abeli alichochewa na imani ya kutoka mu moyo na ya muda murefu katika Yehova na katika namna Yake ya kufanya mambo.

13. Mufano wa Abeli unatufundisha nini?

13 Mufano wa Abeli unatufundisha kama ibada safi inatoka tu mu moyo wenye nia safi​—moyo wenye kujaa imani katika Yehova na wenye kukubali kabisa kanuni zake za haki. Zaidi ya ile, tunajifunza kama ibada safi inaomba mambo mingi zaidi ya tendo moja tu la ushikamanifu kwa Mungu. Maisha yetu yote, ni kusema, mwenendo wetu wote, unapaswa kuwa safi.

Wazee wa Ukoo Wanafuata Mufano wa Abeli

14. Juu ya nini Yehova alikubali zawadi zenye zilitolewa na Noa, Abrahamu, na Yakobo?

14 Abeli alikuwa mutu wa kwanza mwenye hakamilike mwenye alimutolea Yehova ibada safi, lakini hakukuwa wa mwisho kabisa. Mutume Paulo alitaja wengine wenye walimuabudu Yehova mu njia yenye kukubalika​—wanaume kama vile Noa, Abrahamu, na Yakobo. (Soma Waebrania 11:7, 8, 17-21.) Wakati fulani wa maisha yao, kila mumoja wa wale wazee wa ukoo alimutolea Yehova zabihu, na Mungu alikubali zawadi zao. Juu ya nini? Juu, zaidi ya kufanya matendo fulani ya ushikamanifu kwa Mungu, kila mumoja wao alitimiza pia mambo yote ya musingi yenye ibada safi inaomba. Tufikirie mifano yao.

Zabihu za Noa zilionyesha waziwazi ni nani anastahili ibada (Ona fungu la 15, 16)

15, 16. Ni nini inaonyesha kama Noa alitimiza mambo ine ya musingi yenye ibada safi inaomba?

15 Noa alizaliwa miaka 126 tu kisha Adamu kufa; lakini, alikomalia mu dunia ya kuharibika kwa sababu ya ibada ya uongo. * (Mwa. 6:11) Kati ya familia zote zenye ziliishi juu ya dunia mbele ya Garika, Noa na familia yake tu njo walikuwa wanamutumikia Yehova mu njia yenye kukubalika. (2 Pe. 2:5) Kisha kuokoka Garika, moyo wa Noa ulimuchochea ajenge mazabahu, ya kwanza kutajwa mu Biblia, na ulimuchochea kumutolea Yehova zabihu. Kupitia ile tendo ya kutoka mu moyo, Noa alionyesha waziwazi familia yake na wanadamu wengine wenye wangetokana naye kwamba Yehova tu njo anastahili kuwa mupokeaji wa ibada. Kati ya wanyama wote wenye angeweza kutumia juu ya kutoa zabihu, Noa alichagua “wamoja kati ya wanyama wote wenye kuwa safi na wamoja kati ya viumbe vyote vyenye kuruka vyenye kuwa safi.” (Mwa. 8:20) Wale wanyama walikuwa matoleo ya hali ya muzuri sana kwa sababu Yehova mwenyewe alikuwa amesema kwamba wako safi.​—Mwa. 7:2.

16 Noa alitoa zile zabihu za kuteketezwa ku mazabahu yenye alijenga. Je, namna ile ibada ilitolewa ilikuwa yenye kukubalika? Ndiyo. Biblia inasema kama Yehova alifurahia harufu ya ile toleo na kisha alibariki Noa na wana wake. (Mwa. 8:21; 9:1) Lakini, Yehova alikubali ile toleo zaidi sana kwa sababu ya nia yenye ilichochea Noa kutoa. Zile zabihu zilionyesha zaidi sana kwamba Noa alikuwa na imani yenye nguvu katika Yehova na katika namna Yake ya kufanya mambo. Kwa sababu Noa alimutii Yehova kila siku na alishika kanuni Zake, Biblia inasema kama “alitembea pamoja na Mungu wa kweli.” Kwa hiyo, Noa aliendelea kujulikana kuwa mwenye haki.​—Mwa. 6:9; Eze. 14:14; Ebr. 11:7.

17, 18. Ni nini inaonyesha kama Abrahamu alitimiza mambo ine ya musingi yenye ibada safi inaomba?

17 Abrahamu alizungukwa na ibada ya uongo. Mu muji wa Uru, kwenye Abrahamu alikuwa anaishi, kulikuwa hekalu kwa ajili ya mungu-mwezi mwenye kuitwa Nanna. * Hata baba ya Abrahamu aliabudu miungu ya uongo wakati fulani. (Yos. 24:2) Lakini, Abrahamu alichagua kumuabudu Yehova. Inawezekana alijifunza juu ya Mungu wa kweli kutoka kwa babu yake Shemu, mumoja wa wana wa Noa. Waliishi mu kipindi kimoja kwa miaka 150 hivi.

18 Mu maisha yake yote, Abrahamu alitoa zabihu mingi. Lakini sikuzote matendo yake ya ibada ilitolewa kwa ule mupokeaji tu mwenye kustahili, ni kusema, Yehova. (Mwa. 12:8; 13:18; 15:8-10) Je, Abrahamu alipenda kumutolea Yehova toleo lenye kuwa mu hali ya muzuri kabisa? Ile ulizo ilijibiwa kabisa wakati Abrahamu alionyesha kama iko tayari kutoa mwana wake mupendwa, Isaka, kuwa zabihu. Ile wakati, Yehova alimuonyesha waziwazi namna alipaswa kutoa ile zabihu. (Mwa. 22:1, 2) Na Abrahamu alikuwa tayari kufuata ile muongozo bila kuacha hata nukta moja. Yehova njo aliambia Abrahamu asiue mwana wake. (Mwa. 22:9-12) Yehova alikubali matendo ya ibada ya Abrahamu kwa sababu ilitolewa na mutu mwenye nia safi. Paulo aliandika: “Abrahamu alikuwa na imani katika Yehova, na hilo likahesabiwa kwake kuwa haki.”​—Ro. 4:3.

Yakobo aliwekea familia yake mufano muzuri (Ona fungu la 19, 20)

19, 20. Ni nini inaonyesha kama Yakobo alitimiza mambo ine ya musingi yenye ibada safi inaomba?

19 Yakobo aliishi sana Kanaani, inchi yenye Yehova alikuwa ameahidi Abrahamu na wazao wake. (Mwa. 17:1, 8) Ilikuwa fasi kwenye watu walikuwa wamejiingiza mu ibada yenye kupotoka sana mupaka Yehova akasema kwamba ile inchi “itatapika wakaaji wake.” (Law. 18:24, 25) Wakati alieneza miaka 77, Yakobo alitoka Kanaani, akaoa, na kisha kipindi fulani, akarudia kule pamoja na familia kubwa. (Mwa. 28:1, 2; 33:18) Lakini, wamoja mu familia yake walikuwa wameambukizwa na ibada ya uongo. Hata hivyo, wakati Yehova aliomba Yakobo aende Beteli na ajenge mazabahu, Yakobo alitenda bila kukawia-kawia. Kwanza, aliambia familia yake: “Muondoe miungu ya kigeni yenye kuwa katikati yenu, na mujisafishe.” Kisha akafuata kwa uaminifu maagizo yenye alikuwa amepewa.​—Mwa. 35:1-7.

20 Yakobo alijenga mazabahu mingi mu Inchi ya Ahadi, lakini sikuzote mupokeaji wa ibada yake alikuwa tu Yehova. (Mwa. 35:14; 46:1) Hali ya zabihu zake, namna alimuabudu Mungu, na nia yenye ilimuchochea afanye vile ilikuwa muzuri, njo maana Biblia inataja Yakobo kuwa “mutu mwenye hana lawama.” Ile maneno inatumiwa kuhusu watu wenye kukubaliwa na Mungu. (Mwa. 25:27) Kupitia maisha yake yote, Yakobo aliwekea taifa la Israeli, lenye lingetokana naye, mufano muzuri.​—Mwa. 35:9-12.

21. Mifano ya wazee wa ukoo inaweza kutufundisha nini kuhusu ibada safi?

21 Mifano ya wazee wa ukoo inaweza kutufundisha nini kuhusu ibada safi? Kama wao, sisi pia tunazungukwa na watu, pengine hata watu wa familia, wenye wanaweza kutufanya tusishikamane tu na Yehova. Juu ya kupiganisha ile uvutano, tunapaswa kukomalisha imani yenye nguvu katika Yehova na tunapaswa kuwa hakika kwamba kanuni zake za haki ni za muzuri kabisa. Tunaonyesha imani ya vile kwa kumutii Yehova na kwa kutumia wakati wetu, nguvu yetu, na mali yetu juu ya kumutumikia. (Mt. 22:37-40; 1 Ko. 10:31) Inatia moyo sana kujua kama wakati tunamuabudu Yehova kulingana na uwezo wetu wote, vile yeye anatuomba, na kwa nia safi, anatuona kuwa wenye haki!​—Soma Yakobo 2:18-24.

Taifa Lenye Kushikamana na Ibada Safi

22-24. Namna gani Sheria ilionyesha ulazima wa kufikiria kwa uzito mwenye alipaswa kuwa mupokeaji wa zabihu za Waisraeli, hali ya zabihu, na namna zilipaswa kutolewa?

22 Yehova alipatia wazao wa Yakobo Sheria, yenye bila shaka iliwaonyesha mambo yenye alitaka wafanye. Kama wangemutii Yehova, wangekuwa ‘mali yake ya pekee’ na “taifa takatifu.” (Kut. 19:5, 6) Tuone namna Sheria ilikazia mambo ine ya musingi yenye ibada safi inaomba.

23 Yehova alionyesha waziwazi ni nani alipaswa kuwa mupokeaji wa ibada ya Waisraeli. Alisema: “Haupaswe kuwa na miungu mingine isipokuwa mimi.” (Kut. 20:3-5) Zabihu zenye walimutolea zilipaswa kuwa za hali ya juu sana. Kwa mufano, zabihu za wanyama zilipaswa kuwa bila kasoro, bila ulemavu wowote. (Law. 1:3; Kum. 15:21; linganisha na Malaki 1:6-8.) Zawadi zenye zilitolewa kwa Yehova zilisaidia Walawi, lakini wao pia walipaswa kutoa matoleo yao kipekee. Zawadi zenye walitoa zilipaswa kutoka kati ya ‘zawadi zote za muzuri sana zenye walipokea.’ (Hes. 18:29) Kuhusu namna yao ya kuabudu, Waisraeli walipewa maagizo yenye kuwa wazi kuhusu nini walipaswa kumutolea Yehova kuwa zabihu, fasi walipaswa kutolea zile zabihu na namna zilipaswa kutolewa. Kwa ujumla, walipewa sheria zaidi ya 600 juu ya kuongoza mwenendo wao, na waliambiwa: “Munapaswa kuwa waangalifu kufanya kama vile Yehova Mungu wenu amewaamuru. Musigeuke kuenda kuume wala kushoto.”​—Kum. 5:32.

24 Je, Waisraeli walipaswa kutoa zabihu zao fasi ni fasi? Hapana. Yehova aliomba watu wake wajenge tabenakulo, na ikakuwa fasi ya maana zaidi ya ibada safi. (Kut. 40:1-3, 29, 34) Ile wakati, kama Waisraeli walipenda matoleo yao ikubaliwe na Mungu, walipaswa kuipeleka ku tabenakulo. *​—Kum. 12:17, 18.

25. Kuhusu zabihu, ya maana zaidi ilikuwa nini? Fasiria.

25 Lakini, ya maana zaidi, ni nia yenye ilimuchochea Mwisraeli atoe zawadi! Alipaswa kuchochewa na moyo wenye kupenda Yehova na kanuni zake. (Soma Kumbukumbu la Torati 6:4-6.) Wakati Waisraeli walifanya ibada ya kidesturi tu, Yehova alikataa zabihu zao. (Isa. 1:10-13) Kupitia nabii Isaya, Yehova alionyesha kwamba hadanganywe na ushikamanifu wa inje tu, wakati alisema: “Watu hawa . . . wananiheshimia kwa midomo yao, lakini moyo wao uko mbali sana na mimi.”​—Isa. 29:13.

Ibada ku Hekalu

26. Ku mwanzo, hekalu lenye lilijengwa na Sulemani lilitimiza daraka gani mu ibada safi?

26 Miaka mingi kisha Israeli kuanza kuishi mu Inchi ya Ahadi, Mufalme Sulemani alijenga fasi ya maana zaidi ya ibada safi yenye ilikuwa ya mukubwa zaidi kuliko tabenakulo. (1 Fa. 7:51; 2 Ny. 3:1, 6, 7) Ku mwanzo, Yehova njo alikuwa mupokeaji wa zabihu zote zenye zilitolewa ku hekalu. Sulemani na raia wake walitoa zabihu mingi za hali ya muzuri na mu namna yenye Sheria ya Mungu ilionyesha. (1 Fa. 8:63) Lakini, haiko garama ya majengo ya hekalu na hesabu kubwa ya zabihu njo ilifanya Yehova akubali ibada yenye ilitolewa ku hekalu. Ya maana zaidi ni nia yenye iliwachochea watoe zile zawadi. Sulemani alikazia ile jambo wakati wa kumutolea Yehova hekalu. Alisema: “Moyo wenu ukuwe kamili kwa Yehova Mungu wetu kwa kutembea katika masharti yake na kwa kushika amri zake kama vile leo.”​—1 Fa. 8:57-61.

27. Wafalme wa Israeli na raia wao walifanya nini, na Yehova alitenda namna gani?

27 Ya kuhuzunisha ni kwamba, Waisraeli hawakuendelea kufuata ile shauri ya hekima ya ule mufalme. Hawakutimiza moja ao zaidi kati ya mambo ya musingi yenye ibada safi inaomba. Wafalme wa Israeli na raia wao walifuata mioyo yao yenye kupotoka, walipoteza imani katika Yehova, na waliacha kanuni zake za haki. Kwa upendo, Yehova aliwatumia manabii tena na tena juu ya kuwarekebisha na kuwaonya kuhusu matokeo ya matendo yao. (Yer. 7:13-15, 23-26) Mumoja kati ya wale manabii ni mwanaume muaminifu mwenye kuitwa Ezekieli. Aliishi wakati mugumu wa historia ya ibada safi.

Ezekieli Anaona Namna Ibada Safi Inachafuliwa

28, 29. Ni mambo gani yenye tunajua kuhusu Ezekieli? (Ona kisanduku “Ezekieli​—Maisha na Wakati Wake.”)

28 Ezekieli alijua muzuri namna ibada ilikuwa inafanyika ku hekalu lenye lilijengwa na Sulemani. Baba yake alikuwa kuhani na alikuwa anatumika ku hekalu wakati ilikuwa siku yake. (Eze. 1:3) Inawezekana miaka ya kwanza ya Ezekieli ilikuwa ya furaha. Bila shaka baba yake alimufundisha juu ya Yehova na juu ya Sheria. Tena, karibu na wakati Ezekieli alizaliwa, “kitabu cha Sheria” kilivumbuliwa mu hekalu. * Mutawala wa ile wakati, mufalme muzuri Yosia, aliguswa moyo na mambo yenye alisikia na kwa hiyo alifanya yake yote juu ya kuendelesha ibada safi.​—2 Fa. 22:8-13.

Bila shaka baba ya Ezekieli alimufundisha juu ya Yehova na juu ya Sheria (Ona fungu la 28)

29 Kama wanaume waaminifu wenye waliishi mbele yake, Ezekieli alitimiza mambo ine yenye ibada safi inaomba. Wakati tunachunguza kitabu cha Ezekieli, tunaona kama alimutumikia Yehova peke yake, aliendelea kumutumikia kwa moyo wake wote, na alifanya kwa utii mambo yenye Yehova alimuomba na mu namna yenye Yeye alitaka. Ezekieli alifanya ile yote kwa sababu alichochewa na moyo wenye kujaa imani. Lakini haikukuwa vile kuhusu watu wengi wa wakati wake. Wakati alikuwa anakomaa, Ezekieli alikuwa anasikia maunabii ya Yeremia, mwenye alianza kazi yake mu mwaka wa 647 M.K.Y. na mwenye alionya watu kwa bidii kuhusu hukumu ya Yehova yenye ilikuwa inakuja.

30. (a) Maunabii yenye Ezekieli aliandika inaonyesha nini? (b) Unabii ni nini, na ni habari gani tunapaswa kujua juu ya kuelewa maunabii yenye Ezekieli alitoa? (Ona kisanduku “Habari za Kujua Ili Kuelewa Maunabii ya Ezekieli.”)

30 Maandishi ya Ezekieli yenye kuongozwa na roho ya Mungu inaonyesha namna watu wa Mungu walikuwa wameacha kabisa kumutumikia Yeye. (Soma Ezekieli 8:6.) Wakati Yehova alianza kupatia Yuda nizamu, Ezekieli alikuwa kati ya wale wenye walipelekwa mu utekwa Babiloni. (2 Fa. 24:11-17) Hata kama alipelekwa akiwa mufungwa, Ezekieli hakupewa azabu. Yehova alikuwa na kazi yenye angemupatia afanye kati ya watu Wake wenye walikuwa wamepelekwa mu uhamisho. Maono ya kushangaza na maunabii yenye Ezekieli aliandika inaonyesha namna ibada safi ingerudishwa mu Yerusalemu. Lakini zaidi ya ile, inatusaidia kuelewa muzuri zaidi namna ibada safi itafikia kurudishwa kabisa kwa ajili ya wale wote wenye kumupenda Yehova.

31. Kitabu hiki kitatusaidia kufanya nini?

31 Mu sehemu za kufuata za kitabu hiki, tutapata picha ya makao ya Yehova, kwenye anaishi, tutaona namna ibada safi ilichafuliwa kabisa, tutajifunza namna Yehova anarudisha watu wake mu hali ya muzuri na kuwapigania, na tutachungulia mu siku zenye kuja wakati kila mwanadamu mwenye kuishi atamuabudu Yehova. Mu sura ya kufuata, tutachunguza maono ya kwanza yenye Ezekieli aliandika. Itatusaidia tumuone Yehova mu akili yetu na pia sehemu ya mbinguni ya tengenezo lake, na itaonyesha sababu gani yeye peke yake njo anastahili ibada safi.

^ fu. 4 Inaonekana Eva alipata mimba ya Abeli wakati fulani tu kisha Adamu na Eva kufukuzwa mu Edeni. (Mwa. 4:1, 2) Mwanzo 4:25 inasema kama Mungu alichagua Seti “pa nafasi ya Abeli.” Adamu alikuwa na miaka 130 wakati alizaa Seti, kisha Abeli kuuawa kwa jeuri. (Mwa. 5:3) Kwa hiyo, inaonekana Abeli alikuwa na miaka 100 hivi wakati Kaini alimuua.

^ fu. 15 Mwanzo 4:26 inaonyesha kama wakati wa Enoshi, mujukuu wa Adamu, “watu wakaanza kuitia jina la Yehova.” Lakini, inaonekana walikuwa wanafanya vile mu namna ya kukosa heshima, inawezekana waliita sanamu zao mu jina la Yehova.

^ fu. 17 Mungu mwanaume mwenye kuitwa Nanna alijulikana pia kwa jina la Sini. Hata kama wakaaji wa Uru waliabudu miungu mingi, mahekalu na mazabahu mu ile muji ilitumiwa zaidi sana kwa ajili ya ibada ya Nanna.

^ fu. 24 Kisha Sanduku takatifu kuondolewa mu tabenakulo, inaonekana kama Yehova alikubali zabihu zenye zilitolewa fasi ingine tofauti na tabenakulo.​—1 Sa. 4:3, 11; 7:7-9; 10:8; 11:14, 15; 16:4, 5; 1 Ny. 21:26-30.

^ fu. 28 Inaonekana Ezekieli alianza kutoa unabii wakati alikuwa na miaka 30, mu mwaka wa 613 hivi M.K.Y. Kwa hiyo, pengine alizaliwa mu mwaka wa 643 hivi M.K.Y. (Eze. 1:1) Yosia alianza kutawala mu mwaka wa 659 M.K.Y., na kitabu cha Sheria, pengine kile kitabu cha kwanza kabisa, kilivumbuliwa wakati fulani karibu na mwaka wa 18 wa utawala wake, ao mwaka wa 642-641 hivi M.K.Y.