Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 3

“Nilianza Kuona Maono ya Mungu”

“Nilianza Kuona Maono ya Mungu”

EZEKIELI 1:1

WAZO KUBWA: Maono ya Ezekieli kuhusu gari la mbinguni

1-3. (a) Fasiria mambo yenye Ezekieli anaona na kusikia. (Ona picha ku mwanzo wa habari.) (b) Ni nguvu gani ilimuwezesha Ezekieli kuona na kusikia ile mambo, na mambo yenye aliona na kusikia ilikuwa na matokeo gani juu yake?

EZEKIELI anaangalia kule mbali, anakaza macho kuelekea bonde kubwa, lenye muchanga. Anafunga macho kidogo, kisha anaifungua sana. Haitike kabisa mambo yenye anaona. Kule mbali, karibu na kwenye macho yake inaishia, anaona upepo mukali unakuja. Lakini haiko upepo wa kawaida. Wakati upepo mukali wenye unavuma kutoka kaskazini unapiga nywele na nguo zake na kuzifanya ziende huku na huku, anaona wingu kubwa, la murefu sana. Ile wingu inaangaziwa na moto wenye kumeremeta, na kungara kwake kunamukumbusha metali ya kuyeyushwa ya bei sana. * Kadiri ile wingu inakimbia haraka kwenye Ezekieli iko, sauti inaendelea kupanda​—makelele kama ya jeshi kubwa lenye kutembea.​—Eze. 1:4, 24.

2 Wakati alikuwa na miaka 30 hivi, kijana huyu anajionea jambo la kwanza kati ya mambo mingi ya kufuatana yenye hawezi kusahau. Anasikia “mukono wa Yehova” juu yake, ni kusema, nguvu yenye haiwezi kushindwa ya roho takatifu ya Yehova. Mambo yenye roho itamuwezesha kuona na kusikia ni ya ajabu, ya kushangaza sana kupita filme yoyote yenye picha na sauti za pekee yenye mutengeneza-filme wa leo amekwisha kufanya. Maono yenye Ezekieli ataona itamufanya aanguke uso chini ku udongo, akiwa amelemewa kabisa.​—Eze. 1:3, 28.

3 Lakini, Yehova hatafute tu kushangaza huyu mwanaume. Maono ya kwanza ya Ezekieli​—kama vile ile maono ingine yenye kuandikwa mu kitabu hiki cha kupendeza cha unabii​—iko na mafundisho ya maana sana, kwa ajili yake na kwa ajili ya watumishi waaminifu wa Yehova leo. Tuchunguze basi kwa uangalifu mambo yenye Ezekieli anaona na kusikia.

Hali za ile Wakati

4, 5. Hali zilikuwa namna gani wakati Ezekieli aliona ile maono?

4 Soma Ezekieli 1:1-3. Tujikumbushe kwanza hali za ile wakati. Ilikuwa mwaka wa 613 M.K.Y. Kama vile tulijifunza mu sura yenye ilitangulia, Ezekieli alikuwa anaishi Babiloni kati ya wahamishwa wenzake wenye walikuwa wanaishi wakiwa kikundi karibu na muto Kebari. Inaonekana Kebari ilikuwa mufereji wenye ulifanywa na watu, wenye watu wangeweza kusafiri juu yake na mashua; ilitoka ku muto Efrati na kuungana tena na ile muto kule mbele.

Ezekieli alikuwa anaishi kati ya wahamishwa karibu na muto Kebari (Ona fungu la 4)

5 Yerusalemu, kwenye wahamishwa walikuwa wanaishi, ilikuwa mbali ku kilometre 800 hivi. * Hekalu, kwenye baba ya Ezekieli alikuwa anatumikia akiwa kuhani, lilikuwa limeangukia mu upotovu ao mwenendo mubaya sana na ibada ya sanamu. Kiti cha ufalme mu Yerusalemu, kwenye Daudi na Sulemani walikuwa wametawala katika utukufu zamani, kilikuwa sasa mu hali ya kuhuzunisha. Yehoyakini, mufalme mwenye hakukuwa na imani, alikuwa Babiloni pamoja na wahamishwa. Sedekia, mwenye alimukomboa ku kiti cha ufalme, alikuwa anafuata tu kile mufalme wa Babiloni alikuwa anasema, na alikuwa mutu muovu.​—2 Fa. 24:8-12, 17, 19.

6, 7. Juu ya nini Ezekieli angewaza kama alikuwa anaishi mu wakati wa mubaya sana?

6 Kwa mutu wa imani sawa vile Ezekieli, ile ilipaswa kuwa wakati wa mubaya sana mu maisha yake. Pengine wamoja kati ya wahamishwa wenzake walijiuliza: ‘Je, Yehova ametuacha milele? Je, guvernema hii ya mubaya ya Babiloni na miungu yake mingi ya uongo itaondoa kabisa ibada safi ya Yehova na kuondoa utawala wake mu dunia?’

7 Kwa kuwa sasa uko na zile habari mu akili, juu ya nini usianze kujifunza kipekee ile habari kwa kusoma maelezo ya kupendeza ya Ezekieli kuhusu maono yake ya kwanza? (Eze. 1:4-28) Wakati utakuwa unafanya vile, jaribu kujitia pa nafasi ya Ezekieli, kwa kuona mambo yenye aliona na kusikia mambo yenye alisikia.

Muto Efrati karibu na Karkemishi (Ona fungu la 5-7)

Gari Lenye Kuwa Tofauti Kabisa

8. Ezekieli aliona nini mu maono, na jambo lenye aliona lilifananisha nini?

8 Kwa kifupi, Ezekieli aliona nini? Aliona kitu kama vile gari kubwa, lenye kushangaza sana, lenye kuwa na kiti cha ufalme. Lilikuwa na magurudumu ine ya munene-munene yenye kufuatwa na viumbe ine vya roho vyenye havikukuwa vya kawaida, vyenye kutajwa kuwa makerubi mu mistari ya kufuata. (Eze. 10:1) Juu ya ile magurudumu kulikuwa jukwaa kubwa, kama barafu (glace), lenye juu yake kulikuwa kiti cha ufalme cha Mungu chenye utukufu, chenye kuikaliwa na Yehova mwenyewe! Sasa, ile gari ilifananisha nini? Maono ya Ezekieli ilifananisha kabisa kitu kimoja: sehemu ya mbinguni ya tengenezo la Yehova lenye utukufu la ulimwenguni pote. Juu ya nini tunasema vile? Fikiria mambo tatu yenye inafanya tuseme vile.

9. Namna gani maelezo kuhusu gari inaonyesha kama Yehova njo mwenye kuongoza viumbe vyake vya mbinguni?

9 Yehova njo anaongoza viumbe vyake vya mbinguni. Ona kwamba mu hii maono, kiti cha ufalme cha Yehova kiko juu ya makerubi. Vilevile, mu sehemu zingine za Neno la Mungu, Yehova anazungumuziwa ao anaonyeshwa akikaa akiwa mufalme juu ao katikati ya makerubi wake. (Soma 2 Wafalme 19:15; Kut. 25:22; Zb. 80:1) Kusema kweli, hakae kabisa-kabisa juu ya makerubi wake​—sawa vile iko na lazima ya kubebwa na vile viumbe vya roho vyenye nguvu—​na pia hana lazima ya kupanda juu ya gari la kweli-kweli. Lakini wale makerubi wanatetea mamlaka yake makubwa zaidi, na anaweza kuwatuma fasi yote mu ulimwengu kusudi wafanye mapenzi yake. Makerubi, kama vile malaika wote watakatifu wa Mungu, wanatimiza maamuzi ya Yehova wakiwa watumishi wake, ao wajumbe wake. (Zb. 104:4) Ni mu ile maana, Yehova “anapanda” juu yao wote, kwa kuwaongoza akiwa mutawala wao. Ni kama vile wanafanyiza gari moja kubwa na lenye kufanya kazi kwa umoja.

10. Ni nini inaonyesha kama ile gari haifananishe tu wale makerubi ine?

10 Ile gari haifananishe tu wale makerubi ine. Makerubi wenye Ezekieli aliona walikuwa ine. Namba ine inatumiwa mara mingi mu Biblia juu ya kuonyesha usawa ao hali ya kuwa kamili, ni kusema, inaonyesha kama kitu fulani kinatia ndani kila mutu, hakuna mwenye haiko ndani. Kwa hiyo basi, wale makerubi ine wanafananisha wana wote wa roho wa Yehova wenye kuwa waaminifu. Ona pia kwamba, magurudumu na hata makerubi wenyewe wanajaa macho, ile inaonyesha uangalifu mukubwa sana wenye viumbe vingi sana vya roho viko nao, hapana tu vile viumbe ine vyenye kuonyeshwa. Na maelezo yenye Ezekieli anatoa kuhusu gari inaonyesha kama ni gari kubwa, na ile inafanya makerubi waonekane kuwa wadogo. (Eze. 1:18, 22; 10:12) Vilevile, sehemu ya mbinguni ya tengenezo la Yehova ni kubwa, inafanyizwa na zaidi ya wale makerubi ine.

Ezekieli alishangazwa sana na maono ya gari la Yehova la mbinguni (Ona fungu la 8-10)

11. Danieli aliona maono gani yenye kufanana na ile ya Ezekieli, na kwa hiyo tunaweza kusema nini?

11 Danieli aliona maono ya mbingu yenye kufanana na ile ya Ezekieli. Nabii Danieli aliishi miaka mingi mu uhamisho mu muji wa Babiloni, na yeye pia alipewa maono ya mbingu. Ya kufurahisha ni kwamba, mu ile maono pia, kiti cha ufalme cha Yehova kilikuwa na magurudumu. Maono ya Danieli inakazia zaidi sana ukubwa wa familia ya Yehova ya mbinguni ya viumbe vya roho. Danieli aliona “maelfu elfu . . . na elfu kumi mara elfu kumi” ya wana wa roho wa Mungu wakisimama mbele ya Yehova. Walikaa kama Tribinali ya mbinguni, kila mumoja ku fasi yake yenye amepewa. (Dan. 7:9, 10, 13-18) Je, hauone kama inapatana na akili kusema kwamba maono ya Ezekieli inafananisha tengenezo lilelile lenye utukufu la viumbe vya roho?

12. Juu ya nini kujifunza maandiko kama ile yenye inahusu maono ya Ezekieli ya gari la mbinguni kunaweza kutulinda?

12 Yehova anajua kwamba, kukaza akili yetu juu ya mambo ya kiroho, yenye mutume Paulo aliita kuwa “vitu vyenye havionekane,” kunaweza kutulinda. Juu ya nini tunasema vile? Juu, tuko viumbe vya mwili na damu, tuko na zoezi ya kufikiria sana “vitu vyenye vinaonekana,” ni kusema, mambo ya kimwili, yenye ni ya wakati kidogo tu. (Soma 2 Wakorinto 4:18.) Mara mingi, Shetani anatumia ile zoezi kusudi atufanye kuwa watu wenye kuwaza tu mambo ya kimwili. Ili kutusaidia tusikuwe na ile zoezi, kwa upendo Yehova anatutolea maandiko kama ile ya unabii wa Ezekieli, yenye inatupatia vikumbusho vya muzuri kuhusu ukubwa wa kushangaza sana wa familia ya Yehova ya mbinguni!

“Magurudumu Yenye Kuzunguka!”

13, 14. (a) Ezekieli alitoa maelezo gani kuhusu magurudumu yenye aliona? (b) Gari la Yehova lenye kuwa na kiti cha ufalme liko na magurudumu. Juu ya nini inapaswa kuwa vile?

13 Kwanza, Ezekieli anakaza uangalifu wake juu ya wale makerubi ine, na mu Sura ya 4 ya kitabu hiki, tutaona mambo yenye viumbe na umbo ya ajabu ya vile viumbe inatufundisha kuhusu Yehova. Lakini, Ezekieli aliona magurudumu ine karibu na wale makerubi, inaonekana ilikuwa kwenye pembe ine, na hivyo ilifanyiza uwanja mukubwa wenye pande ine zenye kuwa sawasawa. (Soma Ezekieli 1:16-18.) Ile magurudumu ilionekana kuwa yenye kufanyizwa na krisolito, jiwe la samani lenye mutu anaweza kuonea ndani ao lenye linaweza kupitisha mwangaza na la rangi ya manjano ao manjano-kijani. Ile krisolito yenye kupendeza ilimeremeta.

14 Maono ya Ezekieli inatia mukazo mukubwa juu ya magurudumu ya gari. Waza kidogo: Kiti cha ufalme chenye kiko na magurudumu! Ile haiko jambo ya kawaida, hauone vile? Kwa kawaida tunajuaka kama kiti cha ufalme kinawekwa fasi fulani tu, na ni vile, kwa sababu watawala wa dunia hawawezi kufanya mamlaka yao ifike mbali sana. Lakini mamlaka makubwa zaidi ya Yehova iko tofauti na utawala wowote wa mwanadamu. Kama vile Ezekieli alikuwa karibu kujifunza, mamlaka makubwa zaidi ya Yehova haina mipaka. (Ne. 9:6) Kwa kweli, Mutawala huyu Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi anaweza kutumia mamlaka yake kila fasi!

15. Ezekieli aliona nini kuhusu ukubwa na muundo wa magurudumu?

15 Ezekieli alishangazwa sana na ukubwa wa magurudumu. Aliandika hivi: “Mizingo yake ilikuwa juu sana kiasi ya kwamba iliogopesha sana.” Tunaweza kuwazia Ezekieli akipandisha kichwa chake juu aone ile mizingo (jantes) mikubwa, ya kumeremeta na ya murefu kuelekea juu katika anga. Na aliongeza jambo hili la kushangaza sana: “Mizingo ya [magurudumu] yote ine ilikuwa imejaa macho kuizunguka pande zote.” Lakini, pengine jambo la kushangaza sana kuliko yote, ni muundo wenye hauko wa kawaida wa magurudumu. Alieleza: “Kuonekana kwa magurudumu hayo na muundo wake vilikuwa kama vile gurudumu lilikuwa ndani ya gurudumu lingine.” Maana yake nini?

16, 17. (a) Ni mu maana gani ile gari iko na magurudumu ndani ya magurudumu? (b) Magurudumu inaonyesha nini kuhusu gari la Yehova?

16 Ni wazi kama, kila gurudumu lenye Ezekieli aliona, lilikuwa kwa kweli magurudumu mbili yenye kuingiana moja ndani ya lingine, gurudumu moja lilikutana na lingine katikati ya kipenyo (axe) chenye kuwa wima na kufanyiza pembe muraba. Ile inatusaidia kuelewa juu ya nini magurudumu ilikuwa inaenda namna Ezekieli alifasiria: “Wakati yalienda, yangeweza kuenda upande wowote wa zile pande ine bila kugeuka wakati yalikuwa yanaenda.” Magurudumu inaonyesha nini kuhusu gari la mbinguni lenye Ezekieli aliona?

17 Magurudumu ya urefu wa kushangaza vile inaweza kufanya safari ya murefu mu kuzunguka mara moja tu. Kwa kweli, ile maono inaonyesha kama ile gari inaenda na mbio ya mwangaza wa radi! (Eze. 1:14) Zaidi ya ile, watengenezaji wa magari wanaweza kupenda kutengeneza magurudumu yenye inaweza kuenda upande wowote ao kubadilisha mwendo kama ile magurudumu ya kushangaza, lakini hawawezi kufanya vile. Ile gari inaweza kuenda upande fulani bila kupunguza mwendo ao hata kugeuka! Lakini haifanye vile ovyo-ovyo. Macho yenye inajaa ku mizingo ya magurudumu inaonyesha kabisa kama ile gari inaona kabisa kila kitu chenye kuwa pembeni yake, kila upande.

Magurudumu ilikuwa na ukubwa wa kushangaza sana na ilikuwa inaenda mbio sana (Ona fungu la 17)

18. Ukubwa wa kushangaza sana wa magurudumu na macho mingi yenye inajaa juu yake vinatufundisha nini?

18 Basi, ni jambo gani lenye Yehova alikuwa anafundisha Ezekieli​—na watu wote waaminifu—​kuhusu sehemu ya mbinguni ya tengenezo Lake? Fikiria mambo yenye tumekwisha kuona. Kitu chenye kumeremeta chenye kufanyiza magurudumu na ukubwa wa magurudumu vinaonyesha kama sehemu ya mbinguni ni yenye utukufu na ya kushangaza sana. Macho yenye inajaa ku magurudumu inaonyesha kama sehemu ya mbinguni inaona kila kitu. Macho ya Yehova inaona mambo yote. (Mez. 15:3; Yer. 23:24) Zaidi ya ile, Yehova iko na mamilioni ya watumishi wenye ni malaika, wenye anaweza kutuma fasi yoyote mu ulimwengu, na wale malaika wanaweza kuchunguza mambo kwa uangalifu na kupelekea habari Mutawala wao Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi.​—Soma Waebrania 1:13, 14.

Muundo wa magurudumu ulionyesha kama inaweza kuenda upande wowote (Ona fungu la 17, 19)

19. Mbio na uwezo wa gari la Yehova wa kuenda upande wowote vinatufundisha nini juu ya Yehova na sehemu ya mbinguni ya tengenezo lake?

19 Tena, tunaona kama ile gari iko na mbio sana na inaweza kuenda upande wowote. Fikiria kidogo tofauti kati ya sehemu ya mbinguni ya tengenezo la Yehova na guvernema za wanadamu, mashirika na matengenezo yao! Hazina uwezo wa kumaliza matatizo ya dunia, zinashindwa kujipatanisha na hali zenye kubadilika-badilika, na njo maana haziwezi kutengeneza mambo na kwa hiyo zitaharibiwa. Lakini gari la Yehova linaonyesha kabisa kama Mungu mwenye kuliongoza ni mwenye usawaziko na mwenye kujipatanisha na hali. Kama vile jina lake linaonyesha, anaweza kuwa kitu chochote chenye kinaombwa juu atimize kusudi lake. (Kut. 3:13, 14) Kwa mufano, anaweza kubadilika haraka kuwa Mupiganaji-Vita mwenye nguvu juu ya kupigania watu wake ao kuwapatia azabu ao malipizi kwa sababu ya uasi wao, lakini anaweza pia kubadilika haraka kuwa Mwenye Kusamehe zambi kwa rehema na mwenye kutunza na kurudisha mu hali ya muzuri hata watenda-zambi wenye wamepondwa roho kabisa.​—Zb. 30:5; Isa. 66:13.

20. Ni nini inatushangaza sana kuhusu gari la Yehova?

20 Kufikia hapa, maono ya Ezekieli inaweza kutuchochea tujiulize, ‘Je, ninashangazwa kabisa na gari la Yehova?’ Tusisahau kama ile gari inafananisha jambo fulani lenye liko sasa. Tusiwaze hata kidogo kama Yehova, Mwana wake, na malaika wote hawaone magumu fulani yenye inatuvunja moyo. Wala tusiwaze kwamba Mungu wetu atachelewa kutupatia mambo yenye tuko nayo lazima ao kwamba tengenezo lake litashindwa kujipatanisha na hali ngumu mupya yenye inaweza kutokea mu ulimwengu huu wenye kubadilika-badilika wenye kutuzunguka. Ni muzuri tukumbuke kama tengenezo la Yehova liko linafanya kazi, na liko linasonga mbele kila siku. Zaidi ya ile, Ezekieli alisikia sauti mbinguni ikilalamika: “Magurudumu yenye kuzunguka!”​—inaonekana ile ilikuwa amri ya kuomba magurudumu ianze kuenda. (Eze. 10:13) Bila shaka namna Yehova anafanya tengenezo lake lisonge mbele ni jambo la kushangaza sana. Lakini, mwenye tunapaswa kushangaa zaidi ni Yehova mwenyewe.

Mwenye Kuongoza Gari

21, 22. Ni nini inaunganisha sehemu za ile gari?

21 Ezekieli aliacha kuangalia magurudumu na akaanza kuangalia juu, na kule aliona “mufano wa anga lenye kumeta-meta kama barafu yenye kuogopesha.” (Eze. 1:22) Mbali juu ya vichwa vya wale makerubi, kulikuwa anga kubwa, lenye kungara na lenye utukufu wenye unaweza kupitisha mwangaza. Lakini, kufikia hapa, musomaji mwenye anaelewa namna mashine inatumika anaweza kujiuliza maulizo mingi kuhusu ile gari. Kwa mufano, wengine wanaweza kujiuliza: ‘Ni nini inakamatisha jukwaa ao anga lenye kuwa juu ya magurudumu? Na namna gani magurudumu inaweza kutembea bila kuwa na vyuma vya katikati vya kuiunganisha?’ Ujue kama ile gari haiongozwe na sheria za asili, kwa sababu ni ya mufano, inafananisha jambo fulani la kweli-kweli mu makao ya roho. Ona pia maneno hii ya maana: “Roho yenye ilikuwa inatenda juu ya vile viumbe vyenye uzima ilikuwa pia ndani ya yale magurudumu.” (Eze. 1:20, 21) Ni roho gani ilikuwa inatenda juu ya makerubi na juu ya magurudumu?

22 Bila shaka, ilikuwa roho takatifu ya Yehova, nguvu kubwa zaidi mu ulimwengu wote. Ile nguvu ya utendaji njo inaunganisha gari pamoja, inaitia nguvu, na kuongoza muzuri kabisa hatua zake zenye kupatana. Kwa kuwa sasa tuko na zile habari mu akili, tufuate Ezekieli wakati anakaza uangalifu wake juu ya Ule mwenye kuongoza gari.

Ezekieli alipaswa kutafuta maneno ya kufasiria mambo yenye aliona yenye ilikuwa nguvu kueleza

23. Ezekieli anatumikisha maneno gani juu ya kujaribu kueleza namna Yehova iko, na juu ya nini anatumia ile maneno?

23 Soma Ezekieli 1:26-28. Mu maelezo yote ya maono hii, Ezekieli anatumikisha mara mingi maneno kama vile “-onekana kama,” “-fanana na,” na “kitu kama.” Lakini mu maandiko hii, anatumikisha sana ile maneno. Inaonekana anajaribu kutafuta maneno ya kufasiria mambo yenye aliona yenye kuwa nguvu kueleza. Aliona “kitu chenye kilionekana kama jiwe la yakuti, na kilifanana na kiti cha ufalme.” Je, unaweza kufikiria kiti cha ufalme chenye kuchongwa kutokana na jiwe la yakuti la rangi ya bluu sana? Na Mutu wa Maana Sana alikuwa anakaa ku ile kiti. “Alionekana kama mwanadamu.”

24, 25. (a) Upinde wa mvua wenye kuzunguka kiti cha ufalme cha Yehova unatukumbusha nini? (b) Wakati fulani, maono kama hii ilikuwa na matokeo gani juu ya wanaume wenye imani wa zamani?

24 Ule mutu mwenye utukufu hakuonekana muzuri-muzuri kabisa, sababu Yehova alikuwa anatosha miale ya utukufu kutoka ku kiuno kuenda chini na kutoka ku kiuno kuenda juu. Tunaweza kuwazia namna nabii Ezekieli alikuwa anafunga macho kidogo na kuifunika wakati alikuwa anaangalia ile umbo yenye utukufu. Kwa mwisho, Ezekieli aliona jambo hili lenye kupendeza sana kuhusu ile maono: “Kulikuwa mwangaza kumuzunguka pande zote kama mwangaza wa upinde wa mvua katika wingu siku ya mvua.” Je, umekwisha kujisikia mwenye furaha sana wakati uliona upinde wa mvua? Ile upinde ya mvua inatukumbusha kabisa utukufu wa Muumbaji wetu! Ile upinde ya mvua ya rangi mbalimbali, yenye kutulia mu mbingu inatukumbusha pia agano la Yehova la amani lenye alifanya kisha Garika. (Mwa. 9:11-16) Hata kama Mweza-Yote iko na nguvu mingi, yeye ni Mungu wa amani. (Ebr. 13:20) Amani inajaa mu moyo wake na inapanuka mupaka kwa wale wote wenye kumuabudu kwa uaminifu.

Upinde wa mvua wenye utukufu wenye kuzunguka kiti cha ufalme cha Yehova unatukumbusha kama tunatumikia Mungu wa amani (Ona fungu la 24)

25 Maono ya utukufu wa Yehova Mungu yenye Ezekieli aliona ilikuwa na matokeo gani juu yake? Ezekieli aliandika kile kilitokea: “Wakati niliuona, nikaanguka uso chini.” Kwa sababu ya kushangaa sana na kumuogopa Mungu, Ezekieli alianguka chini. Manabii wengine walitenda vile wakati walipokea maono kutoka kwa Yehova; mambo yenye waliona iliwafanya wajisikie kuwa wa hali ya chini sana, na hata iliwalemea. (Isa. 6:1-5; Da. 10:8, 9; Ufu. 1:12-17) Lakini kisha, wale wanaume walijisikia kuwa wametiwa nguvu na mambo yenye Yehova aliwafunulia. Bila shaka Ezekieli alijisikia vile. Sasa, kusoma habari za Maandiko kama hizi kunapaswa kuwa na matokeo gani juu yetu?

26. Namna gani maono yenye Ezekieli aliona ilimutia nguvu?

26 Kama Ezekieli alikuwa anahangaishwa na mashaka na woga kuhusu hali ya watu wa Mungu kule Babiloni, bila shaka ile maono ilimutia nguvu. Kwa kweli, ya maana haikukuwa watu waaminifu wa Mungu wakuwe Yerusalemu ao Babiloni ao fasi ingine yoyote. Hata kama wangekuwa wapi, gari la Yehova lenye utukufu lingefika kwenye walikuwa! Ni nguvu gani ya Shetani yenye inaweza kumuzuia Mungu mwenye kuongoza tengenezo la mbinguni lenye utukufu vile? (Soma Zaburi 118:6.) Pia, Ezekieli aliona kama, gari la mbinguni haliko mbali sana na watu. Sababu, magurudumu yake ilikuwa inagusa kabisa dunia! (Eze. 1:19) Kwa hiyo, Yehova alikuwa anajua muzuri kabisa hali ya watu wake waaminifu wenye walikuwa mu uhamisho. Hawakukuwa fasi kwenye Baba yao mwenye upendo hangeweza kufika juu ya kuwahangaikia!

Gari Linakufundisha Nini?

27. Maono ya Ezekieli inatufundisha nini leo?

27 Je, maono ya Ezekieli inaweza kutufundisha mambo fulani leo? Ndiyo! Kumbuka, Shetani iko anatayarisha mashambulizi makubwa sana juu ya ibada safi ya Yehova. Anapenda atufanye tuamini kama tuko peke yetu, mbali, kwenye Baba yetu wa mbinguni na tengenezo lake hawawezi kufika. Usiache uongo wa vile uingie hata kwa kiasi kidogo mu akili ao moyo wako! (Zb. 139:7-12) Kama Ezekieli, tuko na sababu mingi za kushangaa sana. Pengine hatutaanguka uso chini kama vile alifanya. Lakini, tunapaswa kushangaa na kushituka sana wakati tunafikiria nguvu, mwendo, uwezo wa kuenda upande wowote, uwezo wa kujipatanisha na hali, na utukufu wenye kungara wa sehemu ya mbinguni ya tengenezo la Yehova la ulimwenguni pote.

28, 29. Ni mambo gani inaonyesha kama gari la Yehova liko linasonga mbele mu miaka mia moja yenye imepita?

28 Kumbuka pia kwamba, tengenezo la Yehova liko na sehemu ya duniani. Ni kweli kwamba, sehemu ya duniani inafanyizwa na wanadamu wenye hawakamilike. Lakini, fikiria mambo yenye Yehova amefanya ku dunia! Mu dunia yote, Yehova amechochea wanadamu wa kawaida tu juu wafanye mambo yenye hawangeweza kufanya kwa uwezo wao wenyewe. (Yoh. 14:12) Kuangalia tu kurasa za kitabu Ufalme wa Mungu Unatawala! kunaweza kutukumbusha namna kazi ya kuhubiri imeenea mu njia ya kushangaza mu miaka mia moja yenye imepita. Tunaweza pia kufikiria maendeleo ya haraka yenye tengenezo la Yehova limefanya juu ya kupatia Wakristo wa kweli elimu, kupata ushindi mbalimbali ku tribinali, na pia katika kutumia teknolojia ya sasa juu ya kutimiza mapenzi ya Mungu!

29 Wakati tunafikiria ile yote yenye imefanywa kuhusu kurudisha ibada safi mu siku za mwisho za mupangilio huu mubaya wa mambo, inakuwa wazi zaidi na zaidi kwamba gari la Yehova liko linasonga mbele. Tuko na pendeleo kubwa sana la kutumika pamoja na tengenezo hili na kumutumikia Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi kama ule!​—Zb. 84:10.

Sehemu ya duniani ya tengenezo la Yehova inaendelea kusonga mbele (Ona fungu la 28, 29)

30. Tutazungumuzia nini mu sura ya kufuata?

30 Lakini, kungali mambo mingi yenye maono ya Ezekieli inatufundisha. Mu sura ya kufuata, tutachunguza kwa uangalifu zaidi vile “viumbe vyenye uzima” vyenye kushangaza, ao makerubi. Vinaweza kutufundisha nini kuhusu Mutawala wetu mutukufu Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova Mungu?

^ fu. 1 Ezekieli alitaja elektramu, ni kusema, muchanganyiko wa feza na zahabu.

^ fu. 5 Ile njo ilikuwa makilometre kati ya Babiloni na Yerusalemu kama mutu anafuata njia ya kunyooka, lakini inawezekana njia yenye wahamishwa walifuata ilikuwa ile makilometre karibu mara mbili.