Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 6

“Sasa Mwisho Uko Juu Yako”

“Sasa Mwisho Uko Juu Yako”

EZEKIELI 7:3

WAZO KUBWA: Namna hukumu za Yehova zenye zilitabiriwa kuhusu Yerusalemu zilitimia

1, 2. (a) Ni matendo gani ya kushangaza yenye Ezekieli alifanya? (Ona picha ku mwanzo wa habari.) (b) Matendo yake ilionyesha nini?

HABARI kuhusu matendo ya kushangaza ya Ezekieli inaenea haraka kati ya wahamishwa Wayahudi wenye wanaishi mu inchi ya Babiloni. Kwa juma moja, alikuwa amekaa kati ya wahamishwa bila kusema kitu na mu hali ya kushangaa sana, lakini sasa, anasimama mara moja na kujifungia mu nyumba yake. Sasa, wakati majirani wake wenye kushangaa wanaendelea kuangalia, nabii anatoka mu nyumba yake, anakamata tofali ao brike moja, anaitia mbele yake, na anafanya muchoro juu yake. Kisha, bila kusema kitu, Ezekieli anaanza kujenga ukuta ya kidogo.​—Eze. 3:10, 11, 15, 24-26; 4:1, 2.

2 Wenye kumuangalia wanaendelea kuongezeka, na inawezekana wanajiuliza, ‘Mambo yote hii, njo kusema nini?’ Ni kisha wakati fulani tu njo wahamishwa Wayahudi wataelewa kwamba matendo ya kushangaza ya nabii Ezekieli ilikuwa inaonyesha tukio fulani lenye kuogopesha sana lenye lingekuja na lenye lingeonyesha kasirani ya Mungu ya haki. Ilikuwa tukio gani? Ile tukio ilikuwa na matokeo gani juu ya taifa la zamani la Israeli? Iko na maana gani kwa waabudu wa kweli leo?

‘Kamata Tofali . . . Kamata Ngano . . . Kamata Upanga Mukali’

3, 4. (a) Ni sehemu gani tatu za hukumu ya Mungu zenye Ezekieli alionyesha? (b) Ezekieli alifanya nini juu ya kuonyesha namna Yerusalemu ingezungukwa kwa ajili ya vita?

3 Mu mwaka wa 613 hivi M.K.Y., Yehova aliambia Ezekieli aonyeshe kupitia alama sehemu tatu za hukumu ya Mungu yenye ingekuja juu ya Yerusalemu. Zile sehemu zilikuwa: Kuzunguka muji kwa ajili ya vita, mateso ya wakaaji wake, na uharibifu wa muji na watu wake. * Acha basi tuzungumuzie zile sehemu tatu kwa urefu.

4 Kuzunguka Yerusalemu kwa ajili ya vita. Yehova aliambia Ezekieli: “Kamata tofali na ulitie mbele yako. . . . Uuzunguke kwa ajili ya vita.” (Soma Ezekieli 4:1-3.) Tofali lilifananisha muji wa Yerusalemu, lakini Ezekieli alifananisha jeshi la Babiloni lenye Yehova alitumia. Ezekieli aliambiwa pia ajenge ukuta ya kidogo, ya kuzunguka muji kwa ajili ya vita, na atengeneze vyombo vya kubomolea. Kisha alipaswa kuvizungusha pembeni-pembeni ya tofali. Vilifananisha vyombo vya vita vyenye maadui wa Yerusalemu wangetumia wakati wa kuzunguka muji na kuushambulia. Juu ya kuonyesha namna maaskari adui wangekuwa na nguvu kama chuma, Ezekieli alipaswa kutia “kikaangio cha chuma,” ao bamba, kati yake na muji. Kisha alikaza ‘uso wake juu ya’ muji. Ile mambo yote yenye alifanya ilikuwa “alama kwa nyumba ya Israeli” ya kuonyesha kwamba jambo fulani lenye hawakuwazia lilikuwa karibu kutokea. Yehova angetumia jeshi la maadui juu ya kuzunguka Yerusalemu kwa ajili ya vita, muji mukubwa wa watu wa Mungu, kwenye hekalu la Mungu lilikuwa!

5. Fasiria namna Ezekieli alionyesha mambo yenye ingepata wakaaji wa Yerusalemu.

5 Mateso ya wakaaji wa Yerusalemu. Yehova alimuagiza Ezekieli: ‘Kamata ngano, shayiri, maharagi ya munene-munene, dengu, mutama, na ngano ya kusemeti . . . na uvifanye kuwa mukate,’ na “utapima na kula shekeli makumi mbili (20) za chakula kwa siku.” Kisha Yehova akaeleza: “Nitaondoa akiba ya chakula.” (Eze. 4:9-16) Mu onyesho hii, Ezekieli hafananishe jeshi la Babiloni; lakini, anafananisha wakaaji wa Yerusalemu. Mambo yenye nabii alifanya ilionyesha kwamba wakati maadui wangezunguka muji kwa ajili ya vita, chakula ingekosekana mu muji. Ile wakati, watu wangechanga vitu vyenye haiko kawaida kuchanga juu watengeneze mukate, ile inaonyesha kama watu wangekula kitu chochote chenye wangepata. Njaa ingekuwa kali kadiri gani? Ezekieli anafanya sawa vile iko anazungumuza moja kwa moja na wakaaji wa Yerusalemu, kwa kusema: “Baba wenye kuwa kati yenu watakula wana wao, na wana watakula baba zao.” Ku mwisho, watu wengi wangeteseka sababu ya “mishale hatari yenye kuleta njaa,” na ile ingefanya watu “waharibike.”​—Eze. 4:17; 5:10, 16.

6. (a) Ni mambo gani mbili Ezekieli alifanya mu wakati moja? (b) Amri ya Mungu ya kuomba Ezekieli ‘apime na agawanye nywele’ ilionyesha nini?

6 Uharibifu wa Yerusalemu na watu wake. Mu sehemu hii ya onyesho ya unabii, Ezekieli alifanya mambo mbili mu wakati moja. Kwanza, Ezekieli alifanya onyesho ya mambo yenye Yehova angefanya. Yehova alimuambia: “Kamata upanga mukali ili uutumie kama wembe wa mukata-nywele.” (Soma Ezekieli 5:1, 2.) Mukono wa Ezekieli wenye ulitumia upanga ulifananisha mukono wa Yehova​—hukumu yake—​yenye ingetolewa kupitia jeshi la Babiloni. Pili, Ezekieli alifanya onyesho ya mambo yenye ingepata Wayahudi. Yehova alimuambia: “Nyoa kichwa chako na ndevu zako.” Tendo la Ezekieli la kunyoa kichwa chake lilifananisha namna Wayahudi wangeshambuliwa na kuuawa. Tena, amri ya kumuomba ‘akamate mizani za kupimia na agawanye nywele hizo katika mafungu’ ilionyesha kama hukumu ya Yehova juu ya Yerusalemu itatimia, hapana mu njia yenye inakosa utaratibu, lakini mu njia yenye inapangwa na kwa ukamili.

7. Juu ya nini Yehova aliambia Ezekieli agawanye nywele mu mafungu tatu na atendee kila fungu mu njia tofauti?

 7 Juu ya nini Yehova aliambia Ezekieli agawanye mu mafungu tatu nywele zenye alinyoa na atendee kila fungu mu njia tofauti? (Soma Ezekieli 5:7-12.) Ezekieli aliteketeza ao kulunguza fungu moja la nywele “ndani ya muji” juu ya kuonyesha wenye walikuwa wanaangalia kwamba wakaaji fulani wa Yerusalemu watakufia ndani ya muji. Ezekieli alipiga fungu lingine la nywele kwa upanga “kuzunguka muji pande zote” juu ya kuonyesha kama wakaaji wengine watauawa inje ya muji. Alisambaza fungu la mwisho la nywele ku upepo juu ya kuonyesha kama wakaaji wengine watasambazwa kati ya mataifa, lakini ‘upanga utawafuatilia.’ Kwa hiyo, hata kama wenye wangeokoka wangeenda kuishi wapi, hawangepata amani yoyote.

8. (a) Onyesho ya Ezekieli ilikuwa na jambo gani lenye kuleta tumaini? (b) Namna gani maneno ya unabii kuhusu “nywele kidogo” ilitimia?

8 Lakini, onyesho ya unabii ya Ezekieli iko na jambo fulani lenye kuleta tumaini. Kuhusu nywele zenye Ezekieli alinyoa, Yehova aliambia nabii wake hivi: “Unapaswa kukamata nywele kidogo na kuzifunga katika mikunjo ya nguo yako.” (Eze. 5:3) Ile amri ilionyesha kama Wayahudi kidogo wenye wangesambazwa kati ya mataifa wangeokoka. Wamoja kati ya wale wenye walifananisha “nywele kidogo” wangekuwa kati ya wahamishwa wenye wangerudia Yerusalemu kisha miaka 70 ya utekwa mu Babiloni. (Eze. 6:8, 9; 11:17) Je, ile maneno ya unabii ilitimia? Ndiyo. Miaka fulani kisha kumalizika kwa utekwa wa Babiloni, nabii Hagai alionyesha kama wamoja kati ya Wayahudi wenye walisambazwa kati ya mataifa walirudia kabisa Yerusalemu. Walikuwa “wanaume wazee wenye walikuwa wameona ile nyumba ya kwanza,” ni kusema, hekalu la Sulemani. (Ezr. 3:12; Hag. 2:1-3) Yehova alifanya mipango juu ibada safi ilindwe, kama vile tu alikuwa ameahidi. Habari zaidi kuhusu kurudishwa kwa watu wa Mungu mu inchi yao itazungumuziwa mu Sura ya 9 ya kitabu hiki.​—Eze. 11:17-20.

Unabii Huu Unatufundisha Nini Kuhusu Matukio Yenye Kuja?

9, 10. Ni matukio gani makubwa ya wakati wenye kuja yenye maonyesho ya Ezekieli inafanya tufikirie?

9 Matukio yenye Ezekieli alionyesha inafanya tufikirie matukio makubwa yenye Neno la Mungu linaonyesha kama itatokea wakati wenye kuja. Matukio gani kwa mufano? Kama vile alitendea muji wa zamani wa Yerusalemu, Yehova atatumia guvernema za dunia juu ya kufanya jambo lenye mutu hawezi kuwazia​—kushambulia matengenezo yote ya dini za uongo yenye kuwa mu dunia. (Ufu. 17:16-18) Kama vile tu uharibifu wa Yerusalemu ulikuwa “musiba wa pekee,” vilevile “taabu kubwa” na vita ya Armagedoni itakuwa tukio lenye ‘halijatokea’ hata siku moja.​—Eze. 5:9; 7:5; Mt. 24:21.

10 Neno la Mungu linaonyesha kama wafuasi moja moja wa dini ya uongo hawataharibiwa wakati matengenezo ya dini ya uongo itaharibiwa. Kwa sababu ya woga, wale wafuasi wenye wataokoka kisha kuharibiwa kwa dini ya uongo watajiunga na watu wengine wa hali zote wenye watakuwa wanatafuta fasi ya kujificha. (Zek. 13:4-6; Ufu. 6:15-17) Hali yao inatukumbusha mambo yenye ilipata wakaaji wa Yerusalemu ya zamani wenye waliokoka kisha kuharibiwa kwake na kusambazwa “kwenye upepo.” Kama vile tuliona mu  fungu la 7, hata kama hawakuuawa ile wakati, Yehova alichomoa “upanga ili kuwafuatilia.” (Eze. 5:2) Vilevile, fasi zote za kujificha kwenye wale wenye wataokoka kisha kuharibiwa kwa dini ya uongo watakimbilia hazitazuia upanga wa Yehova usiwafikie. Watauawa ku Armagedoni, pamoja na wengine wote wenye kufananishwa na mbuzi.​—Eze. 7:4; Mt. 25:33, 41, 46; Ufu. 19:15, 18.

Tutakuwa “bubu” kuhusu kutangaza habari njema

11, 12. (a) Kuelewa unabii wa Ezekieli kuhusu namna Yerusalemu ingezungukwa kwa ajili ya vita kunatufanya tukuwe na mawazo gani leo juu ya kazi ya kuhubiri? (b) Inawezekana ujumbe wenye tunahubiri utabadilika kuwa ujumbe gani?

11 Kuelewa unabii huu kunatusaidia tukuwe na mawazo gani juu ya kazi ya kuhubiri na juu ya ulazima wa kuifanya haraka? Kunatusaidia kuelewa kama tunapaswa kufanya nguvu yetu yote leo juu ya kusaidia watu wakuwe watumishi wa Yehova. Juu ya nini? Wakati wenye unabakia juu ya ‘kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote’ uko mufupi. (Mt. 28:19, 20; Eze. 33:14-16) Wakati shambulizi la “fimbo” (guvernema za dunia) juu ya dini litaanza, hatutahubiri tena ujumbe wa wokovu. (Eze. 7:10) Tutakuwa “bubu” kuhusu kutangaza habari njema, sawa vile Ezekieli alikuwa bubu, ni kusema, aliacha kutangaza ujumbe wake, wakati fulani wa utumishi wake. (Eze. 3:26, 27; 33:21, 22) Kwa kweli, kisha dini ya uongo kuharibiwa, watu watajaribu, mu njia fulani, bila kuwa na tumaini lolote ‘kutafuta maono kwa nabii,’ lakini hawatapewa mafundisho yoyote yenye itawasaidia waokoke. (Eze. 7:26) Wakati wa kupata mafundisho ya namna ile na wa kuwa mwanafunzi wa Yesu utakuwa umepita.

12 Lakini, tutaendelea kuhubiri. Juu ya nini tunasema vile? Wakati wa taabu kubwa, inawezekana tuanze kuhubiri ujumbe wa hukumu wenye utakuwa kama mvua ya majiwe. Ile ujumbe itaonyesha waziwazi kama mwisho wa ulimwengu muovu uko juu ya wanadamu.​—Ufu. 16:21.

“Angalia, Unakuja!”

13. Juu ya nini Yehova aliambia Ezekieli alalie upande wake wa kushoto na kisha alalie upande wake wa kuume?

13 Zaidi ya kutabiri namna Yerusalemu ingeharibiwa, Ezekieli alionyesha pia ni wakati gani ingeharibiwa. Yehova aliambia Ezekieli alalie upande wake wa kushoto mu siku 390 na alalie upande wake wa kuume mu siku 40. Kila siku ilifananisha mwaka moja. (Soma Ezekieli 4:4-6; Hes. 14:34) Ile onyesho, yenye inaonekana Ezekieli alikuwa anafanya wakati fulani tu kila siku, ilionyesha mwaka wenye Yerusalemu ingeharibiwa. Inaonekana miaka 390 ya kosa la Israeli ilianza mu mwaka wa 997 M.K.Y., mwaka wenye ufalme wa makabila 12 uligawanyika mu sehemu mbili. (1 Fa. 12:12-20) Inaonekana miaka 40 ya zambi ya Yuda ilianza mu mwaka wa 647 M.K.Y., mwaka wenye Yeremia alipewa mugao wa kuwa nabii juu ya kuonya watu wa ufalme wa Yuda, kwa kutumia maneno ya waziwazi, kuhusu uharibifu wenye ulikuwa unakuja. (Yer. 1:1, 2, 17-19; 19:3, 4) Kwa hiyo, vipindi vyote mbili vingeisha mu mwaka wa 607 M.K.Y., mwaka wenye Yerusalemu ilianguka na kuharibiwa, kama vile Yehova alikuwa ametabiri. *

Namna gani Ezekieli alionyesha mwaka wenye Yerusalemu ingeharibiwa? (Ona fungu la 13)

14. (a) Namna gani Ezekieli alionyesha kama alikuwa hakika kwamba Yehova hangechelewa hata kidogo? (b) Ni mambo gani ingetokea mbele ya kuharibiwa kwa Yerusalemu?

14 Wakati Ezekieli alipokea unabii wa siku 390 na siku 40, pengine hakuelewa Yerusalemu ingeharibiwa mu mwaka gani kabisa. Lakini, mu miaka yenye ilitangulia uharibifu wa Yerusalemu, alionya Wayahudi tena na tena kwamba hukumu ya Yehova ilikuwa inakuja. Alitangaza hivi: “Sasa mwisho uko juu yako.” (Soma Ezekieli 7:3, 5-10.) Ezekieli alijua bila shaka kwamba Yehova hangechelewa hata kidogo. (Isa. 46:10) Nabii Ezekieli alitabiri pia matukio yenye ingetokea mbele ya kuharibiwa kwa Yerusalemu: “Musiba utakuja juu ya musiba.” Ile misiba njo ingevunja matengenezo ya jamii, ya dini, na ya guvernema.​—Eze. 7:11-13, 25-27.

Wakati Yerusalemu ilizungukwa kwa ajili ya vita ilifanana na “chungu cha kupikia” chenye kutiwa “juu ya moto” (Ona fungu la 15)

15. Ni mambo gani ya unabii wa Ezekieli ilianza kutimia tangu mwaka wa 609 M.K.Y. na kuendelea?

15 Miaka kidogo kisha Ezekieli kutangaza kuanguka kwa Yerusalemu, unabii wake ulianza kutimia. Mu mwaka wa 609 M.K.Y., Ezekieli alipata habari kama Yerusalemu imeanza kushambuliwa. Ile wakati, sauti ya tarumbeta iliita wakaaji wa muji wakuje pamoja juu ya kupigania muji wao, lakini kama vile Ezekieli alikuwa ametabiri, “hakuna” mwenye alikuwa “anaenda katika vita.” (Eze. 7:14) Wakaaji wa Yerusalemu hawakukuja pamoja juu ya kupigania muji wao na kupigana na Wababiloni wenye waliuvamia. Pengine Wayahudi fulani walifikiri kama Yehova angekuja kuwaokoa. Alifanyaka vile wakati Waashuru walitaka kukamata Yerusalemu na ile wakati malaika moja wa Yehova aliua maaskari wengi sana wa jeshi lao. (2 Fa. 19:32) Lakini mara hii, hakuna malaika mwenye alifika juu ya kuwasaidia. Kisha wakati fulani tu, muji wenye kuzungukwa kwa ajili ya vita ulifanana na “chungu cha kupikia” chenye kilikuwa “juu ya moto,” na wakaaji wake walikamatwa sawa vile “vipande vya nyama” ndani ya chungu. (Eze. 24:1-10) Muji wa Yerusalemu uliharibiwa kisha kuzungukwa kwa ajili ya vita mu miezi 18 ya mateso makali.

“Mujiwekee Hazina Mbinguni”

16. Namna gani tunaweza kuonyesha leo kama tuko hakika kwamba Yehova hatachelewa hata kidogo?

16 Sehemu hii ya unabii wa Ezekieli inaweza kutufundisha nini? Je, iko na uhusiano na ujumbe wenye tunahubiri na namna watu wanaitikia ile ujumbe? Tayari Yehova amekwisha kuamua ni wakati gani dini ya uongo itaharibiwa​—na mara hii tena hatachelewa hata kidogo. (2 Pe. 3:9, 10; Ufu. 7:1-3) Hatujue kabisa tarehe ya ile uharibifu. Lakini, kama vile Ezekieli, tunaendelea kutii agizo la Yehova la kuonya watu tena na tena, kwa kusema: “Sasa mwisho uko juu yako.” Sababu gani inaomba tutangaze ile ujumbe tena na tena? Sababu ni ileile yenye ilifanya Ezekieli atangaze ujumbe wake tena na tena. * Watu wengi wenye alitangazia unabii wa Mungu kuhusu kuanguka kwa Yerusalemu hawakuuamini. (Eze. 12:27, 28) Lakini kisha, wahamishwa fulani Wayahudi wenye walikuwa Babiloni walionyesha kama walikuwa na moyo muzuri, na walirudia mu inchi yao. (Isa. 49:8) Vilevile, watu mingi leo wanakataa kuamini kama ulimwengu huu utafikia mwisho. (2 Pe. 3:3, 4) Wanadamu wangali na wakati wa kukubali ujumbe wa Mungu. Lakini, mbele ile wakati iishe, tunataka kusaidia watu wenye moyo muzuri wapate barabara yenye inapeleka ku uzima.​—Mt. 7:13, 14; 2 Ko. 6:2.

Hata kama watu wengi hawasikilize, tunaendelea kutafuta watu wenye moyo muzuri (Ona fungu la 16)

Juu ya nini wakaaji wa Yerusalemu ya zamani ‘walitupa feza yao katika barabara’? (Ona fungu la 17)

17. Ni hali gani na matukio gani tutajionea wakati wa taabu kubwa yenye kuja?

17 Unabii wa Ezekieli unaonyesha pia kama wakati matengenezo ya dini itashambuliwa mu siku zenye kuja, watu wa makanisa ‘hawataenda katika vita’ juu ya kupigania dini zao. Lakini, wakati wataona kama kilio chao cha kuomba musaada, “Bwana, Bwana,” hakijibiwe, “mikono yao itaninginia kwa uregevu” na “kutetemeka.” (Eze. 7:3, 14, 17, 18; Mt. 7:21-23) Kisha watafanya nini? (Soma Ezekieli 7:19-21.) Yehova anasema hivi: “Watatupa feza yao katika barabara.” Ile maneno yenye ilitimia kuhusu wakaaji wa Yerusalemu ya zamani inaonyesha waziwazi namna mambo itakuwa wakati wa taabu kubwa. Ile wakati, watu watatambua kama feza haiwezi kuwaokoa mu musiba wenye kuja.

18. Unabii wa Ezekieli unatupatia somo gani kuhusu mambo yenye tunapaswa kutanguliza mu maisha?

18 Je, unaona somo yenye tunapata mu sehemu hii ya unabii wa Ezekieli? Ni muzuri tujue ni mambo gani tunapaswa kutanguliza mu maisha. Fikiria jambo hili: Wakaaji wa Yerusalemu walibadilisha mara moja mawazo yao kuhusu mambo yenye inapaswa kutangulizwa mu maisha kisha tu wao kuelewa kama mwisho wa muji wao na wa maisha yao umefika na kama vitu vya kimwili haviwezi kuwaokoa. Walitupa vitu vyao na kuanza ‘kutafuta maono kwa nabii’​—lakini ilikuwa kuchelewa sana. (Eze. 7:26) Tofauti na wao, sisi tayari tunajua muzuri kama mwisho wa ulimwengu huu muovu uko juu yetu. Kwa hiyo, kuamini ahadi za Mungu kumetuchochea tutangulize mambo yenye inafaa mu maisha. Njo maana, tunafanya mambo mingi juu ya kupata utajiri wa kiroho, wenye uko na samani ya kudumu na wenye hautatupwa “katika barabara.”​—Soma Matayo 6:19-21, 24.

19. Maneno ya unabii ya Ezekieli inatuhusu leo namna gani?

19 Kwa kifupi, ni mu njia gani maneno ya unabii wa Ezekieli juu ya kuanguka kwa Yerusalemu inatuhusu leo? Inatukumbusha kama wakati wenye unabakia juu ya kusaidia wengine wakuwe watumishi wa Mungu uko mufupi. Kwa hiyo, tunapaswa kutimiza kazi ya kufanya wanafunzi kwa uharaka. Tunafurahi sana wakati watu wenye moyo muzuri wanaanza kumuabudu Baba yetu, Yehova. Lakini, tunaendelea kupatia hata wale wenye hawakamate hatua onyo lenye Ezekieli alipatia watu wa siku zake: “Sasa mwisho uko juu yako.” (Eze. 3:19, 21; 7:3) Wakati ileile, azimio letu ni kuendelea kumutumainia Yehova na kuendelea kutia ibada yake pa nafasi ya kwanza mu maisha yetu.​—Zb. 52:7, 8; Mez. 11:28; Mt. 6:33.

^ fu. 3 Inapatana na akili kusema kwamba Ezekieli alionyesha zile alama zote mbele ya watu. Juu ya nini tunasema vile? Juu, kuhusu maonyesho fulani, kama vile kupika mukate na kubeba mizigo, Yehova aliamuru waziwazi Ezekieli aifanye “mbele ya macho yao.”​Eze. 4:12; 12:7.

^ fu. 13 Kwa kuruhusu Yerusalemu iharibiwe, Yehova alileta hukumu yake hapana tu juu ya ufalme wa Yuda wa makabila mbili lakini pia juu ya ufalme wa Israeli wa makabila kumi na mbili. (Yer. 11:17; Eze. 9:9, 10) Ona kitabu Étude perspicace des Écritures, Buku la 1, uku. 467, Chronologie​—De 997 av. n. è. à la désolation de Jérusalem.”

^ fu. 16 Ona kwamba mu maelezo ya mufupi yenye kupatikana mu Ezekieli 7:5-7, Yehova anatumia maneno “unakuja,” “utakuja,” na “imefika” mara sita.