Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 11

“Nimekuweka Kuwa Mulinzi”

“Nimekuweka Kuwa Mulinzi”

EZEKIELI 33:7

WAZO KUBWA: Yehova anaweka mulinzi na anaonyesha kazi yake

1. Manabii wenye Yehova aliweka kuwa walinzi walikuwa wanafanya nini, na kisha kulitokea nini?

MULINZI anasimama juu ya kuta za Yerusalemu, anatia mukono ku macho juu ya kuilinda kadiri jua linaendelea kushuka. Anaangalia kule mbali kwenye macho yake inaishia. Mara moja, anainua tarumbeta yake, anavuta pumuzi, na anapiga ile tarumbeta juu ya kuonya watu kama jeshi la Babiloni liko linakuja! Lakini wakaaji wa ile muji wenye hawahangaike wamechelewa na hawana tena wakati wa kutenda kisha kusikia mulio wa tarumbeta ya mulinzi. Mu miaka mingi, walinzi wenye Yehova aliweka, ao manabii, walikuwa wanaonya watu kama ile siku itafika; lakini watu walikataa kusikiliza. Sasa jeshi la Babiloni linazunguka muji. Kisha kuzunguka muji kwa ajili ya vita mu miezi mingi, maaskari wanatoboa kuta za muji, wanabomoa kabisa hekalu, wanachinja ao kukamata wakaaji wa Yerusalemu wenye hawana imani, wenye ni waabudu-sanamu.

2, 3. (a) Ni hali gani yenye itafikia wakaaji wa dunia? (b) Tutazungumuzia maulizo gani?

2 Leo, majeshi ya Yehova yenye itatimiza hukumu yake iko inaelekea wakati wenye itapigana na wakaaji wa dunia wenye hawana imani. (Ufu. 17:12-14) Ile pigano njo itakuwa mwisho kabisa wa taabu kubwa ya historia ya wanadamu. (Mt. 24:21) Lakini watu wengi wangali na wakati wa kukubali onyo yenye inatolewa na wale wenye Yehova amechagua juu wafanye kazi ya mulinzi.

3 Ni nini ilimuchochea Yehova aweke walinzi? Mulinzi anatangazaka ujumbe wa namna gani? Ni nani wamefanya kazi ya mulinzi, na sisi kazi yetu ni nini? Tuzungumuzie majibu ya ile maulizo.

“Unapaswa Kuwaonya Kutoka Kwangu”

4. Juu ya nini Yehova aliweka walinzi? (Ona picha ku mwanzo wa habari.)

4 Soma Ezekieli 33:7. Kwa kawaida walinzi walikuwa wanasimama ku ukuta wa muji juu ya kusaidia wakaaji wakuwe salama. Kuweka walinzi kulionyesha waziwazi kama mutawala anahangaikia raia wake. Hata kama sauti ya tarumbeta ya mulinzi ingeweza kushitua wakaaji wenye kulala, ingeweza kuokoa maisha ya wenye walitenda kisha kuisikia. Vilevile, Yehova aliweka walinzi, hapana juu ya kuogopesha Waisraeli kupitia ujumbe wa hukumu, lakini juu alihangaikia watu wake na alitaka kuokoa maisha yao.

5, 6. Ni mu njia gani moja haki ya Yehova inaonekana waziwazi?

5 Wakati aliweka Ezekieli kuwa mulinzi, Yehova alifunua sifa fulani za utu wake zenye zinatutia moyo. Tufikirie tu sifa mbili.

6 Haki: Haki ya Yehova inaonekana waziwazi wakati anatendea kila mumoja wetu bila ubaguzi. Kwa mufano, hata kama watu wengi sana walisikia na kisha wakakataa ujumbe wa Ezekieli, Yehova hakuona Waisraeli wote kuwa kikundi cha waasi; lakini, alitafuta kuona namna kila mutu aliitikia kipekee. Alisema tena na tena kuhusu kuzungumuza na “muovu” na “mwenye haki.” Mu luga ya kwanza-kwanza, ile maneno iko ku umoja, hapana ku uwingi, ile inaonyesha kama Yehova anaona kila mutu kipekee. Kwa hiyo, Yehova anahukumu kila mutu kulingana na namna anatenda kisha kusikia ujumbe.​—Eze. 33:8, 18-20.

7. Yehova anahukumu watu kulingana na nini?

7 Haki ya Yehova inaonekana pia mu namna anahukumu watu. Watu wanahukumiwa, hapana kulingana na mambo yenye walifanyaka zamani, lakini kulingana na namna wanaitikia wakati onyo inatolewa. Yehova aliambia Ezekieli: “Wakati ninamuambia muovu: ‘Hakika utakufa,’ naye anaacha zambi yake na kutenda haki na uadilifu, . . . hakika ataendelea kuishi.” Kisha Yehova anaongeza musemwa huu wa maana: “Hakuna zambi yoyote yenye alitenda yenye itahesabiwa juu yake.” (Eze. 33:14-16) Hata kama ni vile, wale wenye walikuwa wanafanya matendo ya haki hawapaswe kufikiri kama utii wao wa zamani unawapatia sababu ya kuasi leo. Yehova alisema kwamba ikiwa mutu ‘anategemea haki yake mwenyewe na kufanya makosa, hakuna tendo moja kati ya matendo yake yenye haki lenye litakumbukwa, lakini atakufa kwa sababu ya makosa yenye amefanya.’​—Eze. 33:13.

8. Haki ya Yehova inaonekana tena mu njia gani ingine?

8 Haki ya Yehova inaonekana tena mu namna anatoa onyo mbele atende. Ezekieli alianza kazi yake miaka sita hivi mbele jeshi la Babiloni liharibu Yerusalemu. Lakini Ezekieli hakukuwa wa kwanza kuonya watu wa Mungu kama wataombwa watoe hesabu. Kwa zaidi ya miaka mia moja mbele Yerusalemu iharibiwe, Yehova alituma nabii Hosea, Isaya, Mika, Odedi, na Yeremia juu wafanye kazi ya mulinzi. Yehova aliomba Yeremia akumbushe Waisraeli hivi: “Niliweka walinzi wenye walisema, ‘Musikilize sauti ya baragumu!’” (Yer. 6:17) Yehova na wale walinzi hawakupaswa kulaumiwa wakati watu walipoteza maisha yao wakati Wababiloni walifikia kuleta hukumu ya Yehova.

9. Ni mu njia gani Yehova alionyesha upendo mushikamanifu?

9 Upendo: Yehova alionyesha upendo mushikamanifu kwa kutuma walinzi waonye wenye haki lakini pia waovu​—wenye walihuzunisha sana moyo wake na kumuharibishia sifa. Waza kidogo: Waisraeli walijulikana kuwa watu wa Yehova, lakini walimugeuzia mugongo tena na tena na walifuata miungu ya uongo! Yehova alionyesha huzuni kubwa yenye alikuwa nayo wakati walimuasi kwa kulinganisha taifa la Israeli na bibi muzinifu. (Eze. 16:32) Ijapokuwa vile, Yehova hakuwachoka mara moja. Alitafuta namna ya kuwasaidia wamurudilie tena, hapana kuwalipiza kisasi. Alikuwa anatumia upanga wake wa hukumu ku mwisho, wakati mambo yote ilikuwa imeshindikana. Juu ya nini? Alimuambia Ezekieli: “Sifurahie kifo cha muovu, lakini tofauti na hilo mutu muovu abadilishe njia yake na kuendelea kuishi.” (Eze. 33:11) Yehova hakukuwa anafurahia kifo cha muovu ile wakati, na leo ni vile.​—Mal. 3:6.

10, 11. Namna Yehova alitendea watu wake inaweza kutufundisha nini?

10 Namna Yehova alitendea Waisraeli mu njia ya haki na ya upendo inaweza kutufundisha nini? Somo ya kwanza ni hii: Hatupaswe kuona watu wenye tunahubiri kuwa sehemu ya kikundi fulani tu cha watu, lakini tunapaswa kuona kila mutu kipekee. Ni kosa kubwa sana ikiwa tunaanza kuwaza kama mutu fulani hastahili kusikia ujumbe wenye tunahubiri sababu ya mwenendo wake wa zamani ao kabila yake, hali yake ya maisha, ao luga yake! Yehova alifundisha mutume Petro somo yenye ingali ya maana sana leo: “Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa mutu mwenye anamuogopa na kufanya mambo yenye kuwa sawa anakubaliwa naye.”​—Mdo. 10:34, 35.

Je, tunaona watu namna Yehova anawaona? (Ona fungu la 10)

11 Somo ingine ya maana ni hii: Tunapaswa kuendelea kujichunguza; mambo ya muzuri yenye tulifanyaka zamani haitupatie haki ya kufanya mambo ya mubaya leo. Ni muzuri tusisahau kama, sisi na watu wenye tunahubiriaka, tuko na mielekeo ileile ya zambi. Shauri lenye mutume Paulo alipatia kutaniko la Korinto linatuhusu sisi pia: “Ule mwenye anawaza kama anasimama afanye angalisho asianguke. Hakuna jaribu lenye limewapata ninyi isipokuwa lile lenye kuwa la kawaida kwa watu.” (1 Ko. 10:12, 13) Hatupendi hata kidogo kuwa watu wenye ‘wanategemea haki yao wenyewe,’ na kuwaza kwamba hata kama tunajiendesha mubaya, hatutapewa azabu juu tunafanyaka pia mambo ya muzuri. (Eze. 33:13) Hata kama tumemutumikia Yehova miaka mingi, inaomba tuendelee kuwa wanyenyekevu na watiifu.

12. Kama tulifanyaka zambi nzito zamani, nini hatupaswe kusahau?

12 Lakini namna gani kama tulifanyaka zambi nzito zamani na zamiri yetu ingali inatusumbua ao kutuhangaisha? Ujumbe wa Ezekieli unatufundisha kama Yehova atapatia azabu wakosaji wenye hawatubu. Lakini, tunajifunza tena kama Yehova ni Mungu wa upendo kwanza, hapana wa kisasi. (1 Yo. 4:8) Kama tunaonyesha kupitia matendo yetu kwamba tumetubu, hatupaswe hata kidogo kuwaza kama rehema ya Mungu haiwezi kufunika zambi zetu. (Yak. 5:14, 15) Yehova alikuwa tayari kusamehe Waisraeli wenye walifanya uzinifu wa kiroho, na iko tayari kutusamehe sisi pia.​—Zb. 86:5.

“Sema na Wana wa Watu Wako”

13, 14. (a) Walinzi walipaswa kutangaza nini? (b) Isaya alitangaza habari gani?

13 Soma Ezekieli 33:2, 3. Walinzi wa Yehova walipaswa kutangaza nini? Sehemu ya maana sana ya kazi yao ilikuwa kutangaza maonyo. Lakini walitangaza pia habari njema. Ona mifano fulani.

14 Isaya, mwenye alitumika kuanzia mwaka wa 778 hivi mupaka 732 M.K.Y., alionya watu kama Wababiloni watakamata Yerusalemu na kupeleka wakaaji wake mu uhamisho. (Isa. 39:5-7) Lakini roho ya Mungu ilimuongoza pia aandike hivi: “Sikiliza! Walinzi wako wanapandisha sauti yao. Wanapiga vigelegele vya shangwe pamoja, kwa maana wataona jambo hilo waziwazi wakati Yehova atakusanya tena Sayuni.” (Isa. 52:8) Isaya alitangaza habari ya muzuri kupita yote​—ibada safi ingerudishwa!

15. Yeremia alitangaza habari gani?

15 Yeremia, mwenye alitumika kuanzia mwaka wa 647 mupaka mwaka wa 580 M.K.Y., anatajwa mara mingi kimakosa kuwa “mutangaza-misiba.” Ni kweli kwamba alifanya kazi ya maana ya kuonya Waisraeli waovu kuhusu misiba yenye Yehova angeleta juu yao. * Lakini alitangaza pia habari njema, alitabiri kwamba siku moja watu wa Mungu wangerudia mu inchi yao na kwamba ibada safi ingerudishwa kule.​—Yer. 29:10-14; 33:10, 11.

16. Habari yenye Ezekieli alitangaza ilisaidia je watu wenye walikuwa mu utekwa Babiloni?

16 Ezekieli aliwekwa kuwa mulinzi mu mwaka wa 613 M.K.Y., na alibakia mu mugao wake mupaka mwaka wa 591 hivi M.K.Y. Kama vile Sura ya 5 na ya 6 ya kitabu hiki zilionyesha, Ezekieli alionya kwa bidii watu wa Israeli kuhusu uharibifu wenye ungekuja juu yao. Kwa kufanya vile, alijiondolea hatia yoyote ya damu ya uzima wenye ungepotea. Ile wakati, hakuonya tu wahamishwa kama Yehova atapatia azabu waasi-imani wenye kuwa Yerusalemu, lakini pia alisaidia wale wenye walikuwa mu utekwa kule Babiloni waendelee kuwa nguvu kiroho na kuwa tayari kwa ajili ya kazi yenye iliwangojea mu siku zenye zilikuwa mbele yao. Ku mwisho wa miaka 70 ya uhamisho, Yehova angeikalisha mabaki mu inchi ya Israeli yenye ilirudishwa mu hali ya muzuri. (Eze. 36:7-11) Kikundi cha wale mabaki kingefanyizwa zaidi sana na watoto na wajukuu wa wale wenye walimusikiliza Ezekieli kwa uangalifu. Kama vile sura zingine za Sehemu ya 3 ya kitabu hiki zinaonyesha, Ezekieli alikuwa na habari njema ya kutangaza, juu ya kuhakikishia watu kama siku moja ibada safi ingerudishwa mu Yerusalemu.

17. Ni wakati gani Yehova alikuwa anaweka walinzi?

17 Je, manabii wenye walisema na watu wa Mungu mu ile kipindi ya karibu na kuharibiwa kwa Yerusalemu mu 607 M.K.Y., wao tu njo walikuwa walinzi wenye Yehova alitumia? Jibu ni hapana. Mbele kutokee jambo fulani kubwa lenye linahusiana na utimizo wa kusudi lake, Yehova alikuwa anaweka walinzi juu ya kuonya waovu na juu ya kutangaza habari njema.

Walinzi mu Karne ya Kwanza

18. Yohana Mubatizaji alifanya kazi gani?

18 Mu karne ya kwanza (1-100) K.K.Y., Yohana Mubatizaji alifanya kazi ya mulinzi. Alionya Waisraeli wa kimwili kwamba kisha wakati kidogo wangekataliwa. (Mt. 3:1, 2, 9-11) Lakini hakuishia pale. Yesu alisema kama Yohana njo alikuwa “mujumbe” mwenye alitabiriwa, mwenye alitayarishia Masiya njia. (Mal. 3:1; Mt. 11:7-10) Kazi yake ilitia ndani kutangaza habari njema yenye kuonyesha kwamba “Mwana-Kondoo wa Mungu,” Yesu, amefika na atatosha “zambi ya ulimwengu.”​—Yoh. 1:29, 30.

19, 20. Ni mu njia gani Yesu na wanafunzi wake walifanya kazi ya mulinzi?

19 Kati ya walinzi wote, Yesu njo alikuwa mulinzi mukubwa zaidi. Kama vile Ezekieli, Yesu alitumwa na Yehova ku “nyumba ya Israeli.” (Eze. 3:17; Mt. 15:24) Yesu alionya taifa la kimwili la Israeli kama lilikuwa karibu kukataliwa na kama Yerusalemu ingeharibiwa. (Mt. 23:37, 38; 24:1, 2; Lu. 21:20-24) Lakini kazi yake ya kwanza ilikuwa kutangaza habari njema.​—Lu. 4:17-21.

20 Wakati alikuwa ku dunia, Yesu aliambia wanafunzi wake: “Muendelee kukesha.” (Mt. 24:42) Walitii amri yake na walifanya kazi ya mulinzi, kwa kuonya watu kama Yehova alikuwa amekataa Israeli wa kimwili na muji wa kidunia wa Yerusalemu. (Ro. 9:6-8; Gal. 4:25, 26) Sawa vile walinzi wenye waliwatangulia, wanafunzi wa Yesu walikuwa pia na habari njema ya kutangaza. Ujumbe wao ulitia ndani habari ya muzuri ya kuonyesha kama sasa Watu wa Mataifa wanaweza kuwa kati ya Israeli wa Mungu wenye kutiwa-mafuta na kuwa na pendeleo la kusaidia Kristo kurudisha ibada safi ku dunia.​—Mdo. 15:14; Gal. 6:15, 16; Ufu. 5:9, 10.

21. Namna gani Paulo aliweka mufano muzuri?

21 Kati ya walinzi wa karne ya kwanza (1-100), mutume Paulo aliweka mufano muzuri kabisa. Alitimiza daraka lake kwa uzito. Sawa vile Ezekieli, alijua kama angekuwa na hatia ya damu ikiwa angeshindwa kutimiza mugao wake. (Mdo. 20:26, 27) Kwa kufuata mufano wa walinzi wengine, Paulo hakuonya tu watu lakini pia alitangaza habari njema. (Mdo. 15:35; Ro. 1:1-4) Tena, akiongozwa na roho takatifu, alitaja unabii wenye uliandikwa na Isaya: “Ni yenye kupendeza sana juu ya milima, miguu ya mutu mwenye kuleta habari njema,” na alitumia ile unabii kuhusu kazi yenye wafuasi wa Kristo walifanya wakati walikuwa wanahubiri juu ya Ufalme wa Mungu.​—Isa. 52:7, 8; Ro. 10:13-15.

22. Ni nini ilitokea kisha kifo cha mitume?

22 Kisha kifo cha mitume, uasi-imani wenye ulitabiriwa uliingia sana mu kutaniko la Kikristo. (Mdo. 20:29, 30; 2 Te. 2:3-8) Mu kipindi kirefu sana chenye kiliombwa kusudi ngano na magugu ikomae, hesabu ya Wakristo wa uongo wenye kufananishwa na magugu ilimeza wafuasi waaminifu wa Kristo wenye kufananishwa na ngano, na mafundisho ya uongo ilifunika ujumbe wenye kuwa wazi wa Ufalme wa Mungu. (Mt. 13:36-43) Lakini, wakati saa ilifika ya Yehova kutengeneza mambo, alionyesha tena upendo wake na haki yake kwa kuweka walinzi juu watoe onyo lenye kuwa wazi na juu watangaze habari njema. Wale walinzi walikuwa nani?

Yehova Anaweka Tena Walinzi Juu Waonye Waovu

23. Russell na wenzake walifanya kazi gani?

23 Mu miaka yenye ilitangulia 1914, Charles Taze Russell na wenzake walifanya kazi ya ule “mujumbe” mwenye alipaswa ‘kufungua njia’ mbele Ufalme wa Masiya uwekwe. * (Mal. 3:1) Walifanya pia kazi ya mulinzi, kwa kutumia gazeti Le Phare de la Tour de Sion et Messager de la Présence de Christ juu ya kuonya watu kuhusu hukumu ya Mungu na juu ya kueneza habari njema ya Ufalme wa Mungu.

24. (a) Namna gani mutumwa muaminifu amefanya kazi ya mulinzi? (b) Walinzi wa zamani wamekufundisha nini? (Ona muchoro “Walinzi Fulani Wenye Ni Mufano Muzuri.”)

24 Kisha Ufalme kuwekwa, Yesu aliweka kikundi kidogo cha wanaume juu wakuwe mutumwa muaminifu. (Mt. 24:45-47) Kuanzia pale, mutumwa muaminifu, mwenye ni Baraza Lenye Kuongoza, amefanya kazi ya mulinzi. Ile baraza inaongoza kazi ya kutoa onyo kuhusu “siku ya kisasi” na ya kutangaza “mwaka wa nia njema wa Yehova.”​—Isa. 61:2; ona pia 2 Wakorinto 6:1, 2.

25, 26. (a) Wafuasi wote wa Kristo wanapaswa kutii amri gani, na wanaonyesha je kama wanatii ile amri? (b) Tutazungumuzia nini mu sura ya kufuata?

25 Mutumwa muaminifu njo mwenye anaongoza kazi ya mulinzi, lakini Yesu anapatia wafuasi wake “wote” amri ya ‘kuendelea kukesha.’ (Mk. 13:33-37) Tunatii ile amri kwa kuendelea kuwa macho kiroho, na kutegemeza kwa uaminifu mulinzi wa leo. Tunaonyesha kama tuko macho kwa kuhubiri. (2 Ti. 4:2) Ni nini inatuchochea tuhubiri? Kwanza, ni juu tunataka kusaidia watu waokoke. (1 Ti. 4:16) Sasa hivi watu wengi watapoteza maisha yao sababu ya kupuuza onyo la mulinzi wa leo. (Eze. 3:19) Lakini tena, tunapenda sana kutangazia wengine habari ya muzuri zaidi yenye inaonyesha kama ibada safi ilisharudishwa! Leo, tuko mu “mwaka wa nia njema wa Yehova,” na mulango uko wazi juu watu mingi zaidi wakuje tuabudu pamoja nao Mungu wetu wa haki na upendo, Yehova. Sasa hivi watu wote mu dunia wenye wataokoka mwisho wa mupangilio huu muovu watatawaliwa muzuri na utawala wenye rehema wa Mwana wake, Kristo Yesu. Hatupaswe kabisa kujizuia kusaidia mulinzi wa leo kutangaza ile habari njema!​—Mt. 24:14.

Tunategemeza kwa furaha mulinzi wa leo wakati tunatangaza habari njema (Ona fungu la 25)

26 Hata mbele mupangilio huu muovu uishe, tayari Yehova ameunganisha watu wake mu njia ya kushangaza sana. Sura ya kufuata itazungumuzia unabii kuhusu vipande mbili vya muti vyenye vilitumiwa juu ya kuonyesha namna amewaunganisha.

^ fu. 15 Neno “musiba” linapatikana mara 60 hivi mu kitabu cha Yeremia.

^ fu. 23 Juu ya kupata habari zaidi kuhusu hii unabii na utimizo wake, ona kitabu Ufalme wa Mungu Unatawala!, sura ya 2, “Kuzaliwa kwa Ufalme Mbinguni.”