Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 13

“Fasiria Hekalu”

“Fasiria Hekalu”

EZEKIELI 43:10

WAZO KUBWA: Maana ya maono ya kushangaza ya Ezekieli kuhusu hekalu

1-3. (a) Juu ya nini maono ya majengo makubwa ya hekalu ilipaswa kufariji Ezekieli? (Ona picha ku mwanzo wa habari.) (b) Tutazungumuzia nini mu sura hii?

WAZIA Ezekieli iko sasa na miaka 50. Amefanya miaka 25 mu uhamisho. Hekalu la Yerusalemu limefanya miaka mingi mu hali ya kubomoka-bomoka. Ikiwa Ezekieli amekwisha kuwaza kama kuko siku atakuwaka kuhani kule, kwa sasa anatambua kama ni nguvu. Miaka 56 hivi inapaswa kupita mbele kipindi cha uhamisho kimalizike, kwa hiyo Ezekieli anajua kama pengine hataishi siku mingi juu aone namna watu wa Yehova watarudishwa mu inchi yao, wala kuona namna hekalu litajengwa upya. (Yer. 25:11) Je, kuwaza vile kunamufanya akuwe na huzuni?

2 Kwa wema wake, Yehova anachagua wakati hii juu ya kupatia Ezekieli maono yenye iko na habari mingi, maono yenye itapatia ule mwanaume muaminifu faraja mingi na tumaini! Kupitia ile maono, nabii anapelekwa mupaka mu inchi yao na anawekwa ku mulima murefu sana. Pale ku mulima murefu sana, “mutu fulani mwenye kuonekana kwake kulikuwa kama kwa shaba” anakutana naye. Ule malaika anamutembeza mu majengo makubwa sana ya hekalu. (Soma Ezekieli 40:1-4.) Inaonekana sawa vile ni mambo ya kweli kabisa! Ku ngambo ya Ezekieli, ile maono inapaswa kutia nguvu imani yake, kumulemea, na hata kumuvuruga kidogo. Hekalu lenye anaona liko na sehemu mingi zenye anajua, lakini liko pia tofauti sana na hekalu lenye alikuwaka anaona zamani mu Yerusalemu.

3 Ile maono ya kushangaza sana njo inakamata sura kenda za mwisho za kitabu cha Ezekieli. Tuzungumuzie basi mawazo yenye tunapaswa kuwa nayo wakati tuko tunachunguza ile maono na kutafuta kuielewa. Kisha, tutaona kama ile yenye Ezekieli aliona ilikuwa hekalu kubwa la kiroho lenye mutume Paulo alizungumuzia sana miaka mingi yenye ilifuata ao hapana. Kwa mwisho, tutaona kama ile maono ilikuwa na maana gani kwa Ezekieli na kwa wahamishwa wenzake.

Iliomba Mafasirio Ingine

4. Zamani, tulikuwa tunaelewa namna gani maono ya hekalu, lakini sasa tuko na lazima ya nini?

4 Zamani, vichapo vyetu vilionyesha kama Ezekieli alionaka hekalu kubwa la kiroho la Yehova, lenye roho ya Mungu iliongoza mutume Paulo azungumuzie mu barua yenye aliandikia Waebrania. * Kufuatana na ile mawazo, ilionekana kwamba ilikuwa sawa kusema kama sehemu mbalimbali za hekalu lenye Ezekieli aliona mu maono zilifananisha mambo fulani, ao zilikuwa vifananishi vya mambo fulani, kuanzia maelezo yenye Paulo alitoa kuhusu tabenakulo. Lakini, kisha kusali, kujifunza na kufikiri sana tulitambua kama tuko na lazima ya mafasirio ya mwepesi zaidi kuhusu maono ya Ezekieli ya hekalu.

5, 6. (a) Namna gani mutume Paulo alionyesha unyenyekevu wakati alizungumuzia tabenakulo? (b) Paulo alisema nini kuhusu sehemu fulani za tabenakulo, na namna gani mawazo yake inaweza kutusaidia kuelewa maono ya Ezekieli ya hekalu?

5 Ni jambo la hekima tusitafute maana ya kiunabii ao ya mufano mu kila sehemu ya maono ya Ezekieli ya hekalu. Juu ya nini? Fikiria jambo hili: Wakati alizungumuzia tabenakulo na hekalu la kiroho, Paulo alitaja mambo fulani ya tabenakulo, sawa vile, chetezo cha zahabu, kifuniko cha sanduku la agano, na mutungi wa zahabu wenye ndani yake mulikuwa mana. Je, alisema kama ile mambo ilikuwa na maana fulani ya kiunabii? Ni wazi kama roho takatifu haikumuongoza aseme vile. Kuliko kusema vile, Paulo aliandika: “Sasa haiko wakati wa kuzungumuzia mambo hayo kirefu.” (Ebr. 9:4, 5) Paulo alikuwa tayari kufuata muongozo wa roho takatifu na kumungojea Yehova kwa unyenyekevu.​—Ebr. 9:8.

6 Inaomba kuwa na mawazo ya vile pia kuhusu maono ya Ezekieli ya hekalu. Ile maono iko pia na habari mingi. Na inaonekana kwamba ni muzuri zaidi kumungojea Yehova afunue mambo waziwazi kama kuko ulazima wa kupata mwangaza zaidi. (Soma Mika 7:7.) Lakini je, ni kusema roho ya Yehova haijaleta mwangaza wowote kuhusu ile maono? Hapana!

Je, Ezekieli Alionaka Hekalu Kubwa la Kiroho?

7, 8. (a) Kwa sasa tunaelewa mambo namna gani? (b) Kuko tofauti gani kati ya hekalu lenye Ezekieli alionaka mu maono na hekalu la kiroho lenye Paulo alizungumuzia?

7 Kama vile tulisema, mu miaka mingi vichapo vyetu vimefasiria kama Ezekieli alionaka hekalu kubwa la kiroho la Yehova, lenye roho ya Mungu iliongoza Paulo azungumuzie mu barua yenye aliandikia Waebrania. Lakini, kisha kujifunza tena zaidi, tunaelewa kama ile yenye Ezekieli alionaka haikukuwa hekalu kubwa la kiroho. Juu ya nini tunasema vile?

8 Kwanza, hekalu lenye Ezekieli alionaka halipatane na maelezo ya Paulo yenye iliongozwa na roho ya Mungu. Fikiria mambo hii: Mutume Paulo alionyesha waziwazi kama tabenakulo ya wakati wa Musa ilikuwa kivuli na mufano wa kitu fulani kikubwa zaidi. Kama vile hekalu la Sulemani na la Zerubabeli zenye zilijengwa kwa kufuata plani ileile, tabenakulo ilikuwa na chumba chenye kuitwa “Patakatifu Zaidi.” Paulo aliita ile chumba kuwa “mahali patakatifu kwenye kulitengenezwa kwa mikono,” na kueleza kama ilikuwa “mufano wa uhalisi,” hapana uhalisi wenyewe. Ile uhalisi ilikuwa nini? Paulo alieleza: “Mbinguni kwenyewe.” (Ebr. 9:3, 24) Je, ni mbingu njo Ezekieli alionaka? Hapana. Hakuna kitu fulani mu maono ya Ezekieli chenye kinaonyesha kama alikuwa anaona mambo ya mbinguni.​—Linganisha na Danieli 7:9, 10, 13, 14.

9, 10. Kuhusu zabihu, kuko tofauti gani kati ya hekalu lenye Ezekieli alionaka mu maono na hekalu kubwa la kiroho lenye Paulo alizungumuzia?

9 Tofauti kubwa zaidi kati ya maono ya Ezekieli na maelezo ya Paulo inahusu zabihu. Ezekieli alisikia namna watu, wakubwa, na makuhani walipewa maagizo mingi kuhusu kutoa zabihu. Walipaswa kutoa zabihu kwa ajili ya zambi zao wenyewe. Walipaswa pia kutoa zabihu za ushirika, zenye inaonekana mutoaji alipaswa kula sehemu yazo mu vyumba vya kukulia chakula vya hekalu. (Eze. 43:18, 19; 44:11, 15, 27; 45:15-20, 22-25) Je, zile zabihu za tena na tena zilikuwa zinatolewa mu hekalu kubwa la kiroho?

Hekalu lenye Ezekieli alionaka mu maono haiko hekalu kubwa la kiroho

10 Jibu ni wazi na mwepesi. Paulo alieleza: “Wakati Kristo alikuja akiwa kuhani mukubwa wa mambo ya muzuri yenye yamekwisha kufanyika, alipita katika hema kubwa na kamilifu zaidi yenye haikutengenezwa kwa mikono, ni kusema, hapana ya uumbaji huu. Aliingia mahali patakatifu, hapana akiwa na damu ya mbuzi na ya ngombe-dume wadogo, lakini akiwa na damu yake mwenyewe, mara moja kwa wakati wote, na kupata ukombozi wa milele kwa ajili yetu.” (Ebr. 9:11, 12) Kwa hiyo, mu hekalu kubwa la kiroho, zabihu moja tu njo ilitolewa, na ilitolewa mara moja tu. Ile zabihu ni zabihu ya ukombozi, na ilitolewa na Kuhani Mukubwa Zaidi mwenyewe, Yesu Kristo. Ni wazi kama, maono ya Ezekieli ya hekalu na zabihu zake mingi za mbuzi na ngombe-dume hazikufananisha hekalu kubwa la kiroho.

11. Mu siku za Ezekieli, juu ya nini haikukuwa wakati wa Mungu wa kufunua kweli mbalimbali kuhusu hekalu kubwa la kiroho?

11 Ile inatufikisha ku sababu ya pili yenye inaonyesha juu ya nini ile yenye Ezekieli alionaka haikukuwa hekalu kubwa la kiroho: Wakati wa Mungu ulikuwa haujafika wa kufunulia watu mambo ya vile. Usisahau kama, maono ya Ezekieli ilitolewa kwanza kwa wahamishwa Wayahudi kule Babiloni. Walikuwa chini ya Sheria ya Musa. Wakati uhamisho ungemalizika, walipaswa kurudia Yerusalemu na kufuata mambo yenye ile Sheria ilisema kuhusu ibada safi kwa kujenga upya hekalu na mazabahu yake. Kisha walipaswa kuendelea kutoa zabihu kule, na walifanya vile mu miaka karibu 600. Wazia namna Wayahudi wangejisikia kama Ezekieli angewaonyesha hekalu la kiroho​—hekalu lenye ndani yake kuhani mukubwa alipaswa kutoa uzima wake mwenyewe kuwa zabihu, na kisha yeye kufanya vile, hakuna zabihu ingine yenye ingetolewa tena! Wangeona je maono ya vile? Je, ile haingewafanya wasitii tena Sheria ya Musa? Mara mingi, Yehova anafunuaka mambo ku wakati wenye unafaa na wakati watu wake wako tayari.

12-14. Kuko uhusiano gani kati ya hekalu lenye Ezekieli alionaka na maelezo ya Paulo kuhusu hekalu la kiroho? (Ona kisanduku “Mahekalu Tofauti, Somo Tofauti.”)

12 Sasa, kuko uhusiano gani kati ya maono ya Ezekieli ya hekalu na maelezo ya Paulo kuhusu hekalu la kiroho? Inafaa kujua kama Paulo hakutoa maelezo yake kufuatana na maono ya Ezekieli ya hekalu, aliitoa kufuatana na tabenakulo ya wakati wa Musa. Ni kweli kama, Paulo alitaja sehemu mingi zenye zilikuwa pia mu hekalu la Sulemani na la Zerubabeli na zile sehemu zilionekana pia mu maono ya Ezekieli ya hekalu. Lakini kwa ujumla, Ezekieli na Paulo hawakuzungumuzia kitu kimoja mu maandishi yao. * Kuliko kuzungumuzia kitu kimoja, maandishi yao inakamilishana. Mu njia gani?

13 Tunaweza kueleza uhusiano wenye uko kati ya zile habari mbili za Biblia mu njia hii: Mu habari ya Paulo, tunajifunza kuhusu mupango wa Yehova kwa ajili ya ibada, lakini mu habari ya Ezekieli, tunajifunza kuhusu kanuni za Yehova kwa ajili ya ibada. Juu ya kutufundisha kuhusu mupango wa Yehova kwa ajili ya ibada safi, Paulo anafunua maana ya sehemu za hekalu la kiroho sawa vile kuhani mukubwa, zabihu, mazabahu, na Patakatifu Zaidi. Lakini ili kutia mukazo juu ya kanuni za juu za Yehova kwa ajili ya ibada safi, maono ya Ezekieli ya hekalu inatupatia picha yenye iko na habari mingi zenye zinajaza mu akili na moyo wetu somo mbalimbali kuhusu kanuni za Yehova.

14 Sasa, namna yetu mupya ya kuelewa mambo inaishia pale? Kwa kweli, tusiwaze kama maono ya Ezekieli haina maana kubwa kwetu leo. Juu tuone namna ile maono inatuletea faida, acha tuchunguze kwa uangalifu namna ilisaidia Wayahudi mu siku za Ezekieli na mu siku zenye zilifuata.

Ile Maono Ilikuwa na Maana Gani kwa Wahamishwa Wayahudi?

15. (a) Maono ya Ezekieli ilikuwa na wazo gani kubwa? (b) Kuko tofauti gani kati ya Ezekieli sura ya 8 na Ezekieli sura ya 40 mupaka 48?

15 Juu tupate jibu ku ile ulizo, acha tuchunguze maulizo yenye inahusiana na ile ulizo yenye itatusaidia tuelewe mambo muzuri kabisa. Kwanza, ile maono ilikuwa na wazo gani kubwa? Kwa kifupi, wazo kubwa lilikuwa: ibada safi ingerudishwa! Ezekieli alielewa waziwazi ile wazo. Alikuwa ameandika ile yenye sasa ni sura ya 8 ya Ezekieli, na mu ile sura, Yehova alifasiria waziwazi hali ya kuhuzunisha ya hekalu kule Yerusalemu. Na Ezekieli alipaswa kufurahi sana kuandika kwa urefu habari kuhusu mabadiliko ya kushangaza yenye ingetokea, yenye inapatikana mu sura ya 40 mupaka 48. Hapa tunaona kama, ibada safi haipotoshwe, lakini inakuwa namna inastahili kuwa, ni kusema, Yehova anatolewa ibada mu njia ya muzuri sana kulingana na Sheria ya Musa.

16. Maono ya Ezekieli ya hekalu inahakikisha je mambo yenye Isaya alitabiri miaka mia moja mbele?

16 Iliomba ibada ya Yehova iinuliwe ili irudie mu hali yake yenye inastahili. Zaidi ya miaka mia moja mbele, roho ya Mungu iliongoza nabii Isaya aandike hivi: “Katika kipindi cha mwisho cha zile siku, mulima wa nyumba ya Yehova utawekwa imara kabisa kwenye kichwa cha milima, na utainuliwa juu ya vilima.” (Isa. 2:2) Isaya aliona waziwazi mbele ya wakati kwamba ibada safi ya Yehova ingerudishwa na kuinuliwa, ni sawa vile ingewekwa juu ya mulima murefu sana. Na sasa, Ezekieli alijikuta wapi mu ile maono ya Mungu? Alikuwa “juu ya mulima murefu sana,” akiangalia nyumba ya Yehova! (Eze. 40:2) Mu ile njia, maono ya Ezekieli ilihakikisha kama ibada safi ingerudishwa.

Hekalu lenye Ezekieli alionaka lilikuwa fasi ya juu sana, fasi yenye kuinuliwa (Ona fungu la 16)

17. Eleza kwa kifupi mambo yenye iko mu Ezekieli sura ya 40 mupaka 48.

17 Fikiria kwa kifupi mambo yenye Ezekieli aliona na kusikia, kama vile inaandikwa mu sura ya 40 mupaka 48. Aliona namna malaika alikuwa anapima milango mikubwa, ukuta, viwanja, na patakatifu pa hekalu. (Eze. 40-42) Kisha kulitokea jambo moja la ajabu: Yehova alifika kwa utukufu ku hekalu! Yehova alipatia mashauri watu wake waasi, makuhani, na wakubwa. (Eze. 43:1-12; 44:10-31; 45:9-12) Ezekieli aliona muto wenye unatiririka kutoka patakatifu, na ulikuwa unatoa uzima na baraka wakati ulikuwa unaenda kujimwanga mu Bahari ya Chumvi. (Eze. 47:1-12) Na aliona namna inchi inagawanywa sehemu-sehemu, na namna ibada safi inapewa nafasi yake karibu na sehemu ya katikati ya inchi. (Eze. 45:1-8; 47:13–48:35) Ile yote ilionyesha nini? Ni wazi kama, Yehova alikuwa anahakikishia watu wake kama ibada safi ingerudishwa na kuinuliwa. Angebariki nyumba yake ya ibada kwa kuwa pale, na angefanya baraka zitiririke kutoka mu hekalu lake, na ile ingeleta uponyaji, uzima, na utaratibu mu inchi yenye ilirudishwa mu hali ya muzuri.

Hekalu lenye Ezekieli alionaka lilionyesha mu njia ya ajabu sana namna Yehova angerudisha ibada safi (Ona fungu la 17)

18. Je, iliomba kuelewa maono ya hekalu mu njia halisi, vile iko? Fasiria.

18 Pili, je, iliomba kuelewa ile maono mu njia halisi, vile iko? Hapana. Inaonekana Ezekieli na wahamishwa wenzake wenye alielezea maono yake walitambua mara moja kama ile maono haiko ya kuelewa mu njia halisi, vile iko. Juu ya nini? Kumbuka kama Ezekieli aliona hekalu ku “mulima murefu sana.” Ni kweli kwamba ile inapatana muzuri na maelezo ya unabii wa Isaya, lakini kusema kweli, haipatane na fasi kwenye hekalu lilikuwa. Hekalu la Sulemani lilikuwa ku Mulima Moria kule Yerusalemu, na ni pale hekalu lilipaswa kujengwa tena siku moja. Lakini je, Mulima Moria ulikuwa “mulima murefu sana”? Hapana. Kwanza, Mulima Moria unazungukwa na milima yenye iko na urefu sawa wake na ingine yenye kuupita urefu. Tena, majengo ya hekalu yenye Ezekieli aliona ilikuwa ya mukubwa. Eneo lake lilikuwa linazungukwa na ukuta, na ile majengo ilikuwa ya mukubwa sana kiasi ya kwamba haingeenea ku kichwa ya Mulima Moria. Haingeenea hata mu muji wa Yerusalemu wa wakati wa Sulemani! Tena, wahamishwa hawakutazamia kama muto wa kweli-kweli ungetiririka kutoka patakatifu pa hekalu na kujimwanga mu Bahari ya Chumvi, kwenye ungeponyesha maji yenye haina uzima. Kwa mwisho, kwa sababu eneo la inchi ya Ahadi lilikuwa la milima-milima, ile ilifanya mipaka kati ya makabila isikuwe ya kunyooka na ya sawasawa, kama vile inaonyeshwa mu maono. Kwa hiyo, ile maono haipaswe kufasiriwa mu njia halisi, vile iko.

19-21. Yehova alipenda maono ya Ezekieli ikuwe na matokeo gani juu ya watu, na juu ya nini ilipaswa kuwafanya wajisikie vile?

19 Tatu, ile maono ilipaswa kuwa na matokeo gani juu ya watu wa wakati wa Ezekieli? Wakati watu wangekuwa wanafikiri kuhusu kanuni za juu za Yehova kwa ajili ya ibada safi, walipaswa kusikia haya. Yehova aliambia Ezekieli ‘afasirie nyumba ya Israeli kuhusu hekalu.’ Mafasirio ya Ezekieli ilipaswa kuwa wazi kabisa sababu Waisraeli walipaswa “kujifunza plani yake.” Juu ya nini watu walipaswa kufikiri sana kuhusu ile hekalu? Kama vile tuliona, haikukuwa juu waijenge. Lakini, kama vile Yehova alisema, ilikuwa “ili wasikie haya kwa sababu ya makosa yao.”​—Soma Ezekieli 43:10-12.

20 Juu ya nini maono hii ingeweza kugusa zamiri za watu wenye moyo muzuri na kuwafanya wasikie haya? Ona mambo yenye Ezekieli aliambiwa: “Mwana wa binadamu, kaza uangalifu, angalia, na usikilize muzuri kila kitu chenye nitakuambia kuhusu maagizo na sheria za hekalu la Yehova.” (Eze. 44:5) Ezekieli alisikia tena na tena kuhusu maagizo na sheria. (Eze. 43:11, 12; 44:24; 46:14) Tena, Ezekieli alikumbushwa mara mingi kuhusu kanuni za Yehova​—hata kuhusu kanuni ya urefu wa mukono mumoja na kanuni ya vipimo vyenye viko sawa. (Eze. 40:5; 45:10-12; linganisha na Mezali 16:11.) Zaidi ya mara 50 mu maono hii, Ezekieli anatumia maneno ya luga ya zamani yenye inamaanisha “kupima” na “kipimo”!

21 Kwa kuzungumuzia vipimo, sheria, kanuni​—Yehova alitaka kuambia watu wake nini? Inaonekana kama, kwa kutumia maneno mazito, alikuwa anawakumbusha kweli hii ya maana sana: Yehova peke yake tu njo anawekaka kanuni za ibada safi. Wale wenye walikuwa wameacha kufuata zile kanuni walipaswa kusikia haya! Lakini, namna gani ile maono iliwasaidia Wayahudi waelewe vile? Tutachunguza mifano fulani mu sura ya kufuata. Ile itatusaidia kuelewa muzuri zaidi kama ile maono ya kushangaza iko pia na maana fulani kwetu leo.

Juu ya nini maono ya hekalu ilipaswa kufanya watu wenye moyo muzuri wasikie haya? (Ona fungu la 19-21)

^ fu. 4 Hekalu la kiroho ni mupango wa Yehova kwa ajili ya ibada safi wenye unategemea zabihu ya ukombozi ya Yesu Kristo. Tunaelewa kama ile hekalu ilianza mu mwaka wa 29 K.K.Y.

^ fu. 12 Kwa mufano, Paulo alizungumuzia sana kuhani mukubwa na mambo yenye alikuwa anafanya Siku ya kila mwaka ya Kufunika Zambi. (Ebr. 2:17; 3:1; 4:14-16; 5:1-10; 7:1-17, 26-28; 8:1-6; 9:6-28) Lakini mu maono ya Ezekieli, hakuna fasi wanazungumuzia kuhani mukubwa ao Siku ya Kufunika Zambi.