Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 16

“Utie Alama Kwenye Mapaji ya Nyuso”

“Utie Alama Kwenye Mapaji ya Nyuso”

EZEKIELI 9:4

WAZO KUBWA: Namna waaminifu wa wakati wa Ezekieli walitiwa alama ya wokovu na maana ya kutiwa alama leo

1-3. (a) Sababu gani Ezekieli hajue afanye nini, na anapata habari gani kuhusu uharibifu wa Yerusalemu? (b) Tutazungumuzia maulizo gani?

EZEKIELI hajue afanye nini! Ametoka tu kuona maono ya mambo ya kuchukiza yenye Wayahudi waasi-imani wako wanafanya ku hekalu kule Yerusalemu. * Wale waasi wamechafua fasi yenye ilikuwa ya maana sana ya ibada safi mu Israeli. Lakini haiko hekalu tu njo wamechafua. Inchi ya Yuda imejaa jeuri na haiwezi tena kurudia mu hali ya muzuri. Yehova anachukizwa sana na matendo ya watu wake wenye alichagua, njo maana anaambia Ezekieli: “Nitatenda katika kasirani kali.”​—Eze. 8:17, 18.

2 Ezekieli anajisikia mubaya sana kujua kama Yehova amekasirika sana juu ya hali yenye kuwa mu Yerusalemu na ku hekalu lake lenye zamani lilikuwa takatifu, na kama vitaharibiwa! Inawezekana Ezekieli anajiuliza: ‘Halafu waaminifu wenye wako mu muji? Wataokoka? Kama ni vile, wataokoka je?’ Lakini, Ezekieli hatakawia kupata majibu. Kisha tu kusikia hukumu kali yenye itapata Yerusalemu, anasikia sauti kubwa yenye inaita wale wenye wataleta azabu ya Mungu. (Eze. 9:1) Kadiri anaendelea kuona maono, nabii Ezekieli anafarijiwa sana kujua kama uharibifu hautakuwa wa kiholela, lakini utachagua. Kwa kweli, waaminifu wataokoka!

3 Juu tunakaribia mwisho wa mupangilio huu muovu wa mambo, sisi pia tunaweza kujiuliza ni nani wataokoka uharibifu mukubwa wenye uko mbele. Tuzungumuzie basi maulizo hii: (1) Ezekieli aliona nini tena mu maono? (2) Ile maono ilitimia namna gani mu wakati wake? (3) Ile maono ya kiunabii iko na maana gani leo?

“Ita Wale Wenye Wataleta Azabu”

4. Fasiria mambo ingine yenye Ezekieli aliona na kusikia mu maono.

4 Ezekieli aliona na kusikia nini tena mu ile maono? (Soma Ezekieli 9:1-11.) Wanaume saba wanakaribia “kutoka upande wa mulango mukubwa wa juu wenye kuelekea kaskazini,” pengine karibu na fasi kwenye alama ya wivu ilikuwa ao kwenye wanamuke walikuwa wanalia mungu Tamuzi. (Eze. 8:3, 14) Wale wanaume saba wanaingia mu kiwanja cha ndani cha hekalu na kusimama karibu na mazabahu ya shaba ya zabihu. Lakini hawako pale juu ya kutoa zabihu. Mu ile wakati, Yehova hangekubali tena zabihu zenye kutolewa ku hekalu. Wanaume sita wanasimama ‘kila mumoja akiwa na silaha yake ya kuponda-ponda katika mukono wake.’ Mwanaume wa saba alikuwa tofauti kabisa na wengine. Alikuwa anavaa nguo ya kitani, na hakukuwa na silaha, lakini alikuwa na “chombo cha mwandishi cha kuwekea wino.”

5, 6. Ni nini ilipata wale wenye walitiwa alama? (Ona picha ku mwanzo wa habari.)

5 Mwanaume mwenye alikuwa na chombo cha kuwekea wino alipaswa kufanya nini? Yehova mwenyewe alimupatia mugao muzito, kwa kusema: “Pita katika muji wote, katika Yerusalemu yote, na utie alama kwenye mapaji ya nyuso za watu wenye kusumbuka na kulia kwa maumivu kwa sababu ya machukizo yote yenye kufanywa katika muji.” Pengine ile wakati, Ezekieli alikumbuka wazazi waaminifu Waisraeli wenye walitia damu ku sehemu ya juu ya mulango wao na ku miimo ya milango juu ikuwe alama ya kuonyesha kama wazaliwa wao wa kwanza wataokoka uharibifu. (Kut. 12:7, 22, 23) Mu maono ya Ezekieli, je, alama yenye ule mwanaume mwenye alikuwa na chombo cha kuwekea wino angetia juu ya paji la uso ingetimiza kusudi ileile, ni kusema, kuonyesha kama mwenye iko nayo ataokoka uharibifu wa Yerusalemu?

6 Tunapata jibu wakati tunafikiria sababu yenye inafanya ile alama itiwe juu ya watu. Ilipaswa kutiwa juu ya mapaji ya nyuso za wale wenye walikuwa ‘wanasumbuka na kulia kwa maumivu’ kwa sababu ya machukizo yenye ilikuwa ‘inafanywa katika muji.’ Tuseme nini sasa juu ya wale wenye walitiwa alama? Kwanza, moyo wao uliumia sana juu ya ibada ya sanamu yenye ilikuwa inafanywa ku hekalu, na pia juu ya jeuri, uasherati, na mwenendo mubaya sana wenye ulikuwa umejaa mu Yerusalemu. (Eze. 22:9-12) Tena, inaonekana hawakuficha hisia yao. Bila shaka, maneno na matendo ya wale watu wenye moyo muzuri ilionyesha namna walichukizwa sana na mambo yenye ilikuwa inafanywa mu inchi, na ilionyesha kama walipenda sana ibada safi. Mu rehema yake, Yehova angeokoa wale waaminifu.

7, 8. Wanaume wenye walikuwa na silaha za kuponda-ponda walipaswa kutimiza je mugao wao, na ku mwisho mambo ilikuwa je?

7 Sasa, wanaume sita wenye walikuwa na silaha za kuponda-ponda walipaswa kutimiza je mugao wao? Ezekieli alisikia maagizo yenye Yehova aliwapatia: Mufuate ule mwanaume mwenye iko na chombo cha kuwekea wino na muue kila mutu isipokuwa tu ule mwenye ametiwa alama ku paji la uso wake. Yehova aliwaambia tena hivi: “Mutaanzia patakatifu pangu.” (Eze. 9:6) Wale wanaume wenye kuleta azabu walipaswa kuanzia kazi yao ku fasi ya maana sana mu Yerusalemu, ni kusema, ku hekalu, lenye lilikuwa haliko tena takatifu ku macho ya Yehova. Wenye walipaswa kuuawa kwanza ni “wazee wenye walikuwa mbele ya nyumba”​—wazee 70 wa Israeli wenye walikuwa ku hekalu na wenye walikuwa wanatolea miungu ya uongo uvumba.​—Eze. 8:11, 12; 9:6.

8 Ku mwisho, mambo ilikuwa je? Kadiri Ezekieli anaendelea kuangalia na kusikiliza, ule mwanaume mwenye alikuwa na chombo cha kuwekea wino anapatia Yehova ripoti, kwa kusema: “Nimefanya kama vile umeniamuru.” (Eze. 9:11) Ile inafanya tujiulize: ‘Mambo ilikuwa je kuhusu wakaaji wa Yerusalemu? Je, kulikuwa waaminifu fulani wenye waliokoka uharibifu?’

Ile Maono Ilitimia Namna Gani mu Wakati wa Ezekieli?

9, 10. Ni waaminifu gani waliokoka uharibifu wa Yerusalemu, na tunaweza kusema nini juu yao?

9 Soma 2 Mambo ya Nyakati 36:17-20. Unabii wa Ezekieli ulitimia mu mwaka wa 607 M.K.Y. wakati jeshi la Babiloni liliharibu Yerusalemu na hekalu lake. Kama vile “kikombe katika mukono wa Yehova,” Wababiloni walikuwa vyombo vyenye Yehova alitumia ili kumwanga azabu juu ya Yerusalemu yenye ilikosa uaminifu. (Yer. 51:7) Je, ilikuwa uharibifu wa kiholela? Hapana. Maono ya Ezekieli ilionyesha kama Wababiloni hawangeua watu wote.​—Mwa. 18:22-33; 2 Pe. 2:9.

10 Waaminifu fulani waliokoka, kama vile Warekabu, Ebed-meleki Muetiopia, nabii Yeremia, na mwandishi wake Baruku. (Yer. 35:1-19; 39:15-18; 45:1-5) Maono ya Ezekieli inatusaidia kuona kama wale watu walikuwa ‘wanasumbuka na kulia kwa maumivu kwa sababu ya machukizo yote’ yenye ilikuwa inafanywa mu Yerusalemu. (Eze. 9:4) Mbele uharibifu utokee, hakuna shaka kwamba walionyesha kama walichukia uovu mu moyo wao na kwamba walipenda sana ibada safi, na kwa kufanya vile walijitia ku mustari wa watu wenye walipaswa kuokoka.

11. Wanaume sita wenye walikuwa na silaha za kuponda-ponda na mwanaume mwenye alikuwa na chombo cha mwandishi cha kuwekea wino walifananisha nani?

11 Je, wale waaminifu walitiwa alama ya kweli-kweli ya wokovu? Hakuna habari yenye inaonyesha kama mutu fulani​—ikuwe Ezekieli ao nabii mwingine—​alizunguka mu Yerusalemu na kutia alama ya kweli-kweli ku mapaji ya nyuso za waaminifu. Lakini, maono ya kiunabii ya Ezekieli inaonyesha mambo yenye ilikuwa inafanyika mbinguni na yenye wanadamu hawakukuwa wanaona. Mwanaume mwenye alikuwa na chombo cha mwandishi cha kuwekea wino na wale wanaume sita wenye walikuwa na silaha za kuponda-ponda walifananisha viumbe vya kiroho viaminifu, vyenye viko tayari kila wakati kufanya mapenzi ya Yehova. (Zb. 103:20, 21) Hakuna shaka kwamba Yehova alitumia malaika wake ili kuongoza uharibifu juu ya Yerusalemu yenye ilikosa uaminifu. Malaika walihakikisha kwamba uharibifu unachagua, haufanywe kiholela. Ile ilikuwa sawa vile wanatia alama ya mufano juu ya mapaji ya nyuso za wale wenye hawangeuawa.

Maono ya Ezekieli Iko na Maana Gani Leo?

12, 13. (a)  Juu ya nini Yehova alimwanga kasirani yake kali juu ya Yerusalemu, na juu ya nini tunaweza kutazamia kama atafanya vile leo? (b) Je, Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo leo zinafananisha Yerusalemu yenye ilikosa uaminifu? Fasiria. (Ona kisanduku “Je, Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo Zinafananisha Yerusalemu ya Zamani?”)

12 Sasa hivi, tutajionea uharibifu wenye Mungu ataleta wenye haujatokeaka​—“taabu kubwa yenye haijatokea tangu mwanzo wa ulimwengu mupaka sasa, hapana, na haitatokea tena.” (Mt. 24:21) Wakati tunaendelea kungojea ile tukio kubwa sana, maulizo fulani ya maana inatokea: Uharibifu wenye kuja, je, utachagua, ao utakuwa wa kiholela? Je, waabudu wa kweli wa Yehova watatiwa alama ya wokovu mu njia fulani? Mu maneno ingine, je, maono ya kiunabii ya Ezekieli ya mwanaume mwenye iko na chombo cha kuwekea wino inatimia leo? Jibu ku ile maulizo yote tatu ni ndiyo. Juu ya nini tunasema vile? Juu tupate jibu, acha turudie ku maono ya Ezekieli.

13 Je, unakumbuka juu ya nini Yehova alimwanga kasirani yake kali juu ya Yerusalemu ya zamani? Fungua tena Ezekieli 9:8, 9. (Soma.) Wakati Ezekieli aliogopa kama pengine uharibifu wenye ulikuwa unakuja ungemaliza “mabaki wote wa Israeli,” Yehova alitaja sababu ine zenye zilifanya alete ile uharibifu. Kwanza, “kosa” la taifa lilikuwa “kubwa, kubwa sana.” * Pili, inchi ya Yuda ilikuwa “imejaa umwangaji wa damu.” Tatu, Yerusalemu, muji mukubwa wa ufalme wa Yuda, ‘ilijaa upotovu.’ Ine, watu walikuwa wanatetea mwenendo wao muovu kwa kujiambia kama Yehova “haone” matendo yao maovu. Je, ile haifanane na hali ya dunia ya leo yenye kujaa mwenendo mubaya, jeuri, upotovu, na ukosefu wa imani? Bila shaka, sababu Yehova “habadilike,” mambo yenye ililamusha kasirani yake ya haki mu wakati wa Ezekieli, ni ileile njo italamusha kasirani yake kali mu wakati wetu. (Yak. 1:17; Mal. 3:6) Kwa hiyo, tunapaswa kutazamia kama wanaume sita wenye wako na silaha za kuponda-ponda na mwanaume mwenye iko na chombo cha kuwekea wino watakuwa pia na kazi ya kufanya mu siku zetu!

Sasa hivi, wanaume sita wenye wako na silaha za kuponda-ponda watakuwa na kazi ya kufanya (Ona fungu la 12, 13)

14, 15. Ni nini inaonyesha kama kila mara Yehova anaonya watu wake mbele uharibifu utokee?

14 Lakini sasa, namna gani maono ya kiunabii ya Ezekieli inatimia leo? Kama tunaangalia namna ile maono ilitimia zamani, tunaweza kujifunza mambo yenye tunapaswa kungojea sasa na wakati wenye kuja. Fikiria mambo fulani yenye tumejionea ao yenye tutaona yenye inatimiza unabii wa Ezekieli.

15 Yehova anaonya watu mbele uharibifu utokee. Kama vile tuliona mu Sura ya 11 ya kitabu hiki, Yehova aliomba Ezekieli akuwe “mulinzi kwa ajili ya nyumba ya Israeli.” (Eze. 3:17-19) Kuanzia mwaka wa 613 M.K.Y., Ezekieli alionya waziwazi Israeli kuhusu uharibifu wenye ulikuwa unakuja. Manabii wengine, kama vile Isaya na Yeremia, walionya pia watu kuhusu musiba wenye ungekuja juu ya Yerusalemu. (Isa. 39:6, 7; Yer. 25:8, 9, 11) Leo, kupitia Kristo, Yehova ametumia kikundi kidogo cha watumishi wake watiwa-mafuta juu ya kupatia chakula cha kiroho waabudu wa kweli, ao watumishi wa nyumbani, na pia ametumia kile kikundi juu ya kuonya watu kuhusu taabu kubwa yenye iko inakuja mbio sana.​—Mt. 24:45.

16. Je, sisi watumishi wa Yehova tunatiaka alama juu ya watu wenye wataokoka? Fasiria.

16 Haiko watu wa Yehova njo wanatiaka alama juu ya wale wenye wataokoka. Kumbuka kama Ezekieli hakuambiwa azunguke mu Yerusalemu na atie alama ya wokovu juu ya wengine. Vilevile leo, watu wa Yehova hawapewe kazi ya kutia alama juu ya watu wenye wanastahili kuokoka. Lakini, sisi watumishi wa mu nyumba ya kiroho ya Kristo, tumepewa kazi ya kuhubiri. Tunaonyesha kama tunakamata ile kazi kwa uzito kwa kuhubiri kwa bidii habari njema ya Ufalme wa Mungu na kwa kuonya watu kama dunia hii yenye kuharibika inakaribia sana mwisho wake. (Mt. 24:14; 28:18-20) Kwa kufanya vile tunashiriki katika kazi ya kusaidia watu wenye moyo muzuri waingie mu ibada safi.​—1 Ti. 4:16.

17. Watu wanapaswa kufanya nini sasa juu wakuwe ku mustari wa watu wenye watatiwa alama mu wakati wenye kuja?

17 Juu mutu aokoke uharibifu wenye uko unakuja, anapaswa kuonyesha imani yake sasa. Kama vile tuliona, wenye waliokoka uharibifu wa Yerusalemu mu mwaka wa 607 M.K.Y. ni watu wenye walionyesha mbele ya wakati kwamba walichukia uovu mu moyo wao na kwamba walipenda sana ibada safi. Na leo ni vile. Mbele uharibifu ukuje, watu wanapaswa ‘kusumbuka na kulia kwa maumivu,’ maana yake, kuhuzunika sana mu moyo wao juu ya ubaya wa dunia hii. Na kuliko kuficha huzuni yao, wanapaswa kuonyesha kwa maneno na matendo kwamba wanapenda sana ibada safi. Watafanya vile je? Wanapaswa kuitika mahubiri yenye iko inafanywa leo, kuendelea kuiga sifa ao tabia za Kristo, kubatizwa juu ya kuonyesha kama wamejitoa kwa Yehova, na kusaidia kwa uaminifu ndugu za Kristo. (Eze. 9:4; Mt. 25:34-40; Efe. 4:22-24; 1 Pe. 3:21) Ni wale tu wenye wako wanafanya vile sasa​—na wenye wataingia mu taabu kubwa wakiwa waabudu wa kweli—​njo watatiwa alama ya wokovu.

18. (a) Namna gani na wakati gani Yesu Kristo atatia alama wale wenye wanastahili? (b) Je, inaomba watiwa-mafuta nao watiwe alama? Fasiria.

18 Kazi ya kutia alama wale wenye wanastahili itafanyika mbinguni. Mu wakati wa Ezekieli, malaika njo walitia alama ya wokovu juu ya waaminifu. Mu utimizo wa leo wa ile unabii, mwanaume mwenye iko na chombo cha mwandishi cha kuwekea wino anafananisha Yesu Kristo wakati “atakuja katika utukufu wake” juu ya kuhukumu mataifa yote. (Mt. 25:31-33) Yesu atakuja wakati wa taabu kubwa, kisha dini za uongo kuharibiwa. * Ile wakati, mbele tu ya Armagedoni kuanza, Yesu atahukumu watu kwa kuamua kama nani njo kondoo, na nani njo mbuzi. Wale wa “kundi kubwa” watahukumiwa, ao watatiwa alama, ya kuonyesha kama wao ni kondoo, na ile itaonyesha kama wao “wataingia . . . katika uzima wa milele.” (Ufu. 7:9-14; Mt. 25:34-40, 46) Halafu watiwa-mafuta waaminifu? Hawana lazima ya kutiwa alama juu waokoke Armagedoni. Lakini, watatiwa muhuri wao wa mwisho mbele wakufe ao mbele taabu kubwa ianze. Kisha, wakati fulani mbele Armagedoni ianze, watafufuliwa na kuenda mbinguni.​—Ufu. 7:1-3.

19. Ni nani watamusaidia Yesu kuharibu mupangilio huu wa mambo? (Ona kisanduku “Kusumbuka na Kulia kwa Maumivu, Kutiwa Alama, Kuponda-ponda​—Wakati Gani na Namna Gani?”)

19 Mufalme wa mbinguni, Yesu Kristo, na majeshi yake ya mbinguni wataharibu mupangilio huu wa mambo. Mu maono ya Ezekieli, wanaume sita wenye walikuwa na silaha za kuponda-ponda walianza kuharibu wakati tu mwanaume mwenye kuvaa nguo ya kitani alimaliza kazi yake ya kutia alama. (Eze. 9:4-7) Vilevile, uharibifu wenye kuja utaanza kisha Yesu kumaliza kuhukumu mataifa yote na kutia alama ya wokovu juu ya wale wenye kuwa mufano wa kondoo. Kisha, wakati wa vita ya Armagedoni, Yesu ataongoza majeshi ya mbinguni, yenye mutakuwa malaika watakatifu na watawala wenzake 144 000, mu kuharibu kabisa-kabisa dunia hii yenye kuharibika, na kuokoa waabudu wa kweli na kuwaingiza mu dunia mupya.​—Ufu. 16:14-16; 19:11-21.

20. Ni mambo gani ya kutia moyo yenye tunajifunza mu maono ya Ezekieli ya mwanaume mwenye alikuwa na chombo cha mwandishi cha kuwekea wino?

20 Tunafurahia sana mambo ya kutia moyo yenye tunajifunza mu maono ya Ezekieli ya mwanaume mwenye alikuwa na chombo cha mwandishi cha kuwekea wino! Tukuwe hakika kabisa kama Yehova hataharibu wenye haki pamoja na waovu. (Zb. 97:10) Tunajua mambo ya kufanya sasa juu tutiwe alama ya wokovu mu wakati wenye kuja. Kwa sababu tuko waabudu wa Yehova, acha tuazimie kufanya kwa bidii kazi ya kutangaza habari njema na kuonya wale wote wenye wako wanasumbuka na kulia kwa maumivu juu ya ubaya wenye uko mu dunia ya Shetani. Kwa kufanya vile, tunaweza kupata nafasi ya muzuri ya kusaidia wale wenye wako na “muelekeo wenye kufaa kwa ajili ya uzima wa milele” juu wajiunge na sisi mu ibada safi, na hivyo wakuwe ku mustari wa wale wenye watatiwa alama ya wokovu na kuingia mu dunia mupya ya Mungu yenye haki.​—Mdo. 13:48.

^ fu. 1 Maono ya Ezekieli ya mambo ya kuchukiza yenye ilikuwa inafanywa ku hekalu inazungumuziwa mu Sura ya 5 ya kitabu hiki.

^ fu. 13 Kitabu kimoja kinaonyesha kama, nomino ao jina la Kiebrania lenye kutafsiriwa “kosa” linamaanisha “upotovu.” Kitabu kingine kinaonyesha kama ile nomino “ni neno la kidini sana, lenye linatumiwa zaidi sana juu ya kuonyesha hatia kubwa ao uovu mukubwa mbele ya Mungu.”

^ fu. 18 Inaonekana kama, haiko kusema washiriki wote wa dini ya uongo watakufa wakati Babiloni Mukubwa itaharibiwa. Wakati itaharibiwa, hata viongozi fulani wa dini wataweza kuachana na dini ya uongo na kusema kama hawayakuwaka ndani.​—Zek. 13:3-6.