Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kifupi cha Miangaza Mipya

Kifupi cha Miangaza Mipya

Mu miaka mingi, Munara wa Mulinzi umetoa mafasirio ya mupya kuhusu namna tulikuwa tunaelewa sehemu mingi za unabii wa Ezekieli. Na kitabu hiki, Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa Tena!, kiko na miangaza ingine mipya. Ona kama unaweza kujibu maulizo ya kufuata.

Nyuso ine za viumbe vyenye uzima zinafananisha nini?

Namna tulielewa zamani: Uso wa kila kiumbe chenye uzima, ao kerubi, unafananisha moja kati ya sifa ine kubwa za Yehova.

Mwangaza mupya: Hata kama kila uso kati ya zile nyuso ine za vile viumbe vyenye uzima unafananisha moja kati ya sifa ine kubwa za Yehova, wakati tunazitia zote pamoja zile nyuso ine zinafananisha sifa zote zenye Yehova iko nazo. Tena, zile nyuso ine zinatuonyesha ukubwa wa uwezo wa Yehova na utukufu wake.

Juu ya nini tulibadilisha: Mu Neno la Mungu, namba ine inatumiwa mara mingi juu ya kuonyesha kama kitu fulani kinatia ndani kila kitu, ao kiko kamili. Kwa hiyo, wakati nyuso ine zinaonyeshwa pamoja, hazifanyize sifa ine tu za Yehova​—lakini zile sifa njo musingi wa utu wake wa ajabu sana. Tena, kila uso ni wa munyama mwenye anaonyesha ukubwa, uwezo na nguvu. Pia, vile viumbe ine vyenye nguvu vyenye kufananisha uumbaji, kama vile nyuso ine za kila kerubi zinaonyesha, viko chini ya kiti cha ufalme cha Yehova. Ile inaonyesha kama Yehova iko Mutawala Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi juu ya kila kitu.

Mwanaume mwenye kuwa na chombo cha mwandishi cha kuwekea wino anafananisha nani?

Namna tulielewa zamani: Mwanaume mwenye kuwa na chombo cha kuwekea wino anafananisha mabaki ya watiwa-mafuta. Leo, kupitia kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi, watiwa-mafuta wako wanatia alama juu ya mapaji ya nyuso za wale wenye wanakuwa sehemu ya “kundi kubwa.”​—Ufu. 7:9.

Mwangaza mupya: Mwanaume mwenye kuwa na chombo cha mwandishi cha kuwekea wino anafananisha Yesu Kristo. Atatia alama juu ya watu wa kundi kubwa wakati atawahukumu kuwa kondoo wakati wa “taabu kubwa.”​—Mt. 24:21.

Juu ya nini tulibadilisha: Yehova amepatia Mwana wake daraka la kuhukumu. (Yoh. 5:22, 23) Kulingana na Matayo 25:31-33, Yesu njo atatoa hukumu ya mwisho ya kuonyesha kama nani njo “kondoo” na nani njo “mbuzi.”

Je, dada makahaba, Ohola na Oholiba, wanafananisha Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo zenye kugawanyika mu sehemu mbili: Kanisa Katoliki na Kanisa la Kiprotestanti?

Namna tulielewa zamani: Ohola (Samaria, muji mukubwa wa Israeli), dada mukubwa, anafananisha Kanisa Katoliki; Oholiba (Yerusalemu, muji mukubwa wa Yuda), dada mudogo, anafananisha Kanisa la Kiprotestanti.

Mwangaza mupya: Wale dada makahaba hawafananishe sehemu yoyote ya Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo. Lakini, habari yao inatufundisha namna Yehova anajisikia wakati watumishi wake waaminifu wanageuka na kufanya ukahaba wa kiroho. Ni vile anajisikia pia kuhusu dini zote za uongo.

Juu ya nini tulibadilisha: Hakuna musingi wowote wa Kimaandiko wenye unaonyesha kama Ohola na Oholiba wanafananisha Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo. Wakati fulani, Israeli na Yuda walikuwa bibi waaminifu wa Yehova, lakini Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo hazijakuwaka na uhusiano wa vile na Yehova. Tena, habari yenye inalinganisha watu wa Mungu wenye walikosa uaminifu na makahaba mu sura ya 16 na 23 ya kitabu cha Ezekieli inatoa tumaini lenye kuonyesha kama mambo ingebadilika na kurudia mu hali ya muzuri. Lakini, Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo, zenye ziko sehemu ya Babiloni Mukubwa, hazina tumaini la vile hata kidogo.

Je, Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo zinafananisha Yerusalemu ya zamani yenye iliasi?

Namna tulielewa zamani: Yerusalemu yenye ilikosa uaminifu inafananisha Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo. Kwa hiyo, uharibifu wa Yerusalemu unafananisha uharibifu wa Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo.

Mwangaza mupya: Hali zenye zilikuwa mu Yerusalemu yenye ilikosa uaminifu​—sawa vile kuabudu sanamu na upotovu wenye kuenea sana—​zinafanana na hali zenye ziko mu Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo, lakini hatuseme tena kama Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo zinafananisha Yerusalemu ya zamani.

Juu ya nini tulibadilisha: Hakuna musingi wowote wa Kimaandiko wenye unaonyesha waziwazi kama Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo zinafananisha Yerusalemu ya zamani yenye iliasi. Tofauti na Yerusalemu ya zamani, Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo hazijafanyaka ibada safi. Na hata kama Yerusalemu ilifikiaka wakati fulani kupata musamaha wa Yehova, hakuna tumaini la vile kwa ajili ya Dini Zenye Kujiita Kuwa za Kikristo.

Maono ya bonde la mifupa yenye kukauka ilitimia namna gani?

Namna tulielewa zamani: Mu mwaka wa 1918 watiwa-mafuta wenye waliteswa walipelekwa mu utekwa wa Babiloni Mukubwa, na walikuwa mu hali yenye inafanana na kifo yenye inakaribiana na hali ya kutotenda. Ile utekwa iliisha mu mwaka wa 1919 wakati Yehova aliwatia tena nguvu juu watangaze Ufalme.

Mwangaza mupya: Hali yenye inafanana na kifo ya utekwa wa kiroho ilifanya miaka mingi sana na ilianza miaka mingi mbele ya mwaka wa 1918. Ilianza mu karne ya pili (101-200) K.K.Y. na kuisha mu mwaka wa 1919 K.K.Y. na inafanana na kipindi kirefu cha kukomaa kwa mbegu mu mufano wa Yesu wa ngano na magugu.

Juu ya nini tulibadilisha: Utekwa wa Israeli ya zamani ulifanyaka miaka mingi, ulianza mu mwaka wa 740 M.K.Y. na kumalizika mu mwaka wa 537 M.K.Y. Unabii wa Ezekieli unasema kama mifupa ilikuwa “yenye kukauka” ao “yenye kukauka sana,” ile inaonyesha kama wale wenye kufananishwa na ile mifupa walikuwa wamekufa tangu zamani sana. Na unabii unaonyesha namna ile mifupa inarudishwa hatua kwa hatua mu hali ya muzuri, ile yote ilikamata wakati murefu.

Kuunganishwa pamoja kwa vipande mbili vya muti kuko na maana gani?

Namna tulielewa zamani: Kisha kipindi kifupi cha mugawanyiko wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, washiriki waaminifu wa mabaki ya watiwa mafuta walirudia tena mu umoja mu mwaka wa 1919.

Mwangaza mupya: Ile unabii inaonyesha kwamba Yehova atafanya waabudu wake wakuwe mu umoja. Kisha 1919, kadiri wakati ilipita, hesabu yenye kuongezeka ya watu wenye kuwa na tumaini la kuishi ku dunia ilijiunga na mabaki ya watiwa- mafuta. Vikundi vyote mbili viko vinamuabudu Yehova pamoja kama kikundi kimoja cha watu.

Juu ya nini tulibadilisha: Ile unabii haiseme kama kipande cha muti kinapasuliwa kwanza mara mbili na kisha kinaunganishwa na kuwa kipande kimoja. Kwa hiyo, ile unabii haiseme kama kikundi kimoja kingegawanyika na kisha kingerudia mu umoja. Lakini, inaonyesha namna vikundi mbili tofauti vingeungana mu umoja.

Gogu wa Magogu ni nani?

Namna tulielewa zamani: Gogu wa Magogu ni jina la kiunabii la Shetani kisha yeye kufukuzwa mbinguni.

Mwangaza mupya: Gogu wa Magogu ni muungano wa mataifa ya ku dunia yenye itashambulia waabudu wa kweli wakati wa taabu kubwa.

Juu ya nini tulibadilisha: Maelezo yenye unabii unatoa kuhusu Gogu​—kwa mufano, ya kusema kama atapewa kuwa chakula kwa ndege wa kuwinda na kupewa kaburi ku dunia—​inaonyesha kama Gogu haiko kiumbe cha kiroho. Tena, shambulizi la Gogu linafanana na mambo yenye kuzungumuziwa mu kitabu cha Danieli na cha Ufunuo kuhusu shambulizi lenye mataifa ya dunia italeta juu ya watu wa Mungu.​—Da. 11:40, 44, 45; Ufu. 17:14; 19:19.

Je, Ezekieli aliona na kutembea mu hekalu kubwa la kiroho lenye mutume Paulo alizungumuzia kisha?

Namna tulielewa zamani: Hekalu lenye Ezekieli alionaka mu maono njo hekalu la kiroho lenye mutume Paulo alizungumuzia.

Mwangaza mupya: Ezekieli hakuona hekalu la kiroho lenye lilianza mu mwaka wa 29 K.K.Y., lakini aliona maono yenye ilionyesha namna ibada safi yenye ilizungumuziwa mu Sheria ya Musa ingerudishwa kisha uhamisho. Mafasirio ya Paulo yenye iliongozwa na roho ya Mungu kuhusu hekalu la kiroho inakazia zaidi sana kazi yenye Yesu, Kuhani Mukubwa Zaidi, alifanya kuanzia mwaka 29 mupaka 33 K.K.Y. Maono ya Ezekieli ya hekalu, yenye haitaje hata kidogo kuhani mukubwa, inakazia zaidi sana kurudishwa kwa ibada safi kwenye kulianza mu mwaka wa 1919 K.K.Y. Njo maana hatutafute tena kujua kama mambo yote ya kidogo-kidogo na vipimo vya hekalu lenye Ezekieli alionaka mu maono iko na maana gani ya kiunabii. Kuliko kufanya vile, tunatafuta zaidi sana somo zenye maono ya Ezekieli inatufundisha kuhusu kanuni za Yehova kwa ajili ya ibada safi.

Juu ya nini tulibadilisha: Hekalu lenye Ezekieli alionaka mu maono liko tofauti na hekalu la kiroho mu njia fulani za maana. Kwa mufano, zabihu mingi za wanyama zinatolewa ku hekalu la Ezekieli; ku hekalu la kiroho, zabihu moja tu njo inatolewa, “mara moja kwa wakati wote.” (Ebr. 9:11, 12) Miaka mingi mbele Kristo akuje, wakati ilikuwa haijafika juu Yehova afunue kweli nzito juu ya hekalu la kiroho.