Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 21

“Jina la Muji Huo . . . Litakuwa, Yehova Iko Pale”

“Jina la Muji Huo . . . Litakuwa, Yehova Iko Pale”

EZEKIELI 48:35

WAZO KUBWA: Maana ya muji na muchango

1, 2. (a) Ni sehemu gani ya pekee ya inchi yenye inapaswa kutiwa pembeni? (Ona picha ku jalada ao couverture.) (b) Ile maono ilipatia wahamishwa uhakikisho gani?

MU MAONO yake ya mwisho, Ezekieli anaona kwamba kuko sehemu moja ya inchi yenye inatiwa pembeni juu ya kusudi fulani la pekee. Ile sehemu yenye inatiwa pembeni, haiko uriti wa kabila fulani la Israeli, lakini inatolewa kuwa muchango kwa Yehova. Ezekieli anaona pia muji mukubwa wenye uko na jina la kushangaza. Sehemu hii ya maono inapatia wahamishwa uhakikisho huu wa maana sana: Yehova atakuwa nao wakati watarudia mu inchi yao yenye wanapenda.

2 Ezekieli anatutolea mafasirio yenye kuwa wazi kuhusu ile muchango. Acha tuchunguze habari hii yenye iko na maana kwetu leo, sisi watumishi wa kweli wa Yehova.

“Muchango Mutakatifu Pamoja na . . . Muji”

3. Sehemu ya inchi yenye Yehova alitia pembeni ilikuwa na maeneo gani tano, na kila eneo lilikuwa na kazi gani? (Ona kisanduku “Muchango Wenye Mutatia Pembeni.”)

3 Sehemu ya inchi yenye kuwa ya pekee ilikuwa na urefu wa mikono 25 000 (kilometre 13) kutoka kaskazini mupaka kusini na urefu wa mikono 25 000 kutoka mashariki mupaka mangaribi. Ile sehemu ya inchi yenye pande ine zenye kuwa sawasawa iliitwa “muchango muzima.” Iligawanywa mu sehemu tatu tambarare. Sehemu ya juu ilikuwa ya Walawi, na sehemu ya katikati ilitiwa pembeni kwa ajili ya hekalu na makuhani. Zile sehemu mbili zilifanyiza “muchango mutakatifu.” Sehemu ya chini ya kidogo sana, ao ‘eneo lenye lilibakia,’ ilikuwa kwa ajili ya “matumizi ya kawaida.” Ilikuwa kwa ajili ya muji.​—Eze. 48:15, 20.

4. Habari juu ya muchango kwa ajili ya Yehova inatufundisha nini?

4 Habari juu ya muchango kwa ajili ya Yehova inatufundisha nini? Kwa kutia pembeni kwanza sehemu moja ya inchi kwa ajili ya muchango wa pekee na kisha sehemu ingine ya inchi kwa ajili ya makabila, Yehova alionyesha kama mambo ya kiroho njo ilipaswa kuhangaikiwa kwanza. (Eze. 45:1) Kuona kama muchango kwa ajili ya Yehova njo ulitiwa kwanza pembeni wakati wa kugawanya inchi, kulipaswa kupatia wahamishwa somo fulani ya maana sana. Walipaswa kutia ibada ya Yehova pa nafasi ya kwanza kabisa mu maisha yao. Leo, tunaona pia mambo ya kiroho, sawa vile kujifunza Neno la Mungu, kuhuzuria mikutano ya Kikristo, na kazi ya kuhubiri, kuwa mambo ya maana zaidi, yenye tunapaswa kutanguliza kwanza. Mufano wa Yehova unatufundisha kwamba tunapaswa kutia mambo ya kiroho pa nafasi ya kwanza mu maisha yetu.

“Muji Utakuwa Katikati Yake”

5, 6. (a) Muji ao eneo la muji lilikuwa la nani? (b) Ile muji haifananishe nini, na juu ya nini tunasema vile?

5 Soma Ezekieli 48:15. “Muji” pamoja na sehemu yenye kuizunguka ni nini? (Eze. 48:16-18) Mu maono, Yehova aliambia Ezekieli hivi: ‘Eneo la muji . . . litakuwa la nyumba yote ya Israeli.’ (Eze. 45:6, 7) Kwa hiyo, muji pamoja na sehemu yenye kuizunguka haikukuwa sehemu ya muchango wenye ulipaswa ‘kutiwa pembeni kwa ajili ya Yehova.’ (Eze. 48:9) Tukiwa na ile tofauti mu akili, acha sasa tuone mambo yenye ile mupango kwa ajili ya muji inatufundisha leo.

6 Juu ya kujua mambo yenye ile muji inatufundisha, ni muzuri kwanza tujue ile muji haiwezi kuwa nini. Ile muji haiwezi kufananisha muji wa Yerusalemu wenye ulijengwa upya pamoja na hekalu lake. Juu ya nini tunasema vile? Juu, ile muji yenye Ezekieli aliona mu maono haingekuwa na hekalu. Tena, ile muji haikufananisha muji ingine mu inchi ya Israeli yenye ilirudishwa mu hali ya muzuri. Juu ya nini tunasema vile? Juu, wahamishwa wenye walirudiaka mu inchi yao ao wazao wao hawakujengaka muji wenye ulikuwa na mambo mbalimbali kama ile yenye maono inataja. Zaidi ya ile, ile muji haiwezi kufananisha muji wa mbinguni. Juu ya nini tunasema vile? Juu, ile muji ilijengwa ku sehemu ya inchi yenye ilikuwa ya “matumizi ya kawaida [ao, yenye haiko takatifu].” Sehemu ya inchi yenye ni ya matumizi ya kawaida ilikuwa tofauti na sehemu ya inchi yenye ilikuwa kwa ajili ya ibada tu.​—Eze. 42:20.

7. Muji wenye Ezekieli alionaka, ni muji wa namna gani, na inaonekana kama unafananisha nini? (Ona picha ku mwanzo wa habari.)

7 Sasa, muji wenye Ezekieli alionaka, ni nini? Kumbuka kwamba Ezekieli aliona ile muji na ile inchi mu maono ileile. (Eze. 40:2; 45:1, 6) Neno la Mungu linaonyesha kama ile inchi inafananisha inchi ya kiroho, kwa hiyo ule muji unapaswa pia kufananisha muji wa kiroho. Kwa kawaida, wakati mutu anasikia neno “muji,” anaonaka nini mu akili yake? Anaonaka watu wenye kuishi pamoja mu kikundi na wenye kupangwa muzuri. Kwa hiyo, inaonekana kama ule muji wenye kupangwa muzuri wenye Ezekieli alionaka​—wenye ulikuwa na pande ine zenye kuwa sawasawa kabisa—​unafananisha usimamizi wenye kupangwa muzuri.

8. Usimamizi unafanyia kazi wapi, na juu ya nini tunasema vile?

8 Sasa, usimamizi unafanyia kazi wapi? Maono ya Ezekieli inaonyesha kwamba ule muji unafanyia kazi ndani ya inchi ya kiroho. Kwa hiyo, ule usimamizi unafanyia kazi leo ndani ya eneo la watu wa Mungu, ni kusema, unaongoza kazi ya watu wa Mungu. Sasa, kwa kuwa ule muji unajengwa ku sehemu ya inchi yenye ni ya matumizi ya kawaida, ao yenye haiko takatifu, ile inaonyesha nini? Inaonyesha kwamba ule muji haufananishe muji fulani wa mbinguni, lakini unafananisha usimamizi wa kidunia, wenye umekuwa ukifanya kazi kwa faida ya wale wote wenye wanaishi mu paradiso ya kiroho.

9. (a) Ni nani wanafanyiza usimamizi wa kidunia leo? (b) Yesu atafanya nini wakati wa Miaka Elfu?

9 Ni nani wanafanyiza usimamizi wa kidunia? Mu maono ya Ezekieli, mwenye kuongoza serikali ya ule muji aliitwa “mukubwa.” (Eze. 45:7) Alikuwa mwangalizi kati ya watu, lakini hakukuwa kuhani wala Mulawi. Mukubwa huyu anatukumbusha zaidi sana waangalizi wa kutaniko leo wenye hawako watiwa-mafuta. Wachungaji hawa wa kiroho wenye kuwa na upendo na wenye kutoka katika “kondoo wengine” ni watumishi wanyenyekevu wa kidunia wa serikali ya mbinguni ya Kristo. (Yoh. 10:16) Mu Miaka Elfu yenye kuja, Yesu atachagua na kuweka wazee wenye kustahili, ao “wakubwa” mu “dunia yote.” (Zb. 45:16) Chini ya uongozi wa Ufalme wa mbinguni, watasimamia mambo ya watu wa Mungu mu ile Miaka Elfu.

“Yehova Iko Pale”

10. Ule muji uko na jina gani, na ile inahakikisha nini?

10 Soma Ezekieli 48:35. Jina la muji ni “Yehova Iko Pale.” Ile jina inahakikisha kwamba ni muji kwenye watu wanaona kuwa Yehova iko katikati yao kabisa. Kwa kweli, kwa kuonyesha Ezekieli ule muji, Yehova alikuwa anaambia hivi wahamishwa: ‘Nitakuwa na nyiye tena!’ Ni uhakikisho wenye kutia moyo sana!

11. Maono ya Ezekieli juu ya muji na maana ya jina la muji inatufundisha nini?

11 Sehemu hii ya unabii wa Ezekieli inaweza kutufundisha nini? Jina la ule usimamizi wenye kufanana na muji linahakikishia watumishi wa Mungu leo kama Yehova iko pamoja na watumishi wake waaminifu wa ku dunia na ataendelea kuwa nao. Ile jina yenye kuwa na maana kubwa inaonyesha pia kweli hii ya lazima: Ule muji uko, hapana juu ya kupatia mutu fulani utukufu, lakini juu ya kuendelesha njia za Yehova zenye upendo na zenye kuwa sawa. Kwa mufano, Yehova hakupatia ule usimamizi mamlaka ya kugawanya inchi, hata kama wanadamu wanaweza kuona kuwa ni muzuri afanye vile. Tofauti na ile, Yehova anatazamia wasimamizi waheshimie maeneo, ao madaraka, yenye yeye mwenyewe amepatia watumishi wake, kutia ndani watu wa “hali ya chini.”​—Mez. 19:17; Eze. 46:18; 48:29.

12. (a) Ni jambo gani la kushangaza kuhusu muji, na ile inaonyesha nini? (b) Sehemu hii ya maono inakumbusha waangalizi Wakristo jambo gani la lazima?

12 Ni jambo gani lingine la kushangaza kuhusu ule muji wenye kuitwa “Yehova Iko Pale”? Miji ya zamani ilikuwa na kuta za ulinzi na pia hesabu kidogo ya milango mikubwa kadiri iliwezekana, lakini hii muji iko na milango mikubwa 12! (Eze. 48:30-34) Hesabu kubwa ya milango mikubwa (tatu ku kila upande wa muji wenye pande ine zenye kuwa sawasawa) inaonyesha kama wasimamizi wa muji ni watu wenye mutu hawezi kuogopa kuzungumuza nao na wako tayari kusaidia kila mutumishi wa Mungu. Tena, milango mikubwa 12 inaonyesha kama ile muji iko wazi kwa ajili ya kila mutu, kwa ajili ya “nyumba yote ya Israeli.” (Eze. 45:6) Ule muji ulikuwa na milango mingi, na ile ilifanya ikuwe mwepesi kuingia ndani. Ile inakumbusha waangalizi Wakristo jambo fulani la lazima: Yehova anapenda wakuwe wenye urafiki na wenye mutu hawezi kuogopa kuzungumuza nao na wakuwe tayari kusaidia kila mutu mwenye anaishi mu paradiso ya kiroho.

Waangalizi Wakristo ni watu wenye mutu hawezi kuogopa kuzungumuza nao na wako tayari kusaidia wengine (Ona fungu la 12)

Watu wa Mungu “Wanaingia ili Kuabudu” na “Kutumikia Muji”

13. Ni kazi gani mbalimbali zenye Yehova alisema kama watu wangefanya?

13 Turudie kidogo mu wakati wa Ezekieli na tuone nini ingine anasema mu ile maono yenye ilionyesha namna inchi ilipaswa kugawanywa. Yehova anazungumuzia watu wenye kufanya aina mbalimbali za utumishi. “Watumishi wa patakatifu,” ni kusema, makuhani, walipaswa kutoa zabihu na kumukaribia Yehova juu ya kumutumikia. Na “Watumishi wa hekalu,” ni kusema, Walawi, walipaswa “kushugulikia utumishi wake [hekalu] na mambo yote yenye yanapaswa kufanywa ndani.” (Eze. 44:14-16; 45:4, 5) Zaidi ya ile, wafanyakazi wangekuwa wanatumikia karibu na muji. Wale wafanyakazi ni nani?

14. Wafanyakazi wenye kuwa karibu na muji wanatukumbusha nini?

14 Wale wafanyakazi wenye kuwa karibu na muji wanatoka mu “makabila yote ya Israeli.” Kazi yao ni kusaidia. Wanalima mashamba yenye “yatatoa chakula” kwa ajili ya “wale wenye wanatumikia muji.” (Eze. 48:18, 19) Je, ile inatukumbusha jambo fulani lenye sisi pia tunafanya leo? Ndiyo. Leo, wakaaji wote wa paradiso ya kiroho wako na nafasi ya kutegemeza utumishi wa ndugu watiwa-mafuta wa Kristo na utumishi wa washiriki fulani wa “kundi kubwa” wenye Yehova ameweka juu ya kuongoza. (Ufu. 7:9, 10) Njia moja kubwa ya kuonyesha kama tunategemeza utumishi wao ni kuunga mukono uongozi wenye unatoka kwa mutumwa muaminifu.

15, 16. (a) Ni mambo gani ingine tunajifunza mu maono ya Ezekieli? (b) Tuko na nafasi ya kufanya kazi gani yenye kufanana na ile ya wale wafanyakazi?

15 Maono ya Ezekieli iko tena na jambo lingine lenye linaweza kutupatia somo fulani kuhusu kazi ya kuhubiri. Ni jambo gani? Yehova anaonyesha kama watu wa makabila 12 yenye haiko ya Walawi wangekuwa wanafanyia kazi fasi mbili: mu uwanja wa hekalu na mu eneo la kulishia wanyama la muji. Ni kazi gani wangefanyia mu kila fasi? Mu uwanja wa hekalu, watu wa makabila yote ‘wangeingia ili kuabudu’ kwa kumutolea Yehova zabihu. (Eze. 46:9, 24) Mu eneo la muji, watu wa makabila yote wangekuja kutegemeza muji kwa kulima udongo wa muji. Mufano wa wale wafanyakazi unatufundisha nini?

16 Leo, washiriki wa “kundi kubwa” wanafanya kazi sawa zile zenye zilikuwa zinafanywa na wale wenye Ezekieli aliona mu maono. Wanamuabudu Yehova “katika hekalu lakekwa kutoa zabihu za sifa. (Ufu. 7:9-15) Wanafanya vile kwa kushiriki mu kazi ya kuhubiri na kwa kutoa maelezo yenye kujaa imani ku mikutano ya Kikristo. Wanaona ibada yenye wanamutolea Yehova moja kwa moja kuwa daraka kubwa sana. (1 Ny. 16:29) Zaidi ya ile, wengi kati ya watu wa Mungu wanaweza kutegemeza tengenezo la Mungu mu njia mingi. Kwa mufano, wamoja wanasaidia mu kazi ya kujenga na kutunza Majumba ya Ufalme na biro za tawi, na wanasaidia pia mu mipango mbalimbali ya tengenezo la Yehova. Wengine wanategemeza ile mipango kwa kutoa michango. Wakati wanafanya vile, ni sawa vile wanalima inchi, “kwa utukufu wa Mungu.” (1 Ko. 10:31) Wanafanya kazi kwa bidii na furaha kwa sababu wanajua kama Yehova “anapendezwa na zabihu za namna hiyo.” (Ebr. 13:16) Je, wewe pia unafanya vile?

Maelezo ya Ezekieli kuhusu kazi mbalimbali zenye zilikuwa zinafanywa ndani na pembeni-pembeni ya milango mikubwa ya muji inatufundisha nini? (Ona fungu la 14-16)

“Tunangojea Mbingu Mupya na Dunia Mupya”

17. (a) Namna gani maono ya Ezekieli juu ya muchango itatimia mu njia kubwa zaidi mu wakati wenye kuja? (b) Mu Miaka Elfu, kazi ya usimamizi wenye kufananishwa na muji italetea nani faida?

17 Je, mu wakati wenye kuja, maono ya Ezekieli juu ya muchango itatimia mu njia kubwa zaidi? Ndiyo! Fikiria jambo hili: Ezekieli aliona kama sehemu moja ya inchi yenye iliitwa “muchango mutakatifu” ilikuwa mu katikati ya inchi. (Eze. 48:10) Vilevile, kisha Armagedoni, hata tuishi wapi mu dunia, Yehova atakaa pamoja na sisi. (Ufu. 21:3) Mu Miaka Elfu, usimamizi wenye kufananishwa na muji, ni kusema, wale wenye hapa ku dunia watawekwa juu ya kusimamia mambo ya watu wa Mungu, utaeneza mamlaka yake mu dunia yote kwa kutolea muongozo na maagizo yenye upendo wale wote wenye kufanyiza “dunia mupya,” maana yake familia mupya ya wanadamu.​—2 Pe. 3:13.

18. (a) Juu ya nini tukuwe hakika kama usimamizi wenye kufananishwa na muji utatumika kwa umoja na utawala wa Mungu? (b) Jina la muji linatuhakikishia nini?

18 Juu ya nini tukuwe hakika kama usimamizi wenye kufananishwa na muji utatumika kwa umoja kabisa na utawala wa Mungu? Juu, Neno la Mungu linaonyesha waziwazi kwamba muji wa kidunia wenye uko na milango mikubwa 12 ni mufano wa muji wa mbinguni​—Yerusalemu Mupya—​wenye kuwa na milango mikubwa 12, wenye kufanyizwa na wale 144 000 wenye watatawala na Kristo. (Ufu. 21:2, 12, 21-27) Ile inaonyesha kama maamuzi ya ule usimamizi wa kidunia itapatana kabisa na maamuzi yenye Ufalme wa Mungu umekamata kule mbinguni na itatimiza ile maamuzi kwa ukamili. Ndiyo, jina la muji “Yehova Iko Pale” linatuhakikishia sisi wote kama ibada safi itadumu milele na milele mu Paradiso. Mambo ya muzuri sana iko inatuchunga!