Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 1B

Kifupi cha Habari Zenye Kuwa Katika Ezekieli

Kifupi cha Habari Zenye Kuwa Katika Ezekieli

Kwa kifupi, kitabu cha Ezekieli kinaweza kugawanywa hivi:

SURA YA 1-3

Mwaka wa 613 M.K.Y., wakati alikuwa anaishi kati ya Wayahudi wenye walipelekwa mu uhamisho Babiloni, Ezekieli anaona maono ya Yehova na anapewa mugao wa kutolea unabii Wayahudi wenye walikuwa wanaishi karibu na muto Kebari.

SURA YA 4-24

Kati ya mwaka wa 613 na 609 M.K.Y., Ezekieli anatoa ujumbe mbalimbali wa kiunabii wenye kuzungumuzia zaidi sana hukumu juu ya Yerusalemu na watu wake waasi, wenye kuabudu sanamu.

SURA YA 25-32

Kuanzia mwaka wa 609 M.K.Y., mwaka wenye Babiloni inaanza kuzunguka Yerusalemu kwa mara ya mwisho kwa ajili ya vita, Ezekieli anaacha kutoa ujumbe wa hukumu juu ya Yerusalemu, anageukia sasa mataifa adui yenye kuzunguka Israeli​—Amoni, Edomu, Misri, Moabu, Ufilisti, Sidoni, na Tiro.

SURA YA 33-48

Kuanzia mwaka wa 606 M.K.Y., Yerusalemu na hekalu lake vimekuwa mabomoko, mbali, ku mamia ya kilometre. Sasa Ezekieli anakazia ujumbe wa tumaini​—ujumbe wa kufurahisha wa kurudishwa kwa ibada safi ya Yehova Mungu.

Kwa hiyo, kitabu cha Ezekieli kimepangwa kulingana na namna matukio ilifuatana na pia kulingana na habari. Kwanza, maunabii kuhusu uharibifu wa Yerusalemu na hekalu lake inatolewa, kisha maunabii mingi kuhusu kurudishwa kwa ibada safi inafuata. Ile inapatana na akili, kwa sababu maunabii kuhusu kurudishwa kwa ibada safi inaonyesha kwamba ibada safi ilikuwa haifanyike tena ku hekalu.

Zaidi ya ile, maunabii ya Ezekieli juu ya mataifa adui yenye kuzunguka Israeli (sura ya 25-32) inapatikana kati ya ujumbe wake wa hukumu juu ya Yerusalemu na maunabii juu ya kurudishwa kwa ibada safi. Kuhusu ujumbe mbalimbali wa hukumu wenye Ezekieli alitolea ile mataifa, mutu moja mwenye elimu mingi alisema: “Ile ujumbe ni badiliko lenye kufaa kutoka tangazo la kasirani kali ya Mungu mupaka tangazo la rehema Yake kuelekea watu wake, kwa sababu kupatia maadui wao azabu ni sehemu ya ukombozi wa watu Wake.”

Rudia ku sura ya 1, fungu la 18