Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 10B

Kuna Uhusiano Gani Kati ya “Mifupa Mikavu” na ‘Mashahidi Wawili’?

Kuna Uhusiano Gani Kati ya “Mifupa Mikavu” na ‘Mashahidi Wawili’?

MWAKA wa 1919 unabii kuhusu “mifupa mikavu” na unabii kuhusu ‘mashahidi wawili’ ulitimizwa, kuna uhusiano kati ya unabii huo. Maono kuhusu “mifupa mikavu” yalitabiri kipindi kirefu sana (kipindi cha karne nyingi sana) kilichofikia mwisho kundi kubwa la watu wa Mungu lilipokuwa hai tena. (Eze. 37:2-4; Ufu. 11:1-3, 7-13) Unabii kuhusu ‘mashahidi wawili’ unaelezea kipindi kifupi (kilichotimizwa kuanzia mwishoni mwa 1914 hadi mwanzoni mwa 1919) kilichofikia mwisho kikundi kidogo cha watumishi wa Mungu kilipokuwa hai tena. Unabii huo wote ulionyesha kufufuliwa kwa njia ya mfano, na ulitimizwa nyakati zetu mwaka wa 1919 Yehova alipofanya watumishi wake waliotiwa mafuta ‘wasimame kwa miguu yao,’ watoke katika utekwa wa Babiloni Mkubwa, na kukusanywa katika kutaniko lililorudishwa.—Eze. 37:10.

Hata hivyo, ona kwamba kutimizwa kwa unabii huo kunatofautiana kwa njia muhimu sana. Unabii kuhusu “mifupa mikavu” ulitabiri kuwa hai tena kwa watiwa mafuta wote waliobaki. Hata hivyo, unabii kuhusu ‘mashahidi wawili’ ulitabiri kuwa baadhi ya watiwa mafuta wa Mungu waliobaki wangekuwa hai tena—watiwa mafuta hao waliokuwa wakiongoza katika tengenezo waliwekwa rasmi kuwa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.”—Mt. 24:45; Ufu. 11:6. *

“Bonde Tambarare . . . Lililojaa Mifupa”​—Eze. 37:1

  1. BAADA YA 100 W.K.

    Kuanzia karne ya pili W.K. na kuendelea kutaniko la Wakristo waliotiwa mafuta lilipouawa kwa njia ya mfano, “bonde tambarare” lilijaa “mifupa”

  2. MWANZONI MWA 1919

    1919: “Mifupa mikavu” ilikuwa hai tena Yehova alipofanya watiwa mafuta wote watoke katika Babiloni Mkubwa na kukusanywa katika kutaniko lililorudishwa

‘Mashahidi Wawili’​—Ufu. 11:3

  1. MWISHONI MWA 1914

    kuhubiri “wakiwa wamevaa nguo za magunia”

    1914: ‘Mashahidi wawili’ walihubiri “wakiwa wamevaa nguo za magunia” kwa miaka mitatu na nusu. Baada ya kipindi hicho waliuawa kwa njia ya mfano

  2. kifo cha mfano

  3. MWANZONI MWA 1919

    1919: ‘Mashahidi wawili’ walikuwa hai tena kikundi kidogo cha ndugu waliotiwa mafuta kilipokuwa kikiongoza katika tengenezo na kuwekwa rasmi kuwa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara”

^ fu. 4 Tazama gazeti Mnara wa Mlinzi la Machi 2016, “Maswali Kutoka kwa Wasomaji.”