Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 10B

Kuko Upatano Gani Kati ya “Mifupa Yenye Kukauka” na “Mashahidi Wawili?”

Kuko Upatano Gani Kati ya “Mifupa Yenye Kukauka” na “Mashahidi Wawili?”

MU Mwaka wa 1919, maunabii mbili yenye kupatana ilitimia: ya kwanza inahusu “mifupa yenye kukauka,” na ya pili inahusu “mashahidi wawili.” Maono kuhusu “mifupa yenye kukauka” inaonyesha kipindi kirefu sana (chenye kilifanya mamia ya miaka) chenye kilimalizika wakati kikundi kikubwa cha watu wa Mungu kilianza kuishi tena. (Eze. 37:2-4; Ufu. 11:1-3, 7-13) Unabii kuhusu wale “mashahidi wawili” unaonyesha kipindi kifupi (chenye kilitimia ku mwisho wa 1914 mupaka ku mwanzo wa 1919) chenye kilimalizika wakati kikundi kidogo cha watumishi wa Mungu kilianza kuishi tena. Hii maunabii yote mbili ilionyesha ufufuo wa mufano, na yote mbili ilitimia wakati wetu mu mwaka wa 1919 wakati Yehova alifanya watiwa-mafuta wake ‘wasimame kwa miguu yao,’ kwa kuwatosha mu utekwa wa Babiloni Mukubwa, na kuwakusanya mu kutaniko lenye lilirudishwa.​—Eze. 37:10.

Lakini, kuko tofauti moja kubwa mu utimizo wa ile maunabii mbili. Unabii kuhusu “mifupa yenye kukauka” unatabiri kuishi tena kwa washiriki wote wa mabaki ya watiwa-mafuta wa Mungu. Lakini, unabii kuhusu “mashahidi wawili” unatabiri kuishi tena kwa washiriki fulani wa mabaki ya watiwa-mafuta wa Mungu​—wale wenye walikuwa wanaongoza mambo mu tengenezo (wenye kufananishwa na Musa na Eliya) na wenye waliwekwa kuwa “mutumwa muaminifu na mwenye busara.”​—Mt. 24:45; Ufu. 11:6. *

‘Bonde Tambarare . . .Lenye Kujaa Mifupa’​—Eze. 37:1

  1. KISHA 100 K.K.Y.

    Kuanzia karne ya pili (101-200) K.K.Y. na kuendelea wakati kutaniko la Kikristo lenye kutiwa-mafuta liliuawa mu njia ya mufano, “bonde tambarare” lilijaa “mifupa”

  2. KU MWANZO WA 1919

    1919: Ile “mifupa yenye kukauka” iliishi tena wakati Yehova alitosha watiwa-mafuta mu Babiloni Mukubwa na kuwakusanya mu kutaniko lenye lilirudishwa

“Mashahidi Wawili”​—Ufu. 11:3

  1. KU MWISHO WA 1914

    wanahubiri “wakiwa wamevaa nguo za magunia”

    1914: Wale “mashahidi wawili” walihubiri “wakiwa wamevaa nguo za magunia” mu miaka tatu na nusu. Ku mwisho wa ile kipindi, waliuawa mu njia ya mufano

  2. kifo cha mufano

  3. KU MWANZO WA 1919

    1919: Wale “mashahidi wawili” waliishi tena wakati kikundi kidogo cha ndugu watiwa-mafuta kilianza kuongoza mambo mu tengenezo na kikawekwa kuwa “mutumwa muaminifu na mwenye busara”

^ fu. 4 Ona Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 3, 2016, kwenye sehemu “Maulizo ya Wasomaji Wetu.”