Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 10C

Msaada wa Kusimama Tena

Msaada wa Kusimama Tena

TUNAWEZA kuimarishwa kwa kutafakari somo tunalopata kutokana na maono haya yenye kustaajabisha yaliyoandikwa kwenye Ezekieli 37:1-14, somo ambalo tunaweza kulitumia maishani. Ni somo gani?

Nyakati nyingine, huenda tukalemewa na mikazo na majaribu maishani hivi kwamba tukachoka na kushindwa kusonga mbele. Hata hivyo, nyakati kama hizo, tunaweza kuimarishwa tukitafakari maelezo yaliyo wazi ya maono ya Ezekieli kuhusu kurudishwa. Kwa nini? Tunajifunza kutokana na unabii huo kwamba Mungu anayeweza kupuliza uhai ndani ya mifupa iliyokufa kwa kweli anaweza kutupatia nguvu tunazohitaji ili kushinda vikwazo—hata vikwazo ambavyo kwa maoni ya kibinadamu hatuwezi kuvishinda.—Soma Zaburi 18:29; Flp. 4:13.

Huenda tukakumbuka kwamba karne nyingi kabla ya siku za Ezekieli, nabii Musa alisema kwamba Yehova ana nguvu na pia anatamani kutumia nguvu zake kwa ajili ya watu wake. Musa aliandika hivi: “Mungu ni kimbilio tangu nyakati za kale, mikono yake ya milele iko chini yako.” (Kum. 33:27) Naam, tunaweza kuwa na uhakika kwamba tukimtegemea Mungu nyakati za taabu, Yehova ataweka mikono yake yenye upendo chini yetu, atatuinua kwa wororo, na kutusaidia kusimama tena.—Eze. 37:10.