Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KISANDUKU CHA KUFUNDISHIA 10C

Jambo la Kutusaidia Tusimame Tena kwa Miguu Yetu

Jambo la Kutusaidia Tusimame Tena kwa Miguu Yetu

TUNAWEZA kutiwa nguvu wakati tunafikiria somo yenye tunapata mu maono ya kushangaza yenye kuwa mu Ezekieli 37:1-14. Kila mutu anaweza kutumia ile somo mu hali zenye zinaweza kumupata. Ni somo gani?

Wakati fulani, kwa sababu ya mikazo ya maisha na mahangaiko, tunaweza kujisikia kuwa wenye kulemewa sana na kuchoka, na inaweza kuwa nguvu kusonga mbele. Lakini mu hali kama ile, tunaweza kutiwa nguvu wakati tunafikiria maono yenye kuchochea ya Ezekieli kuhusu kurudishwa kwa watu wa Mungu mu hali ya muzuri. Juu ya nini tunasema vile? Juu, kupitia hii unabii tunajifunza kama Mungu, mwenye iko na nguvu ya kutia pumuzi ya uzima mu mifupa yenye kufa, anaweza kabisa kutupatia nguvu yenye tuko nayo lazima juu tushinde magumu​—hata ile yenye inaonekana ku macho ya wanadamu kuwa nguvu kupambana nayo.​—Soma Zaburi 18:29; Flp. 4:13.

Kumbuka kwamba miaka mingi mbele ya siku za Ezekieli, nabii Musa alisema kwamba Yehova iko na nguvu lakini pia iko na nia ya kutumia ile nguvu ili kusaidia watu wake. Musa aliandika hivi: “Mungu ni kimbilio tangu nyakati za zamani, mikono yake ya milele iko chini yako.” (Kum. 33:27) Tunaweza kuwa hakika kwamba, kama tunamulilia Yehova Mungu wetu wakati wa magumu, atatia mikono yake yenye upendo chini yetu, atatuinua kwa upole, na atatusaidia tusimame tena kwa miguu yetu.​—Eze. 37:10.